EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 29, 2015

Mkopo noma! Mfanyabiashara atupiwa vitu nje, Nyumba yauzwa!

DSC_0594
Mfanyabiashara maarufu, Mohamed Majid Seif akitaharuki.
Boniphace ngumije
Mkopo noma! Mfanyabiashara maarufu, Mohamed Majid Seif, mkazi wa Mikocheni A, Kinondoni jijini Dar, ametolewa vitu ndani ya nyumba yake namba A35/210 baada ya kushindwa kulipa mkopo wa Sh. Milioni 210 aliouchukua kwenye Benki ya Boa (Bank Of Africa) mwaka 2011.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, katika tukio hilo lililojiri nyumbani hapo, Seif alikopa kiasi hicho cha fedha akiwa na wenzake, lakini baada ya kushindwa kulipa kwa muda wa miaka miwili kama makubaliano yalivyoonesha, wenzake waliingia mitini na kumuachia msala.
DSC_0486
Vyombo vikipakizwa kwenye gari.
Ilidaiwa kwamba, baada ya Seif kuachiwa msala huo, aliiomba Boa kumuongezea muda ili aweze ‘kuklia’ deni hilo lakini benki haikuwa tayari kutokana na makubaliano waliyoweka Aprili 18, 2011 kuwa zikizidi siku sitini (60) kwenye muda wa makubaliano ya mkopo, bila kulipwa kwa fedha hizo pamoja na riba nyumba iuzwe.
“Baada ya makubaliano kushindikana, benki hiyo ilitangaza kuipiga mnada nyumba hiyo kupitia magazeti ya kila siku ambapo siku ya mnada, ilinunuliwa na Mwanaiba Mohamed Mzee, mkazi wa hapohapo Mikocheni kwa Sh. Milioni 56,” kilisema chanzo hicho.
DSC_0499‘Ubuyu’ uliendelea kudondoshwa kuwa, Seif hakuridhishwa na uamuzi huo uliochukuliwa na benki hiyo, jambo lililomfanya kukimbilia kwenye Mahakama ya Ardhi na Makazi, Kinondoni kuomba kutenguliwa kwa mnada huo.

Ilisemekana kwamba, Seif aliiomba mahakama hiyo kupewa muda zaidi ili alipe deni, lakini baada ya shauri lake kusikilizwa inadaiwa mahakama ilitoa ridhaa ya taratibu za kibenki kuendelea huku baadaye ikiipa kazi kampuni ya mawakili ya Rimina Auction Mart kumuondoa kwa nguvu kwenye nyumba hiyo.
Ilielezwa kwamba, ilipofika Agosti 19, mwaka huu ndipo Kampuni ya Rimina walipofika nyumbani hapo na kutupa vitu vyote nje bila kumuuliza mtu yeyote yule na kuikabidhi nyumba kwa mwenyewe (aliyeinunua) kupitia muwakilishi wake.
DSC_0579
Barua ya makabidhiano.
Wakati akitolewa vitu nje, mfanyabiashara huyo hakuwepo eneo la tukio, alipotonywa kilichokuwa kinaendelea nyumbani kwake, aliibuka na kutaka kuleta utata lakini tayari mwenye nyumba alikuwa ameshakabidhiwa mali yake huku jamaa huyo na mkewe wakitafuta hifadhi mpya.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate