EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, May 30, 2015

MABESTE CHARITY SHOW KUHAMIA TEGETA

Pam Daffa.
Venance Mabeste 'Mabeste'.
BAADA ya kufanya shoo maalum ya kuchangia matibabu kwa mkewe, Lisa Karl Fickenscher, staa wa Hip Hop Bongo, Venance Mabeste ‘Mabeste’ anatarajiwa kuiendeleza shoo hiyo tena Jumapili hii ndani ya Club 71, Kibo Complex jijini Dar.

WAUMINI: MAPADRI WARUHUSIWE KUOA

Mwandishi wetu
Mpasuko! Kufuatia kuibuka wimbi la kashfa za ngono zinazowagusa waseja wa daraja la upadri duniani, baadhi ya waumini wa madhehebu mbalimbali yakiwemo Katoliki na Anglikana, wameibuka na kudai kuwepo kwa marekebisho ya sheria ya makanisa hayo yanayoruhusu watumishi hao kuoa kwani kwa sasa wanayaaibisha, jambo ambalo linaharibu imani juu ya Ukristo.
Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo.
NINI KIMETOKEA?
Hayo yanakuja kufuatia tukio la hivi karibuni la kunaswa kwa Padri Anatoly Salawa ambaye ana cheo cha Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference, Tec) aliyekutwa na mrembo vichakani.
Father Salawa alinaswa na mrembo huyo vichakani ndani ya gari maeneo ya Kurasini jijini Dar.
Mbali na tukio hilo, pia yapo matukio mengine ya mafumanizi likiwemo lile la Father Urbanus Ngowi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi aliyefumaniwa ‘laivu’ na mke wa mtu aliyetajwa kwa jina la mama P.

WEMA, IDRIS NUSU WAZICHAPE

Musa mateja
MALKIA anayemiliki Kampuni ya Endless Fame Production, Wema Isaac Sepetu na Mshindi wa Big Brother Africa 2014/15, Idris Sultan ambao wamekuwa marafiki wakubwa katika siku za hivi karibuni, nusu wazichape kavukavu baada ya kupishana kauli huku wivu wa kimapenzi ukitajwa.
Malkia anayemiliki Kampuni ya Endless Fame Production, Wema Isaac Sepetu.
Tukio hilo lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita nje ya Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kilimanjaro iliyopo Posta jijini Dar ambapo kwa pamoja walikuwa wamehudhuria sherehe ya utoaji Tuzo za Watu.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tafrani ya wawili hao kutaka kukunjana ilitokea baada ya kumalizika kwa shuguli hiyo ambapo Idris alimpora Wema tuzo yake aliyoshinda na kwenda nayo kwenye gari lake.
Ugomvi huo ulipamba moto na kusababisha watu waliokuwa wakiwashuhudia kutaharuki ambapo Wema alikwenda kwenye gari lake lililokuwa likiendeshwa na Petit Man lakini Idris alimfuata akionekana kumuonea wivu na kumtaka apande gari lake waondoka jambo ambalo Wema alilitolea nje na kumfungia kioo.
Mshindi wa Big Brother Africa 2014/15, Idris Sultan.
Baada ya kuona Wema amemtolea nje, Idris alikwenda kwenye gari lake na kuliegesha mbele ya gari la Wema ‘kum-block’ ili asiondoke ambapo alishuka na kumwambia Petit Man ahakikishe anamfuata kwa nyuma jambo ambalo Petit Man alishindwa kulitekeleza baada ya Wema kukataa.
Baada ya kushuhudia vurugu hizo, mwanahabari wetu alimfuata Wema ili kujua kilichotokea ambapo mwanadada huyo alisema kuwa haelewi ni kitu gani ambacho kilimkuta Idris siku hiyo maana kama angekuwa anakunywa pombe, angesema labda alizidiwa lakini kwa kilichotokea hadi leo hajui ni kipi kilimkuta.
Wema Isaac Sepetu akiwa na Idris Sultan.
“Yaani hata sielewi Idris alifikwa na nini maana amefanya mambo ya ajabu sana na mara ya kwanza nilijua utani lakini nilimshangaa zaidi baada ya kukomaa hadi kufikia hatua ya kuni-block na gari lake huku akitaka niondoke naye wakati kila mtu alikwenda pale kimpango wake.“Mimi nadhani kuna utoto fulani bado anao na unamsumbua,” alisema Wema lakini Idris hakupatikana kusema chochote.

Friday, May 29, 2015

SKYLIGHT BAND NDIO HABARI YA MUJINI KWA SASA, KARIBUNI KIWANJA KIPYA CHA LUKAS PUB TUSEBENEKE LEO‏

Skylight Band ni mwendo wa kutoa raha sana tukutane Ijumaa hii ndani ya kiota cha Lukas Pub Masaki jijini Dar kwa kuburudika na band hii
Waimbaji wa Skylight Band wakiendelea kutoa burudani ya kukata na shoka kwenye stageni na moja ya nyimbo zao
Joniko Flower naye katika muziki wa live hashikiki kwa sauti,viuno mpaka pumzi ni hatareeeee
KUNAKO Nigeria Flavour….. Sam Mapenzi akitoa burudani huku akisindikizwa na wanamziki wenzake waliokuwa wakimpa support ya nguvu kwenye ngoma za Nigeria ambao ni Joniko Flower (wa kwanza kushoto), Ashura Kitenge(wa pili kutoka kulia) pamoja na Sony Masamba.
Watu navipaji vyao sasa team sky light band ikiongozwa na Ashura Kitenge katika miondoko ya zouk huku akisindikizwa na waimbaji wenzake katikaka,Sony Masamba pamoja na AK 47 meneja wa sky light band
sakata lumba na sky light band hapana chezea hatareee ukigusa lazima unase

Ngassa azuiwa kucheza Sauz


 
Mshambuliaji wa Free State Stars ya Afrika Kusini, Mrisho Ngassa.
Sweetbert Lukonge, Dar es Salaam
UNAWEZA kusema kitumbua kimeingia mchanga! Uamuzi wa kumzuia mshambuliaji Mrisho Ngassa kuitumikia klabu yake mpya ya Free State Stars ya Afrika Kusini, utapitishwa ndani ya siku chache.


Taarifa za uhakika zinaeleza, Ngassa hataruhusiwa kucheza nchini Afrika Kusini alikojiunga na klabu hiyo kwa miaka minne kwa kuwa klabu yake ya zamani ya Yanga imeandika barua kutaka uhamisho wake wa kimataifa (ITC) uzuiwe hadi atakapolipa deni linalokadiriwa kufikia Sh milioni 40.

MAINDA: NIMETUMIKA SANA KWA NGONO, POMBE!

STAA mkongwe wa sinema za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ ametoa ushuhuda mzito (confession) baada ya kukiri kuishi maisha ya starehe ikiwemo unywaji pombe na kukosea mwanaume sahihi wa maisha kwa kuingia kwenye uhusiano tofauti jambo aliloliita ni ‘kumtumikia shetani kwa pombe na ngono’.
Staa mkongwe wa sinema za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’.
Akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wetu hivi karibuni katika mahojiano maalum, Mainda ambaye kwa sasa ni mlokole wa ‘tuimbe na kusifu’ aliweka wazi kuwa kipindi cha nyuma, shetani alimzidi nguvu kwa kujichanganya maeneo ya baa na kunywa pombe jambo ambalo kwa sasa kila akikumbuka huishia kusikitika.
Alisema, kwa sasa hana mpenzi na kwamba hatafuti lakini anamngojea yule ambaye anaamini atatoka kwa Mungu kwa wakati muafaka.Mainda aliweka wazi kuwa anamshukuru Mungu kwa kumuongoza katika njia nyoofu huku akiainisha kuwa maisha bila ya kuwa na Mungu ni ya ajabu sana.
“Kwa kweli maisha ya zamani yalikuwa ya ajabu, ulevi wa pombe, kutoka na wanaume tofauti nikidhani ndiye mwanaume sahihi, zilikuwa ni nguvu za shetani, namshukuru Mungu kwa kunibadilisha kwa kiwango hiki kwani nilimtumikia sana ibilisi kwa mambo machafu, viongozi wangu wa dini wananipa mwanga mkubwa mno juu ya Neno la Mungu na kila nikikumbuka maisha ya nyuma, huwa siyatamani kabisa,” alisema Mainda.

SABABU 10 ZA MASTAA WA KIKE KUTODUMU KWENYE NDOA!


Na Hamida Hassan
Mastaa wengi wamekuwa hawadumu kwenye ndoa zao na wengine kwenye uhusiano wao wa kimapenzi. Ukijaribu kumuuliza kijana yeyote mwenye nia ya kuoa atakuambia bora aoe mwanamke wa kawaida kuliko staa.
Mkali katika tasnia ya filamu Bongo, Yobnesh Yusuph 'Batuli'.
Si suala la kuoa tu, hata kwenye mapenzi ya kawaida ni wachache wanaoanzisha uhusiano na mastaa wakiwa na ndoto za kudumu kwa muda mrefu. Ukiona kijana ‘anamsalandia’ staa ujue ni ili amuonje tu kisha amtose.
Pia ukifuatilia utagundua kuwa, mwanamke wa kawaida akitokea kumpenda staa wa kiume, anatafuta ile sifa ya kuwa naye lakini anajua hawezi kudumu naye.Kutokana na hilo sasa, makala haya yanajaribu kukupa kwa ufupi sababu 10 ambazo zinawafanya mastaa wengi wa kike kutodumu kwenye ndoa.
Tamaa
Hili lipo sana kwa mastaa wa kike. Baadhi yao wana tamaa ya kuwa na maisha f’lani ili waonekane nao wamo wakati uwezo haupo. Matokeo yake sasa akiolewa na mwanaume ambaye hana kitu, akimpata wa pembeni ‘pedeshee’ wa kumtunza, kwa tamaa zao hujikuta wakisaliti.
Unakuta msichana kwa kuwa ni staa, anataka awe na gari zuri, abadili nguo kila siku, simu kali na vitu vingine vya thamani wakati pesa hana na mume naye ni kapuku. Hapo ndipo wengi huamua kuchepuka na matokeo yake sasa hajali tena ndoa.

JOKATE: ALI KIBA NI KILA KITU KWANGU

MREMBO mchakarikaji Bongo,  Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, juzikati aliamua kuvunja ukimya na kusema kuwa mwanamuziki Ali Kiba kwa sasa ndiye kila kitu katika mambo yake mengi ya kimaisha.
Mrembo mchakarikaji Bongo,  Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
Akizungumza na Ijumaa Jokate alisema, watu wanaongea sana kuhusiana na ukaribu wao bila kujua kuwa Kiba ni mtu wake kitambo na sasa ndiye kila kitu kwake kwani ana projekti naye kibao ambazo zinakuja na wasioelewa, ipo siku wataelewa.
Mwanamuziki Ali Kiba.
“Yaani watu wangu wajue Kiba ni kila kitu kwangu ila siyo ishu ya mapenzi, tuna projekti kibao, nawaomba watu wavute subi--ra watajionea kila kinachoendelea kati yetu.Kuanzia sasa Kiba atakuwa akipeperusha ‘brand’ za Kidoti kwa kila atakachofanya ikiwa ni pamoja na mavazi,” alisema Jokate.

SIKU MOJA KABLA YA NDOA BI HARUSI AGOMA KUOLEWA!

Chande Abdallah na Deogratius Mongela
KIMENUKA! Ikiwa ni siku moja tu kabla ya kufungwa kwa ndoa kati ya Zuhura Omari na Abdallah Salehe, katika hali isiyotarajiwa, mke mtarajiwa amekataa kushiriki tendo hilo la kheri licha ya taratibu zote kukamilika na kusababisha tafrani kubwa huko Buguruni Kwa Mnyamani jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita.
Ndugu wakiwa hawana la kufanya baada ya binti huyo kugoma kuolewa.
Tukio hilo lilitokea Mei 23, mwaka huu wakati ndugu wa mume walipokusanyika nyumbani kwa Abdallah tayari kwa shughuli, lakini wakalazimika kuondoka baada ya kuelezwa kuwa mwanamke amekataa kuolewa, ikidaiwa ni mara ya pili baada ya kufanya hivyo tena mwaka jana.
Shuhuda wa tukio hilo aliliambia Ijumaa kuwa baada ya kukataa mwaka jana, taratibu nyingine zote, ikiwa ni pamoja na mahari na zawadi ndogondogo zilipelekwa ukweni na ndoa hiyo ikapangwa kufungwa Mei 22, mwaka huu, lakini ghafla wakapata taarifa hizo za kushangaza.

Thursday, May 28, 2015

Diamond Platinumz aibukia programu ya Mziiki

Nyota wa muziki wa bongo flava nchini Diamond Platinumz amewataka wasanii wa Tanzania kusambaza nyimbo zao kwa njia ya teknolojia kama vile Mziiki iliyozinduliwa hivi karibuni ili ziweze kuwafikia watu wengi na kwa wakati huohuo wanamuziki pia kunufaika na jasho lao.

Diamond anasema kuwa  ameamua kazi zake kuziingiza sokoni tofauti na kazi zake za nyuma ambapo baada ya  kushauriana na wadau anaoshirikiana nao kikazi ameamua aingie sokoni kwa njia ya kidigitali kupitia programu ya Mziiki iliyozinduliwa hivi karibuni ambayo pia yeye ni balozi anayeitangaza.

WANANCHI WATAKIWA KUTOA TAARIFA ZA UKIUKAJI WA KANUNI NA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

Naibu kamishna wa jeshi la polisi kikosi cha Usalama Barabarani, SACP Johanes Kahatano (katikati) akiwafafanulia jambo Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia (kushoto), Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kamishna Msaidizi wa Polisi Mohamed Mpinga, na Mkurugenzi wa Radio One Stereo, Deogratius Rweyunga kuhusiana na  kampeni ya kuzuia ajali barabarani inayojulikana kama “Zuia Ajali Sasa, Toa Taarifa Mapema”  kupitia namba 0800757575. Kampeni inayoendeshwa na jeshi la polisi  kikosi cha Usalama barabarani, Vodacom Tanzania na vyombo vya habari vya kampuni ya IPP .
Mkuu wa jeshi la polisi kikosi cha Usalama Barabarani, Kamanda Mohamed Mpinga (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia (kushoto) kuhusiana na kampeni hiyo.
Deogratius Rweyunga (katikati) akibandika stika yenye namba 0800757575 ambayo imetolewa mahsusi kwa abiria wanaotumia vyombo vya moto kusafiria ili kutoa taarifa bure kuhusu ukiukaji wa sheria na kanuni za usalama barabarani kupitia namba hizo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya “Zuia Ajali Sasa, Toa Taarifa Mapema”.

MTOTO WA JOHARI AIBUA MASWALI

KUFUATIA kuibuka kwa habari ya msanii nguli, Blandina Chagula ‘Johari’ kubeba mimba na kujifungua kwa siri hadi mtoto kufikisha umri wa miezi 7 na kuripotiwa kwa mara ya kwanza na gazeti ‘tumbo moja’ la hili la Risasi Jumamosi, mambo mengi mapya ikiwemo maswali yameibuka na kuzua ‘sintofahamu’ juu ya uhalisia wa jambo hilo, Amani linakupa mchapo kamili.
Msanii nguli, Blandina Chagula ‘Johari’.
Saa chache baada ya habari hiyo kusomwa na mamilioni ya Watanzania wakiwemo wadau wa sanaa na burudani wiki iliyopita, minong’ono na mishangao ilianza kutambaa ambapo wengi walidadisi kwa kina ili kujua ‘lipi ni tui la nazi na yapi ni maziwa’ juu ya habari hiyo.
MASWALI YALIYOIBULIWA
Miongoni mwa maswali yaliyoibuliwa ni pamoja na mimba aliibeba akiwa wapi? Alitoka Dar kwenda Shinyanga anakodai kujifungulia mimba ikiwa na muda gani? Anaweza kuianika kadi ya kliniki? Nini sababu ya kuficha mimba hadi mtoto anafikisha miezi 7 na nini kimemsukuma kumwanika mtoto?
“Jamani, mbona hatuelewi haya mambo? Hivi inawezekana kweli kwa mtu maarufu kama Johari kubeba mimba na hadi kujifungua na mtoto kufikisha miezi yote hiyo (7) bila kujulikana?” alihoji Latifa Lusengi wa Sinza- Makaburini.
“Hiyo mimba aliibebea wapi? Mbona alikuwa akionekana hana tumbo?” alihoji mama Jane wa Mwananyamala.
MASTAA SASA
Kuashiria kuwa mjadala ulikuwa mzito, hoja na maswali hayakuishia kwa wadau tu kwani hata baadhi ya mastaa waliozungumza na mwandishi wetu ama ana kwa ana au kwa njia ya simu kwa nyakati tofauti, walionesha wasiwasi mkubwa juu ya habari ya utata huo huku wengine wakiomba hifadhi za nomino zao kwa kile walichokiita ni “kujitunzia heshima kwa Johari.”
Mtoto wa Johari.
MAINDA
Ruth Suka ‘Mainda’ ndiye alifungua pazia la majadala huu kwa upande wa mastaa, baada ya mwandishi wetu kumpigia simu na kumtaka atoe maoni yake juu ya kujifungua kwa ‘mbia’ wake huyo.“Mmh! Kama kweli Johari amejifungua, basi mimi nampongeza kwani kuzaa ni baraka, lakini sasa afikirie na suala la kufunga ndoa na huyo aliyezaa naye kwani hata umri unamruhusu, asikomee tu mtoto.”
“Nyie acheni utani bwana, sisi tunashinda naye kila siku iwe baa au sehemu tofauti, mbona hatukuona hata hizo dalili na ishara za mimba na sisi wanawake tunajuana sana kwa mambo kama hayo? Sijui lakini,” alihoji  msanii mwingine wa kike ambaye amekuwa akionekana mara kwa mara na Johari na kuomba hifadhi ya jina.
“Kama ni kweli kulikoni afiche mimba?” aliuliza kwa kifupi msanii wa kiume.
JOHARI AZIDI KUPIGILIA MSUMARI
Baada ya mwanahabari wetu kusikia maswali hayo kutoka kwa wadau na baadhi ya wasanii, alimtafuta Johari kupitia simu yake ya kiganjani ambapo alifunguka, kisha kukata simu.

RAY, CHUCHU HANS WAONESHANA MAHABA HADHARANI!


Richard Bukos
MAHABA popote! Licha ya kudaiwa ‘wamemwagana’, wapenzi wawili ambao ni wasanii ndani ya Bongo Movie, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Chuchu Hans wameoneshana mahaba mazito hadharani na kuwaziba midomo waliodhani hawawezi kuwa pamoja tena.
Wasanii ndani ya Bongo Movie, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Chuchu Hans wakionyeshana mahaba.
Ishu hiyo ilinaswa hivi karibuni na ‘kasuku’ wetu maeneo ya Posta jijini Dar, kulikokuwa na sherehe za utoaji wa tuzo za filamu (TAFA) na kuwafanya watu wengi kushangaa huku wakionekana kuteta kwa nyakati tofauti.
“Mmh, hawa wamerudiana kwa mahaba mazito namna hiyo tena? Mbona tulisikia wameachana sasa naona wamegandana tena,” alisikika msanii mwingine (jina tunalo).
Hata hivyo, mwandishi wetu alimfuata Ray na kumuuliza kuhusu minong’ono ya wao ‘kutemana’ ambapo alijibu;
 “Huyu ndiye mke wangu, hayo mengine achana nayo kabisa.”

YAMOTO BAND, MASHAUZI KUWASHA MOTO MANGO GARDEN LEO


KWA mara ya kwanza baada ya miaka mingi, ukumbi wa Mango Garden, ulioko Kinondoni, jijini Dar es Salaam, kupitisha wikiendi bila burudani yoyote, leo usiku ‘utawaka moto’ wakati Yamoto Band na Mashauzi Classic zitakapotoa shoo kabambe hapo.
Wasanii wa yamoto band.
Ni onyesho ambalo limeteka hisia za mashabiki wa muziki kutokana na ukweli kuwa vikundi hivyo viwili havijawahi kukutana katika katika onyesho la pamoja, ukiondoa yale matamasha yanayoshirikisha wasanii wengi.
Kesho, Ijumaa,  Malaika Band ambao hupiga hapohapo Mango Garden, kila Ijumaa, watakuwa Arusha mjini wakitoa burudani.
Mwimbaji na Kiongozi wa Kundi la Mashauzi Classic, Aisha Ramadhani 'Isha Mashauzi'.
Vilevile,  Twanga Pepeta ambao hupiga Mango Garden kila Jumamosi, wasanii hao Jumamosi hii watakuwa Wenge Garden Ukonga.  Bendi ya FM Academia ambayo huibuka Mango Garden na kufukia viraka vya bendi zilizopata dharura ya kuhama ukumbi, Ijumaa hii itakuwa Polisi
Kilwa Road wakati Jumamosi itakuwa Leaders Club katika tamasha la Nyama Choma.

Wednesday, May 27, 2015

MIKE ADAIWA KUMNASA DAVINA

 
Michael Sangu ‘Mike’.
Richard Bukos
SIKU chache baada ya mwigizaji Michael Sangu ‘Mike’ kumwagana na mkewe mwigizaji Ndumbagwe Misayo ‘Thea’, amedaiwa kumnasa staa mwingine wa filamu, Halima Yahaya ‘Davina’ kwa kuwa naye karibu kiasi cha kuibua maswali.
Aliyekuwa mke wa Mike, Ndumbagwe Misayo ‘Thea’.
Katika hafla ya utoaji wa tuzo za TAFA wiki iliyopita katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Mike na Davina licha ya kuwa kama kumbikumbi kila walipokwenda alimtambulisha Davina kwa wasanii wenzake kuwa ni mtu wake.
 
Staa wa filamu, Halima Yahaya ‘Davina’.
Alipoulizwa Davina kama ameridhia kauli ya kuwa ‘misezi’ wa Mike, alikataa katakata na kumpa ‘makavu’ laivu staa huyo:
“Kamwe siwezi kutembea na Mike na haiwezi kutokea hadi nakufa.
Kama anasema hivyo kwa lengo la kutafuta kiki aseme! Asitake kunigombanisha na rafiki yangu Thea (mke wa Mike waliyemwagana) tunaheshimiana sana, tena akiendelea kuropoka ujinga huo atanijua mimi ni nani. Anikome.”

DIAMOND ATELEKEZA WATOTO SHULE!

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS KABANG! Staa anayevuna fedha nyingi kupitia kipaji chake cha muziki, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amewatelekeza watoto katika Shule ya East Africa International jijini Dar ambao aliahidi kuwalipia ada, Risasi Mchanganyiko linakuwa la kwanza kukudondoshea.
 
Wanafunzi wanaodaiwa kutelekezwa na Staa anayevuna fedha nyingi kupitia kipaji chake cha muziki, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Chanzo makini kililiambia gazeti hili juzi kwamba, baada ya Diamond kuwashindanisha watoto hao, Hillary na Hamis (katika picha no. 1 na 2 zilizoko ukurasa wa mbele walipelekwa shule na Diamond) katika shindano la Ngololo lililonyika Januari, mwaka jana katika Viwanja vya Leaders Club, Dar na kushinda aliamua kuwapeleka katika shule hiyo na kuahidi kuwalipia ada kila mwaka lakini kuanzia hapo aliwatelekeza.
“Jamani Diamond kila kukicha anafanya shoo za mamilioni lakini ameshindwa kuwalipia ada wale watoto ambao aliahidi kuwasomesha. Wamesoma mwaka mmoja tu,  mwezi uliopita walitimuliwa na sasa wako nyumbani. Inauma sana kwani hawa watoto walitolewa kwenye shule za kawaida na yeye ndiyo akawapeleka kule,” kilisema chanzo hicho.
WAZAZI WANASEMAJE?
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wazazi wa wanafunzi hao, Fadhili alisema watoto wao walitimuliwa shuleni tangu April mwaka huu kwa kuwa, Diamond hakuwahi kuwalipia ada tangu alipowaingiza pale.“Inauma sana, kwani tangu watoto wetu watimuliwe tumekuwa tukifuatilia kwa mtu tuliyeambiwa ni msimamizi wa Diamond (jina lake linahifadhiwa kwa sasa) lakini hatupi jibu la kueleweka.

 
Nasibu Abdul ‘Diamond akiwa na wanafunzi hao pamoja na mwalimu wao.

RAY ABANWA MTOTO WA JOHARI, AFUNGUKA!

Brighton Masalu na Musa Mateja
SIKU chache baada ya kuripotiwa na gazeti pacha la hili, Risasi Jumamosi kuwa staa wa sinema za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ alibeba mimba na kuzaa kwa siri huku tetesi zikivuma kuwa baba wa mtoto huyo ni msanii mwenzake, Vincent Kigosi ‘Ray’, mambo yameanza kunoga baada ya Ray kufunguka kuwa hahusiki kwa lolote, Risasi Mchanganyiko ‘limemzingira’.
Staa wa filamu Bongo,Vincent Kigosi ‘Ray’.
Hivi karibuni gazeti hili lilimbana staa huyo anayetamba sokoni kwa sasa na Filamu ya Chicken Head baada ya kubambwa nje ya Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Posta jijini Dar, kulikokuwa na sherehe za Tuzo za TAFA ambapo aliweka wazi.
Awali, Ray alisema si busara wala hataki...
kuzungumza mengi juu ya madai hayo kwani hahusiki kwa lolote na kwamba watu wasimtafsiri kutokana na maneno yasiyokuwa na ukweli huku akimtaja mpenzi wake wa sasa, Chuchu Hans kuwa ndiye mwanamke wake wa maisha.
Ray alifunguka kuwa, kati ya mambo yanayomchukiza ni ama kuzushiwa au kuhusishwa na mambo ambayo yanamfanya aonekane wa hovyo katika jamii na kusisitiza kusiwepo na mjadala unaopingana na kauli zake.
Staa wa sinema za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ akiwa na mwanaye.
Huku akiwa amemganda Chuchu kimahaba mbele ya kadamnasi, Ray alikwenda mbele zaidi na kusema ni jambo la heri kujiweka mbali na watu wanaotafuta umaarufu kupitia migongo ya watu, kauli iliyozua viulizo kwa waandishi wetu na yeye kushindwa kuifafanua kwa kile alichokiita ‘hakuwa na mudi ya mazungumzo zaidi’.

Tuesday, May 26, 2015

Wimbo mpya ya Mirror ‘Hapo Ulipo’ iko hapa


mirror
Hii kazi mpya ya msanii kutoka endless fame Mirror ‘Hapo Ulipo’ ,Download na isikilize hapa.

LOWASAA AKUTANA NA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI JANA DODOMA

  Waziri Mkuu mstaafu, Edward lowassa akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari mjini Dodoma jana kuhusu mambo mbalimbali pamoja na safari ya matumaini.
 Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa akizungumza na wahariri mjini Dodoma hao.

MAONYESHO YA PICHA ZA ALBERT MANIFESTER YAFANA JIJINI DAR


Mwimbaji wa nyimbo za injili wa Columbus, Ohio Enock Mwamba(kati) akiimba moja ya nyimbo za injili huku akiwashirikisha Mike Kalambay aliyekuja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Upendo Nkone aliyekuja toka Tanzania maalum kunogesha tamasha la Gospel lililofanyika siku Jumapili May 24, 2015 na kuhitimisha tamasha hilo lililokua la siku 3 mjini humo lililoanzia siku ya Ijumaa May 22, 2015.
Mike Kalambay akiimba huku akitoa neno la Mungu kwa Kifaransa kilichochanganyika na lingala huku mchungaji Fayes (kulia) akitafsiri kwa kiingereza na Kiswahili.
Mike Kalambay akiimba moja ya nyimbo za injili kwenye tamasha la gospel lililofanyika siku ya Jumapili May 24, 2015 mjini Columbus, Ohio.
Mike Kalambay toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo akishambulia jukwaa na nyimbo za injili.
Mwimbaji mahili wa nyimbo za Injili Upendo Nkone akiimba moja ya nyimbo zake kwenye tamasha hilo.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate