EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, May 29, 2015

SABABU 10 ZA MASTAA WA KIKE KUTODUMU KWENYE NDOA!


Na Hamida Hassan
Mastaa wengi wamekuwa hawadumu kwenye ndoa zao na wengine kwenye uhusiano wao wa kimapenzi. Ukijaribu kumuuliza kijana yeyote mwenye nia ya kuoa atakuambia bora aoe mwanamke wa kawaida kuliko staa.
Mkali katika tasnia ya filamu Bongo, Yobnesh Yusuph 'Batuli'.
Si suala la kuoa tu, hata kwenye mapenzi ya kawaida ni wachache wanaoanzisha uhusiano na mastaa wakiwa na ndoto za kudumu kwa muda mrefu. Ukiona kijana ‘anamsalandia’ staa ujue ni ili amuonje tu kisha amtose.
Pia ukifuatilia utagundua kuwa, mwanamke wa kawaida akitokea kumpenda staa wa kiume, anatafuta ile sifa ya kuwa naye lakini anajua hawezi kudumu naye.Kutokana na hilo sasa, makala haya yanajaribu kukupa kwa ufupi sababu 10 ambazo zinawafanya mastaa wengi wa kike kutodumu kwenye ndoa.
Tamaa
Hili lipo sana kwa mastaa wa kike. Baadhi yao wana tamaa ya kuwa na maisha f’lani ili waonekane nao wamo wakati uwezo haupo. Matokeo yake sasa akiolewa na mwanaume ambaye hana kitu, akimpata wa pembeni ‘pedeshee’ wa kumtunza, kwa tamaa zao hujikuta wakisaliti.
Unakuta msichana kwa kuwa ni staa, anataka awe na gari zuri, abadili nguo kila siku, simu kali na vitu vingine vya thamani wakati pesa hana na mume naye ni kapuku. Hapo ndipo wengi huamua kuchepuka na matokeo yake sasa hajali tena ndoa.

Ustaa mwingi
Mastaa wengi wakishajitambua kuwa wao maarufu, basi hata kwa wapenzi wao wanaleta zile nyodo za ustaa. Wanasahau kuwa hata rais anapokuwa na mkewe humnyenyekea kama mke na mambo mengine kuendelea.
Utakuta staa anataka kuonesha ustaa wake kwa mumewe, yaani anataka mume awe chini yeye awe juu kisa tu anatikisa jiji.
Halima Yahaya ‘Davina.
Unyenyekevu katika mapenzi unakuwa haupo, eti anajipa imani kwamba hata akiachwa kwa kuwa anapapatikiwa na wanaume wengine kutokana na ustaa wake, hatakosa wa kumchukua. Hiyo ni dhana potofu!
Uvivu, kupenda kulala…
Baadhi ya mastaa hata wakiolewa wanashindwa kuvaa joho la ‘mke wa mtu’. Wanapenda kukaa tu na kuletewa kila kitu nyumbani. Akicheza muvi moja na kujulikana basi anaona dunia ndiyo yake, hakumbuki kutafuta kazi ya uhakika.
Usiku atapenda atoke, mchana ni mtu wa kulala tu kisa kachoka. Ni mwanaume wa aina gani atakayemvumilia?
Starehe kwa sana
Mke wa mtu hata kama anastahili kustarehe siku mojamoja, lakini baadhi ya mastaa walioingia kwenye ndoa huona wao starehe lazima ichukue sehemu kubwa ya maisha yao. Atalazimisha kila siku watoke na hata kama mume atakuwa si mtu wa kuendekeza mambo hayo, yeye ataomba awe anaenda na mastaa wenzake, akikataliwa inakuwa tatizo.
Hawajitambui
Mastaa wengi wanakosa elimu ya kujitambua. Ndiyo maana wengi wanaitwa malimbukeni. Unakuta staa amepata mume mzuri tu lakini yeye anashindwa kujitambua kuwa yeye ni mke wa mtu asiyestahili kuingiza ustaa wake kwenye maisha yake ya nyumbani.
Ndoa fasheni
Jaribu kuchunguza utagundua kuwa, mastaa wengi wanaolewa kama fasheni. Utamkuta staa wa kike anasema wazi kwamba, amechangia wengi sana hivyo na yeye anataka kuchangiwa hivyo analazimisha kuolewa.
Wanaoolewa kwa sababu hiyo ni wale ambao hata ndoa zao zikivunjika hawaoni hatari, wanaona ni sawa tu kwa sababu angalau wameonja ndoa!
Judith Wambura ‘Jide’.
Uvumilivu wa shida
Mara nyingi watu wanapooana hukubaliana kuishi pamoja kwa shida na raha. Mastaa wengi hawataki shida, wao wanataka raha tu.
Matokeo yake sasa ukiona mambo yanaenda kombo, ni wachache sana wanaoweza kuvumilia shida. Wengi wataanza visa na hatimaye wataomba talaka au kuamua kutoka kwenye ndoa!
Dhana potofu
dhidi yao
Mastaa wengi wanaonekana si watu wa kuolewa. Sasa anapotokea mwanaume wa kumuoa staa, hata kwenye mambo ya kawaida ataona anafanyiwa hivyo kwa sababu ya ustaa.Matokeo yake sasa, hata kama staa huyo atajitahidi ili adumu kwenye ndoa yake atashangaa ile damu ya ustaa inamtesa.
Wanakosa staha
Mke kama mke lazima awe na staha, kitu ambacho baadhi ya mastaa wanakikosa. Utakuta staa kaolewa lakini ana marafiki wengi wa kiume na anataka mume wake asihoji juu ya urafiki wao.Kama ni msanii akiwa lokesheni, afanyiwe lolote na wanaume, avae nguo hata za utupu kisa eti anaigiza. Mbaya zaidi si lokesheni, hata nje ya fani wanataka kuishi kisanii.
Jack Patrick.
Wako tayari kuachika
Mastaa wengi wa kike wakiolewa, wanakaa mkao wa kuachika wakati wowote. Ni wachache wanaofanya jitihada za kutunza ndoa zao. Yaani wanatembea kwenye ile dhana potofu kwamba staa hawezi kudumu kwenye ndoa.
Sababu hizo hapo juu na nyinginezo ndizo zilizosababisha ndoa za mastaa kama vile Nuru Nasoro ‘Nora’, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’, Jack Patrick, Aunt Ezekiel’, Salome Urasa ‘Thea’, Halima Yahaya ‘Davina’, Judith Wambura ‘Jide’, Stara Thomas na wengineo kuvunjika.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate