EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, September 30, 2015

FC PORTO YAITWANGA CHELSEA 2-1



PORTO (4-1-4-1): Casillas 6; Pereira 6, Maicon 7, Marcano 6.5, Indi 6.5 ; Danilo 6; Andre 7.5 (Layun 80), Neves 7 (Evandro 78), Imbula 7.5, Brahimi 8 (Osvaldo 87); Aboubakar 7.
Subs not used: Helton, Bueno, Corona, Tello
Goals: Andre 39, Maicon 52 
Booked: Indi, Marcano, Imbula, Pereira
Manager: Julen Lopetegui 8

MASIKINI ARSENAL, YAPIGWA NA OLIMPIAKOS 2-1 IKIWA NYUMBANI, YASHIKA MKIA KUNDI F


ARSENAL (4-2-3-1): Ospina 4, Bellerin 6.5 (Campbell 86, 6), Gabriel, 6.5, Koscielny 6 (Mertesacker 57, 6), Gibbs 6, Coquelin 6 (Ramsey 60, 6), Cazorla, 6.5, Oxlade-Chamberlain 7, Ozil 6.5, Sanchez 8, Walcott 8
Subs not used: Cech, Debuchy, Monreal, Chambers
Goals: Walcott 35, Sanchez 65 
Booked: Gabriel, Ozil, Sanchez 
Manager: Wenger 5 

OLYMPIACOS (4-1-4-1): Roberto 7.5; Elabdellaoui 7.5, Botia 8, Siovas 8, Leandro Salino 7; Cambiasso 8.5; Pardo 8, Kasami 8, Fortounis 7.5 (Vouras 87), Seba 7.5 (Hernani 73); Ideye 6.5 (Finnbogason 46, 7)
Subs not used: Kapino, Dominguez, Pulido, Masuaku
Goals: Pardo 33, Ospina (OG) 40, Finnbogason 66 
Booked: Roberto, Finnbogason, Fortounis, Cambiasso
Manager: Silva 8
MOM: Cambiasso 
Player ratings by Sami Mokbel

NYOSSO AFUNGIWA KUCHEZA SOKA MIAKA MIWILI, APIGWA FAINI YA NOTI NOTI 200 ZA SH 10,000

Kikao cha Kamati ya nidhamu ya TFF kilichokutana ndani ya saa 72, kimefungia nahodha wa Mbeya City, Juma Said Nyosso kucheza soka kwa miaka miwili.

Pamoja na miaka hiyo miwili, Nyosso ametozwa faini ya Sh milioni mbili kutokana na kitendo chake cha kumshika makalio nahodha wa Azam FC, John Bocco.


Hii ni mara ya pili kwa Nyosso kushiriki katika tukio, mara ya kwanza alimtomasa Elius Maguli wakati akiichezea Simba.

CCM walaani wafuasi wa Ukawa kufanya fujo kwenye ofisi zao Tanga

January MakambaMjumbe wa Kamati ya Kampeni ya CCM, January Makamba.
Chama cha Mapinduzi kinasikitishwa na kitendo cha wafuasi wa vyama vinavyounda UKAWA kupiga mawe na kutupa chupa, baadhi zikiwa na mikojo, kwenye Ofisi ya CCM Mkoa wa Tanga jana, tarehe 28 Septemba 2015, kabla na baada ya mkutano wao wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Tangamano, Tanga Mjini.
Kama ilivyo kawaida yetu miaka yote, CCM iliazimia kufanya kampeni za amani, zinazoheshimu sheria za nchi na utu wa wapinzani wetu. Hadi sasa, tumeweza kuwadhibiti wapenzi, washabiki na wanachama wa CCM wasifanye vitendo vya ufunjifu wa amani.
Tukio la Tanga sio la kwanza. Tarehe 27 Septemba 2015 viongozi wa UKAWA waliwapanga vijana, katika eneo la stendi ya Uyole, mkoani Mbeya ili wasimamishe msafara wa Mgombea wa Urais wa CCM na kumfanyia vurugu na kumpigia kelele ili wananchi wasimsikie vizuri. Ingawa Mgombea wetu alifanikiwa kukabiliana na hali hiyo, tunaamini kwamba huu sio ustaarabu.
Washabiki wa CCM pia wana uwezo wa kupanga na kufanya mambo haya, tena kwa ufanisi mkubwa zaidi. Lakini viongozi wa CCM wa ngazi zote wamekuwa wanawahimiza wasifanye mambo haya kwasababu CCM hatuamini kwamba hiyo ni njia sahihi ya kuomba ridhaa ya Watanzania kuliongoza taifa letu na pia, kwa kuwa sisi ndio tuliokabidhiwa na Watanzania nchi hii kuiongoza, tunafahamu dhamana yetu kubwa ya uongozi wa taifa na ulinzi wa amani ya taifa letu.

Bela atafuta kiki kwa picha za utupu

ISABELA-(1)
Miss Ruvuma 2006, Isabela Mpanda.
KATIKA kile kinachoaminika kama ni kutafuta kiki, Miss Ruvuma 2006, Isabela Mpanda amepiga picha za utupu na kuzitupia katika mitandao ya kijamii akiwa katika pozi mbalimbali.
Rafiki yake mmoja (jina linahifadhiwa) aliyelinyetishia gazeti hili kuhusu uwepo wa picha hizo, alisema kwa jinsi picha hizo zilivyo ni wazi kuwa endapo sheria ya mtandao itafanya kazi yake, basi mrembo huyo atakuwa matatani.
Gazeti hili lilipowasiliana na Isabela baada ya kuziona picha hizo na kutaka kujua jinsi atakavyoshughulika na sheria ya makosa ya mtandao alisema; “Picha siyo kitu cha kunifanya nishtakiwe kwa sababu simtukani mtu, wala mavazi yangu siyo sababu ya kuchukuliwa hatua labda wanaopitia sheria hii wawe hawana kazi ya kufanya.”

Zari atumika kumdhalilisha Wema! Kisa kuzaa na Diamond

zarinah
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, akiwa na mpenzi wake Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’
Mwandishi wetu
WATU wabaya! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia watu wanaoasadikiwa kuwa ni wafuasi wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, kutumia jina na picha ya mwandani wa sasa wa staa huyo, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kumdhalilisha mpenzi wa zamani wa Diamond, Wema Sepetu ‘Madam’, Risasi Mchanganyiko lina mchapo kamili.
Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku chache tangu Zari, ambaye ni mjasiriamali maarufu aliyemzalia Diamond, amfanyie mwanaye Latiffah ‘Tiffah’ sherehe ya kumtoa nje kwa mara ya kwanza (Arobaini).
ZARI (1)
Nasibu Abdul ‘Diamond’.
KIINI CHA UDHALILISHAJI
‘Kirusi’ wa kwanza kuanzisha udhalilishaji huo alijitambulisha katika mtandao wa Instagram kwa jina la Who is Boss ambapo aliweka picha inayomuonyesha Zari akiwa amembeba mtoto wake na Wema akiwa amembeba mbwa kisha kusindikiza ujumbe uliosomeka:
“Ukibeba mimba utalea mtoto na ukitoa mimba utalea mbwa.”
TIMU DIAMOND ZAMSHAMBULIA WEMA
Mara baada ya Who is Boss kuweka picha na ujumbe huo, wafuasi wa Diamond (Team Diamond) walianza kumshambilia Wema kwa kumkejeli na kumtukana matusi mazito yasiyoandikika gazetini.
Wafuasi hao walimtuhumu Wema kuwa alichezea ujana kwa kutoa mimba matokeo yake kwa sasa analea mbwa wakati mwenzake Zari ametumia ujana wake vizuri na ndiyo maana amemzalia Diamond.
wema (3)
Wema Sepetu ‘Madam’.

Jayjay nimeumizwa na mapenzi!

janethMAUMIVU niache! Msanii wa filamu ya Who Is My Child, Janeth Jackson ‘Jayjay’ amekiri kuumizwa na kulizwa na mapenzi mara kwa mara licha ya kuwa na muonekano wenye mvuto machoni kwa wanaume jambo linalomnyima amani ya maisha.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, Jayjay alisema si rahisi kwa watu kuamini ukweli huo kutokana na uzuri wake wa umbo na sura, lakini ukweli ni kwamba hana furaha juu ya mapenzi kufuatia wanaume wengi kumtumia kisha kumkimbia bila kutimiza ahadi zao.
“Sina furaha na mapenzi, nimeumizwa sana na wanaume kila anayekufuata anakuahidi mambo mengi lakini akishatimiza haja zake anakimbia, kwa sasa sitaki tena mapenzi,” alisema Jayjay na kuongeza kuwa sasa anataka kujikita zaidi katika kazi.

Ndoa ya wastara, bond baada ya uchaguzi

WASTARA2GSASA imethibitika kuwa ndoa kati ya muigizaji nyota wa filamu Wastara Juma na Mtangazaji Bond Suleiman itafanyika mara baada ya uchaguzi mkuu ujao.
WASTARA-43Bond ambaye pia ni muigizaji, aliliambia gazeti hili kuwa wawili hao wameshafikia muafaka wa kuoana lakini Wastara yupo bize na kampeni, kwani baada ya kuanguka katika ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya CCM, sasa anazunguka mikoani na Samia Suluhu ambaye ni mgombea mwenza wa John Magufuli jambo ambalo limesababisha washindwe kufanya maandalizi.
“Unajua Wastara amejiingiza kwenye siasa na mimi nataka akomae kwani itakuja kutusaidia baadaye ndiyo maana tumekubaliana kuahirisha ndoa mpaka uchaguzi uishe ndipo tutapanga tena,” alisema.

Monday, September 21, 2015

MABASI 138 YA BRT YATUA DAR


Sehemu ya mabasi 138 ya Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) yaliyowasili katika Bandari ya Dar es Salaam, kwa ajili ya kuanza kutoa huduma ya usafiri katika kipindi cha mpito kwenye miundombino ya mfumo wa mabasi yaendayo haraka (BRT)kuanzaia mwezi ujao.

Mkuu wa Mkowa Dar es Salaam, Bw. Saidi Meck Sadiki akijaribu basi la Mradi wa Mbasi Yaendayo Haraka (DART), alipofanya ziara katika Bandari ya Dar es Salaam kujionea kuwasili kwa Mabasi 138 ya Mradi huo ambayo mwezi ujao yataanza kutoa huduma ya usafiri jijini Dar es Salaam katika Kipindi cha mpito

Mkuu wa Mkowa Dar es Salaam, Bw. Saidi Meck Sadiki akishuka katika basi la Mradi wa Mbasi Yaendayo Haraka (DART), alipofanya ziara katika Bandari ya Dar es Salaam kujionea kuwasili kwa Mabasi 138 ya Mradi huo ambayo mwezi ujao yataanza kutoa huduma ya usafiri jijini Dar es Salaam katika kipindi cha mpito.
Mabasi 138 ya Mwendo Kasi (BRT), yamewasili katika Bandari ya Dar es Salaam kutoka nchini China. Kuwasili kwa mabasi hayo kutasaidia kupunguza tatizo la usafiri katika Jiji la Dar es Salaam. 
 
Katika Bandari ya Dar es Salaam kutoka China tayari kwa huduma ya usafiri. Mkuu wa Mkoa  wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, aliwaambia waandishi wa habari jana baada ya kufanya ziara katika Bandari ya Dar es Salaam kujionea kuwasili kwa mabasi hayo.
 

Global TV Online: Hatimaye hii ndiyo sura ya mtoto wa Diamond

MAGUFULI AFUNIKA CHATO JANA

 Maelfu wa wakazi wa Chato wakisikiliza kwa makini sera za Mgombea Urais kupitia CCM, John Magufuli.
Wakazi wa Chato wakionesha mabango yao mbalimbali.
Nyomi ya wanachama wa CCM kama inavyoonekana leo hii huko Chato.
Msanii wa Bongo Fleva, Madee akitoa burudani kwa wakazi wa Chato.

AUNT: NINGETAKA MTOTO MWEUPE, NINGEZAA NA MZUNGU

Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel akiwa na mzazi mwenzie pamoja na mtoto wao.
Imelda mtema
Sawasawa! Katika kuonesha kuwa amechoshwa na manenomaneno, staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel ameliambia Ijumaa Wikienda kuwa watu wanaosema mwanaye Cookie ni mweusi ndiyo maana hamuoneshi, hawapo sawa kwani angetaka mtoto mweupe angezaa na Mzungu.
Akizungumza na gazeti hili wikiendi iliyopita, Aunt alisema kuwa kuna watu hawana kazi za kufanya bali kufuatilia maisha ya watu kila siku bila sababu za msingi kwa maana kumuonesha mtoto wake ni hiari yake na si kwa ajili ya watu.
“Hivi mpaka nilivyoamua kuzaa na Moo (Moses Iyobo), si nilimuona ni mweusi? Sasa kwa nini watu wanachonga, eti simuoneshi Cookie kwa vile ni mweusi, ningetaka mtoto mweupe si ningemtafuta Mzungu nizae naye?” aliwaka Aunt.

Friday, September 11, 2015

Sheikh Abubakari Zuberi achaguliwa rasmi kuwa Mufti Mkuu wa Tanzania


Baraza Kuu la Waislamu nchini umemchagua aliyekuwa Kaimu Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuberi Bin Ali, kuwa Sheikh Mkuu wa Tanzania.
Sheikh Zuberi amepita bila kupingwa baada ya mpinzani wake Sheikh Ally Muhidin Mkoyogole kuamua kujiondoa katika kinyang'anyiro hicho.
Akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti mstaafu wa Halmashauri Kuu ya Bakwata, Alhaji Ndassiwa amesema majina mawili yaliyotoka kwenye Baraza la Ulamaa yalikuwa ni ya Sheikh Ally Muhidini Mkoyogole na Sheikh Zubeiri.
Mara baada ya uchaguzi huo Sheikh Zuberi mbali na kuwashukuru washiriki wa mkutano huo, amewataka Watanzania kumtanguliza Mungu ili awapatie kiongozi bora katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Hospitali ya Mkoa wa Singida yakabiliwa na uhaba wa Mashuka na Magodoro, Wagonjwa watumia mashuka yao


SHUGHULI za utoaji tiba katika Hospitali ya mkoa wa Singida zimezorota kutokana na kuibuka kwa utata wa matumizi ya shuka za wagonjwa ambapo wagonjwa wanaolazwa kutumia mashuka wanayoyatoa majumbani kwao na kujifunika bila kuyafanyia usafi suala ambalo ni kinyume na taratibu na kanuni za afya.
Tangu ilipoanza kutoa huduma hospitali hiyo na tangu kuanzishwa kwake ilikuwa mkombozi wa huduma za afya kwa wananchi wa Wilaya zote za mkoa huo na zile zinazozunguka mkoa huo kwa upande wa Singida Kaskazini na Mashariki ambapo wananchi wake kwa sasa wanalazimika kufuata huduma hiyo umbali mrefu, ikiwemo katika Hospitali ya mkoa wa Dodoma au kutumia Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Gaspa iliyopo Itigi.
Wagonjwa wanaolazwa katika hospitali hiyo wanaelezwa kuwa hatarini kupata maambukizi ya magonjwa mengine kutokana na kutumia mashuka hayo na uhaba wa magodoro.
Mtaalamu mmoja wa afya hospitalini hapo (jina linahifadhiwa) anasema wanajikuta katika mateso makubwa kutokana na kile alichokieleza kuwa ni uzembe wa dhahiri wa Serikali na wataalamu wenzake kwa kukubali hospitali hiyo kuendelea kutoa huduma tangu awali badala ya kuifunga ili Serikali itoe mashuka na huduma nyingine zinazohitajika.
Muuguzi huyo amebainisha kuwa hata hivyo kwa muda mrefu Hospitali hiyo imejikuta katika msuguano wa chini kwa chini na Ofisi ya Mganga Mkuu wa hospitali hiyo ambayo ilikuwa inataka vifaa hivyo viombwe kwa watu na mashirika mbalimbali ili vipelekwe kabla ya mwezi wa Aprili, 2015 na kuwa chini ya usimamizi na uangalizi wao lakini hadi sasa hakuna jitihada za kuridhisha zinazofanywa ili kutatua tatizo hilo.
Aidha, amesema hali hiyo inatokana na hospitali hiyo kuwa na mashuka 230 pekee kati ya 2,500 yanayohitajika, kiwango ambacho ni chini ya mahitaji hivyo kuulazimu uongozi kutoa ruksa kwa kila mgonjwa anayelazwa kwenda na shuka lake licha ya kuwa hakuna kanuni za kusimamia mashuka hayo.
Kutokana na sakata hilo, baadhi ya wagonjwa mbalimbali wanaotibiwa katika hospitali hiyo ya mkoa akiwemo Frida James (49), ambao ni wagonjwa wa kawaida na wale waliopatiwa rufaa kutoka kwenye Vituo vya Afya Vijijini, Zahanati pamoja na maeneo mengine jirani na nje ya mkoa huo wa Singida amesema baada ya kutumia mashuka hayo yanafuliwa na ndugu zao.
Ameeleza kuwa wakipata ahueni na kuruhusiwa kwenda makwao, baadhi yao wanaacha mashuka hayo hospitalini kwa kuhofia usalama wa afya zao na wengine huondoka nayo.
Mmoja wa wananchi mkoani humo aliyejitambulisha kwa jina moja la Juma, akizungumzia tatizo hilo alieleza kuwa hatua ya kukosekana kwa huduma muhimu ikiwemo ya malazi ni kuwavunja moyo wagonjwa walioandikiwa rufaa ya kutibiwa katika hospitali hiyo na wengine wanaohitaji matibabu.
Naye kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Daniel Tarimo, ameieleza FikraPevu kwamba licha ya jukumu la kuokoa maisha ya wagonjwa, lakini kuna hatari inayotokana na uhaba mkubwa wa mashuka kwa kipindi cha muda usiopungua miezi minne.
Mbali na kukiri hospitali hiyo kukabiliwa na changamoto mbalimbali amesema yeye kama mtaalamu wa afya, wanaotambua kuwa hali hiyo ni hatari kwa wagonjwa wanaotumia mashuka ya nyumbani, huku akiongeza kuwa uongozi wa hospitali haina njia nyingine ya kutatua tatizo hilo wakati wakisubiri kupatiwa msaada na Serikali ili kukubalina na hali halisi.
Hata hivyo, amesema hospitali hiyo pia inakabiliwa na tatizo la uhaba wa magodoro kwa zaidi ya asilimia 75 kwani yaliyopo ni 36 tu kati ya magodoro 230 yanayotakiwa ili kukidhi mahitaji ya wagonjwa wanaolazwa hospitalini hapo.
Kwa muda mrefu hospitali za Serikali nchini zikiwemo zile za Rufaa, zimekuwa zikilalamikiwa na wadau mbalimbali kuwa hatua ya kukosa huduma muhimu ikiwemo ufinyu wa bajeti, kukosekana kwa vyumba vya kuhifadhia maiti vyenye majokofu (Nyingine hazina), ukosefu wa dawa na mengineyo ni moja ya changamoto kubwa inayopigiwa kelele na Watanzania kila kukicha.
Taarifa zinaonyesha kwamba, ukosefu wa huduma hizo hupelekea wananchi kujiingiza katika kundi la ununuaji holela wa dawa katika maduka maalumu yanayouza dawa hizo na kudidimiza Aaya zao.
Mara nyingi matumizi ya dawa muhimu zijulikanazo kama vijiuasumu au ‘antibayotiki’ zinazopatikana kwenye maduka ya dawa muhimu lakini zisipotumiwa ipasavyo, vinadhuru afya ya mgonjwa kutokana na mazoea ya kutumia dawa pasipokuwa na cheti cha mtibabu kutoka kwa daktari. Uuzaji wa dawa za binadamu kwa njia hiyo unatajwa kama njia moja wapo ya wafamasia kujipatia kipato.
Awali, gazeti hili mtandao la FikraPevu mwezi Februari, 2015 liliripoti taarifa iliyohusu hatua ya kuchelewa kutekelezwa kwa mpango wa Serikali unaotaka dawa zote zinazonunuliwa na kusambazwa na Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kuwekwa lebo ya utambuzi kwa lengo la kudhibiti wizi wa dawa hizo unaofanywa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu, na jinsi unavyoneemesha wamiliki wa maduka ya dawa nchini pamoja na kusababisha wananchi kuendelea kukosa huduma katika hospitali za umma.
CHANZO; FIKRA PEVU

Friday, September 4, 2015

Mkuu wa Mkoa Dar aonya watakaoleta vurugu



Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki, amesema kwamba serikali ina taarifa kwamba kuna kundi la vijana ambalo litafanya vurugu wakati huu wa kampeni za uchaguzi na siku ya uchaguzi.
 
Hata hivyo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limesema halina taarifa zozote kuhusu vurugu hizo.
 
Sadiki alitoa taarifa hiyo jana katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, katika viwanja vya Mbagala Charambe jimbo la Mbagala.
 
Kada huyo wa CCM ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam, alipanda jukwaani na kuwahutubia wananchi waliokusanyika kumsikiliza Samia ikiwa siku ya kwanza ya kampeni za chama hicho katika Mkoa wa Dar es Salaam.
 
Hata hivyo, Sadiki hakufafanua vijana hao wameandaliwa na nani wala maeneo waliyoko. Pia hakueleza kama ni kutoka vikundi vya uhalifu wala vyama vya siasa zaidi ya kusema kuwa wameandaliwa kufanya fujo. 
 
POLISI WASEMA HAWANA TAARIFA
Alipotafutwa  Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, kuzungumzia suala hilo alisema hawezi kulizungumzia kwa kuwa bado hajapatiwa taarifa na kuahidi kuwa atakapopatiwa taarifa, atalitolea ufafanuzi.
 
“Sijaisikia hilo suala, siwezi kulizungumzia mpaka nitakapopata taarifa nitaliongelea,” alisema Kamanda Kova.
 
Kamanda Kova alisema ni vyema atafutwe Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke ili alitolee ufafanuzi.
 
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida, alisema wanawake na vijana wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo ukosefu wa ajira.
 
Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgombea mwenza,  alisema CCM inajua changamoto hizo na kwamba mgombea mwenza akiingia Ikulu atazitatua akishirikiana na mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli.
 
SAMIA AMWAGA AHADI MBAGALA
Akizungumza na wananchi wa jimbo la Mbagala, Samia alisema Mbagala siyo kituo cha utalii ambacho wanasiasa wanaweza kwenda na kupiga picha.
 
Alisema atahakikisha anatatua kero ya foleni ya magari ikiwamo kujenga barabara ya Mbagala hadi Kongowe.
 
Pia, aliahidi kujenga soko katika eneo la Temeke pamoja na Kijichi ili kutoa nafasi 5,000 kwa wafanyabiashara kufanya biashara.
 
Kuhusu usumbufu kwa wafanyabiashara  ndogo ndogo jijini Dar es Salaam, alisema hakuna mtu atakayebughudhiwa ikiwamo kulipishwa kodi zinazoleta usumbufu.
 
Aliahidi kuwaunganisha wafanyabishara katika benki mbalimbali ili wapatiwe mikopo ya kuanzisha na kuendeleza biashara.
 
Akizungumzia tatizo la ukoesfu wa maji, Samia alisema katika Jiji la Dar es Salaam kero hiyo itamalizika haraka watakapoingia Ikulu.
 
Samia alisema asilimia 30 ya tenda zote za halmashauri watahakikisha zinatolewa kwa wananchi wa kawaida ambao wananishi katika eneo husika.
 
Akizungumzia msongamano, Samia alisema tatizo hilo litaisha haraka watakapoingia Ikulu kwa kuwa watajenga barabara za juu pamoja na kusimamia usafiri wa reli.
 
MGOMBEA UBUNGE
Akizungumza katika mkutano huo, mgombea wa ubunge wa Jimbo la Mbagala (CCM), Issa Mangungu, alisema jimbo hilo linakabiliwa na uhaba wa vifaa vya ujenzi ukiwamo mchanga.
 
Kuhusu tatizo la barabara, Mangungu aliomba kujengwa njia mbili kutoka Mbagala hadi Kongowe ili kumaliza kero hiyo.
 
MGOMBE UDIWANI
Mgombea udiwani katika Kata ya Kilungule, Said Fela maarufu kama mkubwa Fela, alisema anajua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi.
 
Fela ni mmmiliki wa bendi maarufu ya Yamoto ambayo imepata umaarufu kwa makundi yote wakiwamo wanawake na vijana.
CHANZO: NIPASHE

Masaburi aibuka sakata la vijana kuandamana

  Polisi wafanya upelelezi kubaini ni wa chama gani.
Mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Didas Masaburi.
Mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Didas Masaburi (pichani), amekanusha taarifa za kufadhili vijana wanaodaiwa kuandamana wakipinga aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuondoka ndani ya chama hicho. 
 
Dk. Masaburi alikanusha taarifa hizo jana wakati akizungumza na  waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusiana na uvumi uliozagaa kwenye mitandao ya jamii kuwa vijana 10 wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa sababu ya kuandamana bila ya kibali wakimtaka Dk. Slaa asiondoke kwenye chama hicho walitumwa na yeye.
 
“Tuhuma hizo si za kweli, hata kama ninaunga mkono hoja zilizotolewa na Dk. Slaa kuhusiana na tuhuma za ufisadi dhidi ya viongozi waliohamia Chadema kutoka CCM, lakini siwezi kufadhili maandamano ya wanachama wa Chadema ya kushinikiza  kubakia kwa Dk. Slaa ndani ya chama hicho,” alisema.
 
Alisema vijana aliowapokea katika ofisi ya CCM Jimbo la Ubungo zilizoko Manzese juzi baada ya kurudisha kadi za vyama vyao kikiwamo cha Chadema walifanya hivyo kwa mapenzi yao wakisema wamechoshwa na hadaa katika vyama walivyotoka. Aidha, Dk. Masaburi aliwataka viongozi wa Chadema kujibu hoja zilizotolewa na Dk. Slaa badala ya kutafuta mchawi baada ya kuona amewaumbua na wanachama wao wanakihama chama hicho.
 
Wakati huohuo, Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni, jijini Dar es Salaam limesema linaendelea na upelelezi ili kubaini vijana walioandamana juzi eneo la Morocco, jijini humo iwapo ni wanachama wa Chadema au  la.
 Juzi vijana takribani 100 wanaodaiwa kuwa wanachama wa Chadema waliandamana katika eneo hilo wakishinikiza kurudi katika chama hicho kwa aliyekuwa  katibu mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa, ambaye alitangaza kujitoa na kujitenga na siasa, huku  akimtuhumu mgombea urais wa chama hicho, Edward Lowassa, masuala mbalimbali ua ufisadi.
 
Kamanda wa Polisi wa kanda ya Kinondoni, Camilius Wambura kupita msaidizi wake, jana aliliambia Nipashe kuwa bado wanawashikilia vijana 10 kati ya 100 ambao walitawanywa kwa mabomu ya machozi baada ya kukaidi amri ya jeshi hilo ya kutakiwa kutawanyika, huku wakiendelea na upelelezi kubaini wanatoka chama gani.
CHANZO: NIPASHE

Kampeni Ukawa sasa kwa chopa.

Wakati kampeni za mgombea urais wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kupitia Chadema zikiingia siku ya sita, chama hicho kimetangaza kuanza kampeni zake kwa kutumia helikopta (chopa) nne ambazo zitatikisa anga katika mikoa yote nchini kuomba ridhaa ya wananchi kukichagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
 
Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, akiwahutubia maelfu ya wananchi, alisema kwa sababu Chadema imejipanga kushinda uchaguzi na usalama ni kazi ambayo ni ya wote.
 
Alisema Tanzania nzima kuna majimbo ya uchaguzi 265 ambako Zanzibar yako 50 na Tanzania Bara 215.
 
Aliongeza kuwa siku za kampeni ni siku 60 mgombea urais Ukawa hawezi kufikia majimbo yote hivyo Chadema imeunda vikosi vinne vya askari wa mapambano ambavyo vitaundwa na wabunge makini na baadhi ya viongozi ambao watafanya kampeni nchi nzima kwa kutumia helikopta nne.
 
Aliwataja wabunge hao watakaounda kikosi hicho wanaomaliza muda wao kuwa ni Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Ezekiel Wenje (Nyamagana), David Silinde (Momba), Joseph Mbilinyi maarufu Sugu (Mbeya Mjini), John Mnyika (Ubungo), Halima Mdee (Kawe) na yeye (Mbowe) ambaye ni wa Hai.
 
“Vikosi hivi vitachana nchi nzima kwa kutumia helikopta kuanzia wiki ijayo, hivyo majimbo ambayo mgombea urais hatafika vikosi vitafika na maeneo mengine atakwenda mgombea mwenza,”alisema.
 
Mbowe alisema CCM wameshakuwa laini kama maini hivyo katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ni lazima wataondoka madarakani.  
CHANZO: NIPASHE

SLAA NI SHUJAA WA TAIFA

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dokta Wilbroad Slaa.
Na Amran kaima
HOTUBA ya kwanza tangu ‘atoweke’ kwenye anga za siasa ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dokta Wilbroad Slaa, aliyoitoa juzi Jumanne juu ya kujiweka pembeni, imepokelewa kwa hisia tofauti huku wengi wakimuita kuwa ni shujaa wa taifa kutokana na ujasiri wake, Ijumaa lina kila kitu.
Katika mahojiano yaliyowahusisha wananchi na wachambuzi mbalimbali wa mambo ya kisiasa kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mara baada ya kiongozi huyo kukutana na waandishi wa habari, waliliambia Ijumaa kuwa, Dokta Slaa ni mtu wa aina yake ambaye taifa halijapata kuwa naye tangu kuondoka kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Mwenyekiti wa Chadema na Mbunge wa Hai, Mhe. Freeman Mbowe.
Ana msimamo
Wengi walionesha kufurahishwa na misimamo ya kiongozi huyo tangu ajiingize kwenye masuala ya siasa, kwani siku zote amekuwa mstari wa mbele kuwatetea wanyonge, kuanika maovu na kukemea kila analoliona lipo tofauti na anavyoamini.
“Kwa kweli mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Dk. Slaa ni kati ya viongozi wenye msimamo asiyekubali kuyumbishwa. Amekuwa hivyo tangu nilivyomjua na hata hotuba yake aliyoitoa juzi, inadhihirisha hilo,” alisema Chande Juma wa Kinondoni jijini Dar.
Alisema kama mtu alifuatilia vizuri mazungumzo yake, ni wazi kuwa viongozi wenzake walikubali kubadili msimamo ili kumwezesha Lowassa aingie Chadema, lakini yeye akakataa licha ya kamati ndogo kuundwa ili imshawishi alegeze msimamo.
Mgombea urais kupitia Chadema(Ukawa) Edward Lowassa.
Rushwa ni adui mkubwa kwake
Mchambuzi mmoja wa habari za siasa aliyeomba hifadhi ya jina lake, alisema siku zote anamtambua Dk. Slaa kama mtu mwenye kuichukia rushwa, kwani anaamini hicho ndicho chanzo cha matatizo yote yanayosababisha kero za wananchi kutoisha, licha ya nchi kuwa na rasilimali za kutosha.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate