EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 27, 2015

Urais: Ukawa kimeeleweka

27th July 2015
Chapa
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa.
Hatimaye mchakato wa kumpata mgombea urais kupitia vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) umefikia ukingoni na sasa jina la mgombea huyo linatarajiwa kuwekwa hadharani wakati wowote kuanzia sasa.
 
Taarifa kutoka chanzo kimoja miongoni mwa vigogo wa Ukawa ziliiambia NIPASHE jana kuwa, kazi kubwa ya uteuzi wa jina hilo iliyohusisha wakuu wa vyama vinavyounda Ukawa imeshakamilika na kwamba kilichokuwa kikisubiriwa kabla ya kutangazwa kwa jina la mgombea ni maridhiano ya ndani ya vyama; kazi ambayo pia ilikamilika mwishoni mwa wiki. Ukawa unaundwa na muungano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na NLD.
 
"Watanzania wanaopenda mabadiliko hawana sababu ya kuwa na hofu. Wakati wowote kuanzia leo (jana) jina la mgombea wetu tutaliweka hadharani na baada ya hapo tutaendelea na maandalizi yetu kabambe kuhakikisha kuwa tunahitimisha utawala wa CCM," chanzo hicho kiliiambia NIPASHE jana kwa sharti la kutotajwa. Uhakika wa kuelekea ukingoni mwa maridhiano kuhusu jina la mgombea wa Ukawa umetokana pia na kile kinachodaiwa kutokea kwenye kikao cha Baraza Kuu la CUF kilichofanyika juzi visiwani Zanzibar na pia kikao cha Kamati Kuu Maalum ya Chadema kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.
 
Inaelezwa kuwa wakuu wa CUF wamekwishajadili kwa kina suala la Ukawa na kimsingi wameridhia maamuzi kadhaa yatakayoupa nguvu umoja huo, huku Chadema kupitia kikao chake cha jana ikiridhia pia jina la mgombea kupitia majadiliano yao yaliyohusisha ajenda mbili kuu, ambazo ni maandalizi ya uchaguzi na taarifa za mchakato wa uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge na udiwani unaoendelea nchini kote. Aidha, imeelezwa kuwa kilichobaki hivi sasa ni masuala madogo ambayo yanaendelea kufanyiwa kazi kupitia vikao mbalimbali vinavyoendelea miongoni mwa vyama vinavyounda Ukawa kabla ya kumtangaza mgombea huyo.
 
Hata hivyo, hakuna kiongozi yeyote kutoka miongoni mwa vyama vinavyounda Ukawa aliyepatikana kuzungumzia rasmi suala hilo. 
 
MKUTANO UKAWA NA WAHARIRI
Jana, Ukawa waliitisha mkutano maalum na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine, ilitarajiwa kuwa wangeeleza juu ya mchakato wao wa kumtangaza mgombea wa nafasi ya urais. Hata hivyo, mkutano huo uliahirishwa na haikuelezwa ni lini utafanyika tena.
 
KUKOMBA VIGOGO CCM 
Katika hatua nyingine, imedaiwa kuwa Ukawa bado wako katika majadiliano na baadhi ya makada maarufu wa CCM wanaotarajiwa kuhamia upinzani kwa makundi na hivyo kuupa nguvu zaidi umoja wao.   
 
"Suala hili la kumtangaza mgombea limefikia mahala pazuri. Ila kuna majadiliano zaidi yanaendelea kuhusiana na uwezekano wa kuvuta vigogo zaidi kutoka ndani ya CCM," chanzo kingine kiliiambia NIPASHE.
 
Wiki iliyopita, wabunge waliokuwa makada muhimu wa CCM, Esther Bulaya (Viti Maalum) na James Lembeli wa Jimbo la Kahama walihamia Chadema na kutambulishwa ramsi kwenye mkutano uliohudhuriwa na maelfu ya watu jijini Mwanza.
 
"Kile kilichoonekana Mwanza kwa kina Bulaya na Lembeli ni rasharasha tu... kuna vigogo zaidi wako mbioni kuhamia upinzani na hili linachangia kwa kiasi fulani kutangazwa kwa jina la mgombea wa Ukawa," chanzo hicho kilieleza.
 
Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, ni miongoni mwa vigogo wa CCM wanaotajwa zaidi  kupitia mijadala mbalimbali ya kwenye mitandao ya kijamii kuwa ni miongoni mwa vigogo watakaohamia Ukawa. 
 
Wakati CCM ikikamilisha mchakato wa kumpata mgombea wake na kumtangaza John Magufuli kupeperusha bendera yao katika uchaguzi mkuu tangu Julai 12, Ukawa wameendelea kuwa na kibarua kigumu cha kukamilisha kazi hiyo. 
 
Awali ilidaiwa kuwa Chadema, NCCR-Mageuzi na NLD walishafikia hatua nzuri lakini wakalazimika kuwasubiri wenzao wa CUF ili nao waridhie kupitia kikao chao cha Baraza Kuu kilichofanyika juzi visiwani Zanzibar.
 
Uchaguzi Mkuu nchini unatarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu ili kumpata rais wa awamu ya tano atakayemrithi Rais Jakaya Kikwete aliyeingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate