EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, October 3, 2015

Hatari kubwa! Mafuta ya Transfoma kukaangia Chips, Wabongo wengi kufariki!

Mayasa mariwata na Shani ramadhani
HATARI! Kufuatia kuwepo kwa madai kwamba, baadhi ya wakaanga chipsi mijini, hususan jijini Dar, wamekuwa wakitumia mafuta ya transifoma kukaangia chakula hicho, timu ya Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ ya Global Publishers iliingia mtaani kwa lengo la kujiridhisha.
OFM iliingia kwenye viunga mbalimbali vya jiji hasa sehemu ambazo zina vibanda vya wauza chipsi na kuzungumza nao.
Muuza chipsi maeneo ya Mwananyamala aliyejitambulisha kwa jina moja la Ushie, alipoulizwa kuhusu kuwepo kwa madai hayo, alisema amesikia wapo wanaotumia lakini yeye hatumii.
Mwingine alikutwa na OFM maeneo ya Kinondoni akajitambulisha kwa jina la Idi Juma. Yeye alisema: “Kuna mtu aliwahi kuniletea mafuta ya transifoma akidhani nitanunua ili niwe natumia kukaangia chipsi nikagoma. Lakini wapo wauza chipsi wengi ambao si waaminifu wanatumia.”
Karibu wauza chipsi wote walioulizwa na OFM hawakukiri kuhusu kutumia mafuta hayo. Lakini walisema wenzao wanatumia.Inadaiwa kuwa, wauzaji wanapenda mafuta ya transifoma kwa sababu yanaweza kutumika kwa muda mrefu, hata mwezi mmoja bila kukauka kwenye karai na hayafanyi chipsi kuwa nyeusi kama mafuta halali. Inadaiwa pia, chipsi zilizokaangwa na mafuta hayo ni tamu sana.
TANESCO YATOA TAMKO
Jumatano iliyopita, OFM ilizungumza na Afisa Habari wa Shirika la Ugavi Tanzania (Tanesco), Adrian Severin na kumuuliza kama shirika linajua kutumika kwa mafuta hayo kukaangia chipsi ambapo alisema:
“Tunajua japokuwa hatujawahi kuthibitisha kwa kumwona mtu akiyatumia. Wengine wanayatumia kwenye vipodozi, wengine wanachanganya na oil ya magari. Lakini Tanesco tunatoa wito kwa Watanzania, hususan wanaoishi jirani na transifoma kutoa taarifa mara wanapomwona mtu anapanda kwenye transifoma huku si mfanyakazi wa Tanesco.
“Wizi wa mafuta haya unasababisha transfoma kushindwa kufanya kazi na hivyo maeneo husika kukosa umeme.”
DAKTARI AFAFANUA
OFM lilimtafuta daktari mmoja wa jijini Dar es Salaam, dokta Chale kwa lengo la kumuuliza kama mafuta ya transifoma yakitumika kwenye chakula yana madhara, akajibu:
“Makubwa tu. Kwanza, mtumiaji anaweza kupata ugonjwa wa kansa ya tumbo. Pili, hayo mafuta yanaweza kusababisha maini na figo kushindwa kufanya kazi. Na tabia hii ikiendelea, Wabongo wengi watakufa.”

CHANZO: Global Publishers

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate