EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, March 30, 2015

SHOW YA LADY JAY DEE NA ALI KIBA ILIVYOBAMBA KIOTA CHA M.O.G


DSC_0035Mwanamuziki Lady Jay Dee akitoa burudani na Machozi Band Ijumaa ya tarehe 27 mwezi huu ndani ya kiota chake cha Mog Bar & Restaurant (Nyumbani Lounge) katika show anazofanya mara moja kwa mwezi kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ambapo Ijumaa hiyo alimualika Msanii machachari wa Bongo Flava Ali Kiba kwa ajili ya kukonga nyoyo za mashabiki wake ndani ya kiota hicho.
DSC_0089
Pichani juu na chini ni mashabiki wa Machozi Band wakimtunza manoti Lady Jay Dee.
DSC_0083
DSC_0078
DSC_0046
Umati wa mashabiki wa Machozi Band wakipata burudani kutoka kwa band hiyo inayoongozwa na Lady Jay Dee.
DSC_0048
DSC_0065
DSC_0066
DSC_0204
Msanii nyota nchini, Ali Kiba akitoa burudani ya aina yake ndani ya kiota cha M.O.G Bar & Restaurant baada ya kutikia mualiko wa msanii mwezake Lady Jay Dee na kufanya Live Music bila kutumia CD na kuwafanya mashabiki kupagawa zaidi.
DSC_0217
Ali Kiba akiendelea kuwaburudisha mashabiki wake Machozi Band.
DSC_0219
Warembo walipagawajem sasa.
DSC_0248
Twende kazi hapo sasa.
DSC_0253
Mrembo akijinafasi kwa Ali Kiba.
DSC_0275
#ChekechaCheketua.......Wadada wakichizika na mauno ya Ali Kiba na style yake mpya.
DSC_0283
Mwanadada hakukubali kabisa na kuamua kupanda jukwaani kulipiza mauno ya Ali Kiba.
DSC_0284
Picha inajieleza jinsi Ali Kiba alivyokonga nyoyo za mashabiki wake.
DSC_0296
Lady Jay Dee: Nimemkuta analia, kajilaza, sababu amechoka.....Mengi amevumilia, yalomkwaza, anataka kuondoka....ana siku ya pili sasa, hajarudi nyumbani kulala,...namuonea huruma sana, haya....mapenzi hayana maana
Lady Jay Dee: who the single girl.....who the single boy, Ali Kiba: i am a single boy.......Ali Kiba: who the single girl, .......Lady Jay Dee: i am a single girl.......Lady Jay Dee: who the single boy, Lady Jay Dee na Ali Kiba:....mi na we single boy.
DSC_0300
Tumefunika mbaya mtu wangu....ndio ishara waliyokuwa wakipeana Ali Kiba na Lady Jay Dee.
DSC_0281
DSC_0256
DSC_0010
Binti mrembo binti kwenye kipaji Faraja wa Machozi Band akiwapa raha mashabiki wa Band hiyo Ijumaa ya mwisho wa mwezi huu ndani kiota cha Mog Bar & Restaurant (Nyumbani Lounge).
DSC_0142
Mkali wa Reggae na Dance Hall nchini Double D akiwarusha mashabiki wake ndani ya kiota cha M.O.G Bar & Restaurant.
DSC_0158
Mkali wa Reggae na Dance Hall nchini Double D katika hisia kali za kuwapa raha mashabiki wake.
DSC_0144
Vijana wakijiachia vilivyo baada ya Reggae za Double D kuwakolea ndani ya kiota cha M.O.G Bar & Restaurant.
DSC_0170
Omirady wa Machozi Band akitoa burudani kwa mashabiki wa Band hiyo katika show inayopigwa mara moja kwa mwezi na kuwateka mashabiki wengi ndani ya kiota cha M.O.G Bar & Restaurant.
DSC_0015
Msanii Chiqitita wa Machozi Band akitoa burudani kwa mashabiki wa band hiyo (hawapo pichani).
DSC_0059
Mashabiki wa machozi band wakipata Ukodak.
DSC_0193
Sehemu ya umati wa mashabiki wa Live Band uliofurika Ijumaa ya mwisho wa mwezi huu ndani ya M.O.G Bar & Restaurant kushuhudia show ya wakali wa muziki nchini Lady Jay Dee na Ali Kiba.
DSC_0001
Hawa jamaa ndio wanaohakikisha Lady Jay Dee anakuwa salama siku zote.

Saturday, March 28, 2015

Diamond Platnumz ft Khadija Kopa - Nasema Nawe ( Official Music Video )

Brand new single by Diamond Platnumz Ft Khadija Kopa
titled "Nasema Nawe"
Video Directed by Hanscana

UCHAWI WAFUMULIWA SOKONI

CHANZO: RISASI JUMAMOSI/GPL
WE acha tu! Sangoma mmoja aliyejulikana kwa jina la Mohamed Chimwaganje (44), amezua kizaazaa katika Soko la Kapera lililopo Mwembechai jijini Dar kufuatia kufumua vitu chini ya ardhi vinavyodhaniwa ni vya ushirikina,  Risasi Jumamosi linakujuza.
Sangoma Mohamed Chimwaganje akishika hirizi aliyoitoa katika Soko la Kapera lililopo Mwembechai jijini Dar.
Tukio hilo la aina yake lilijiri asubuhi ya Machi 25, mwaka huu katika soko hilo ambapo awali taarifa zilimfikia sangoma huyo kwamba, baadhi ya  wafanyabiashara wa soko hilo wamekuwa wakiibiwa pesa zao kwa njia ya maajabu  .
MFANYABIASHARA AZUNGUMZA
Akizungumza na Risasi Jumamosi, mmoja wa mashuhuda sokoni hapo alisema kuwa, ilifika wakati wafanyabiashara hao walikuwa hawaingizi faida wakiwa sokoni hapo na wanaweza wakauza lakini kwenye mahesabu jioni, pesa kibao zimepotea, hivyo kusababisha wengi kuacha biashara baada ya kufilisika.
“Lakini cha kushangaza ni kwamba, baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo wamekuwa wakiuza sana vitu visivyokuwa na ubora na vile vyenye ubora kuachwa na wateja ambapo mwishowe huharibika na kutupwa.“Basi, kutokana na hali hiyo tukaamua kumwomba huyo mtaalamu ‘sangoma’ aje afanye mambo yake maana tunamwamini kwa sababu  ameshamponya uchizi mtu mmoja wa hapa mtaani,” alisema mfanyabiashara huyo akikataa kutaja jina lake gazetini.

BODABODA WANUSA KIFO KWA KUKWAPUA MKOBA

Mmoja kati ya vibaka hao akiwa hoi baada ya kupata kichapo kikali.
Mayasa mariwata na denis mtima
Vijana wawili wa bodaboda ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja, hivi karibuni walikoswakoswa kuuawa baada ya kupora mkoba uliokuwa na simu ya mwanamke aliyekuwa akipita njia.
Tukio hilo lilijiri Jumanne iliyopita, saa 1.30 usiku maeneo ya Sinza Afrikasana, pembeni mwa Baa ya Hongera ambapo inadaiwa ni eneo hatari kwa wizi huo.Shuhuda wa tukio hilo alilitonya gazeti hili kuwa, imekuwa ni tabia kwa baadhi ya vijana kutumia usafiri wa bodaboda kupora watu simu na mikoba hasa wanawake na kwamba siku hiyo arobaini ya vijana hao ilikuwa imefika.

LADY JAYDEE AJICHAGULIA JENEZA

Uchuro? Baada ya kutundika mtandaoni kwa mara nyingine picha za jeneza alilojiandalia litakalotumika siku akiaga dunia, mwanamuziki Judith Daines Wambura Mbibo a.k.a Lady Jaydee au Jide, amelaaniwa vikali na mashabiki wake kwa kitendo hicho.
Mwanamuziki Judith Daines Wambura Mbibo a.k.a Lady Jaydee au Jide.
ABADILI RANGI
Mwaka 2012, Jide alitupia mtandaoni picha za jeneza lake lenye mchanganyiko wa rangi ya zambarau na nyeupe lakini safari hii amebadilisha na kutupia mengine mawili yenye rangi ya krimu na nyeupe.
MANENO KUNTU
Kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo anatumia jina la jidejaydee, juzi, mwanadada huyo, pamoja na picha hizo mbili, alisindikiza na maneno kuntu kwa chini yaliyosomeka, ‘Nimebadilisha mawazo yangu, sitaki tena lile la zambarau. Moja kati ya hayo hapo juu. Msinimaindi. Kila mtu atakufa. Nilikuwa nafikiria pia iwe kwa waalikwa tu. Sitaki kufunuliwa’.
MASHABIKI WAMLAANI
Risasi Jumamosi liliinyaka ishu hiyo sekunde chache baada ya Jide kuitupia ambapo ndani ya muda mfupi ‘posti’ hiyo ilikuwa na maoni mengi ya kulaani kitendo hicho.
Baadhi ya mashabiki walieleza waziwazi kuchukizwa na jambo hilo alilolifanya staa wao wanayempenda.
SEHEMU YA MAONI
“Kifo kipo kwa kila binadamu lakini hatutakiwi kukifikiria hivyo dada (Jide) unamkosea muumba wako.
“Wewe ni kioo changu, ila kwa hili kwa kweli sijalipenda.
“Jamani dada mbona unatutisha au haupo sawa leo?
“Wewe wajina umefikiria nini lakini?
“Kama umeshaona unakufa sema tujue.
Muonekano wa jeneza hilo.
“Duh! Dada fanya maombi hiyo ni roho ya umauti.
“Dada nini tena mbona unamkufuru Mungu?                      Hata kama una machungu kiasi gani, huwezi kufanya hivyo kwani ni mipango ya Mungu. Muombe akusamehe.
“Wewe Jide wewe huogopi lakini?

HUKUMU DNA MTOTO WA NAY APRILI 8

Mwandishi wetu
LILE sakata la mtoto si wa Mbongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kwa mujibu wa madai yaliyotolewa na mzazi mwenzake, Siwema limeingia hatua nyingine baada ya ofisi ya mkemia mkuu wa serikali kusema majibu kamili ya kipimo cha vinasaba ‘DNA’ yatatolewa Aprili 8, mwaka huu.
Mbongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa na mzazi mwenzake Siwema pamoja na mtoto wao.
Akizungumza na Risasi Jumamosi juzi jijini Dar, Nay alisema kila kitu kimekwenda sawa, hivyo anachosubiri ni hayo majibu ili ajue moja kwamba mtoto huyo mwenye miezi mitatu  ni wa nani kati yake yeye na mwanaume aliyetajwa na Siwema mwenyewe.
“Ndiyo natoka sasa kwenye ofisi ya mkemia. Hukumu ya DNA ile ni baada ya wiki mbili kuanzia leo (juzi Alhamisi). Lakini we acha tu. Mh! Nimeshafanya kila kitu, ni wao tu,” alisema Nay.
Aliongeza: “Ila mimi nashangaa. Yule mkemia aliyenipima, kaniambia, ‘Nay hukuwa na haja ya kupima DNA, mbona kwa uzoefu wetu hapa ukimwangalia mtoto anaonekana ni wako, ila kwa sababu umeamua kupima mwenyewe sawa.

MZIMU WA KANUMBA WADAIWA KUUA WAWILI

mwandishi wetu
HII ni habari ya kutisha! Takriban miaka mitatu imekatika tangu kifo cha aliyekuwa staa wa Bongo Movies, Steven Kanumba huku watu wawili wakifariki dunia kwa nyakati tofauti lakini nyuma ya pazia ya vifo vyao, mzimu wa Kanumba unatajwa kuhusika kutokana na watu hao kutaka kuishi mahali pa marehemu huyo, endelea kusoma Risasi Jumamosi.
Aliyekuwa staa wa Bongo Movies, marehemu Steven Kanumba.
SOMA TUKIO HILI LA KUSHANGAZA
Itakumbukwa kwamba, baada ya kifo cha Kanumba, mama yake mzazi, Flora Mtegoa ndiye aliyeshika jukumu la kusimamia mali za marehemu mtoto wake (alikuwa na haki).
Miongoni mwa mali hizo ukiachilia mbali, magari, vifaa vya kurekodia filamu, viwanja na filamu zilizokuwa hazijalipwa, mama Kanumba aliimiliki ofisi ya Kanumba iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Kanumba The Great Film iliyokuwa Sinza.Hata hivyo, hivi mapema Februari, mwaka huu, mama Kanumba alitoa vitu kwenye ofisi hiyo kwa madai ya kushindwa kulipa pango, hivyo ofisi ikawa wazi.

Friday, March 27, 2015

Tuzo za watu zaja kivingine, vipengele vyaongezeka


Mhariri mkuu wa Bongo5  Bw. Fredrick Bundara akiwa pamoja na mhariri msaidizi, Sandu George wakizungumza leo na waandishi wa habari katika uzinduzi wa Tuzo za watu 2015t
Kampuni ya Bongo5 Media Group, imezindua msimu mpya na wa pili wa Tuzo za Watu Tanzania zilizoanzishwa mwaka jana ili kuwatuza watu kwenye sekta ya burudani na habari wanaofanya vizuri.
Akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari leo, mhariri mkuu wa mtandao wa Bongo5, Fredrick Bundala amesema tuzo za mwaka huu zimeboreshwa zaidi kwa kuongeza vipengele vitatu vipya.
“Mwaka huu tuzo zimeongezewa nguvu zaidi. Kutoka vipengele 11 tulivyokuwa navyo mwaka jana hadi vipengele 1. Mwaka huu tumeongeza vipengele vitatu muhimu,” amesema Bundala.
Amevitaja vipengele vilivyoongezeka kuwa ni pamoja na muongozaji wa filamu anayependwa, tovuti/blogu inayopendwa na mfadhili maarufu anayependwa.

GWAJIMA AMETUMWA KUMTUSI PENGO

SIKU chache baada ya Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo la jijini Dar, Josephat Gwajima kumtusi Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki nchini, Polycarp Kardinali Pengo, taarifa nyuma ya pazia zimeeleza kuwa mchungaji huyo ametumwa na kikundi cha watu fulani, Uwazi Mizengwe linakupa mchapo kamili.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo la jijini Dar, Josephat Gwajima.
Gwajima alirekodiwa kwenye ibada ya kanisa lake Jumapili iliyopita ambapo ‘alimtusi’ Pengo akituhumu kuwa ni msaliti kwani amekwenda kinyume na Taasisi ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Baraza la Makanisa ya Kipentekoste (CPCT) na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwa kuwataka waumini waisome Katiba Inayopendekezwa kisha wapewe uhuru wa kupiga kura ya “ndiyo” au “hapana” tofauti na vyombo hivyo vyenye dhamana ya kuongoza dini ya Kikristo vilivyotaka waumini waipigie kura ya “hapana” Katiba Inayopendekezwa.

UNYAMA ULIOJE?


Joseph Ngilisho
Unyama ulioje! Wanawake wanne wanaojiita Kundi la ‘Boko Aramu, hivi karibuni wamemteka msichana mmoja mrembo aitwaye Marry kisha kumfanyia kitu mbaya ikiwa ni pamoja na kumdhuru sehemu zake za siri.
Marry akiwa katika Hospitali ya Mount Meru, baada ya kunusurika kuchinjwa.
Sikia simulizi ya Marry
Akizungumza kwa tabu akiwa katika Hospitali ya Mount Meru, Marry ambaye anamiliki saluni ya kike alisema, chanzo cha kufanyiwa hivyo ni wivu wa mapenzi huku akimtaja rafiki yake wa karibu aitwaye Maurin kuhusika.

WANAKWAYA: JOKATE ANATUTIA AIBU

Hamida hassan
Ile skendo ya kupiga picha za nusu utupu na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii huku midume ikijirushia na kujifaidia kwa macho, ukijumlisha aibu mpya ya kukata mauno mbele ya wanaume, staa mwenye jina kubwa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ amewakera wanakwaya wenzake ambao wamedai kuwa anawatia aibu, Ijumaa lina mchapo kamili.Staa mwenye jina kubwa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
TUJIUNGE KANISA LA SAINT PETER, OYSTERBAY, DAR
Ishu ya Jokate kutupia picha za nusu utupu mitandaoni si mpya, mara kadhaa amekuwa akiripotiwa kwa tabia yake hiyo kiasi cha kuwakera wanakwaya hao wa kanisa analosali la Saint Peter lililopo Oysterbay jijini Dar.
Mbali na picha hizo, safari hii anaandamwa na skendo mpya ya kudaiwa kukata mauno mbele ya midume anapokuwa kwenye shoo zake baada ya kutumbukia kwenye muziki wa Bongo Fleva.
AJADILIWA KANISANI
Kwa mujibu wa baadhi ya wanakwaya hao, wamekuwa wakimjadili mara kwa mara hasa wanapokuwa mazoezini kanisani hapo mara baada ya mmoja wao kurushiwa picha za mwanadada huyo kwenye mitandao ya kijamii.
NI AIBU KWA KANISA?
Baadhi ya wanakwaya hao walikwenda mbele zaidi na kudai kwamba mbali na kuwa ni kioo cha jamii lakini bado ni alama ya kanisa hivyo ni aibu kwa kanisa pia kwa sababu binti aliyelelewa kidini kama Jokate hawezi kuwa na tabia za aina hiyo.
Jokate akiwa kwenye pozi.
AU BIASHARA MATANGAZO?
Kuna baadhi walidai labda mwanadada huyo anafanya hivyo ikiwa ni njia ya kujitangaza yeye na biashara yake bila kujali kama anaweza akajiondolea ute wake na heshima aliyoijenga kwa miaka mingi.

Thursday, March 26, 2015

Orodha ya wachezaji na makocha wanaoingiza pesa nyingi zaidi kwa mwaka

makocha 2
makocha wachezaji

NI JUMAPILI HII: USIKU WA BABA NA MWANA SEASON 2

JELA ILIVYOVUNJA UHUSIANO WA MASTAA BONGO


Jack Patrick, akiwa na mumewe wa ndoa, Abdulatif Fundikira.
Na Waandishi wetu
KATIKA ulimwengu wa wapendanao kuna changamoto nyingi ambazo wapenzi hukutana nazo huku wengine wakizishinda na baadhi kushindwa.
Wapo wapenzi walioshindwa kuendelea na uhusiano wao mara baada ya mmoja kuugua, kupata ulemavu na sababu nyingine nyingi, lakini wapo walioendelea kuvumiliana pamoja na sababu zote hizo na hatimaye penzi lao likazidi kuimarika na kuwa mfano katika jamii.
Hali hiyo haipo kwa watu wa kawaida peke yao bali hata kwa mastaa wetu wamejikuta wakiangukia katika mtihani huo na kushindwa kuhimili kusimamia mapenzi yao. Kifungo au jela ni moja ya sababu zinazosababisha ndoa au uhusiano wa mastaa wengi na wenza wao kuharibika.
Katika makala haya tunakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao wamekumbwa na sakata hilo:-
Jack Patrick,

HUKU AKISAKWA KUMPASUA KICHWA MTU TID AMPIGA MENEJA WAKE

PEPO la ugomvi linazidi kumuandama staa wa Bongo Fleva, Khaleed Mohamed ‘TID’, baada ya kusakwa na jeshi la polisi kwa kosa la kumjeruhi mtu mwishoni mwa wiki iliyopita, msanii huyo ametengeneza kicha cha habari kwa mara nyingine akidaiwa kumpiga meneja wake aliyefahamika kwa jina la Tall Mnyama.
Staa wa Bongo Fleva, Khaleed Mohamed ‘TID’.
Katika tukio la awali, TID alidaiwa kutembeza kichapo na kumjeruhi James Richard, mkazi wa Jiji la Dar kwa kosa alilodai kuwa ni kupaki gari kwenye eneo lake, maeneo ya nyumbani kwa msanii huyo, Kinondoni-Sterio jijini Dar.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate