EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, April 25, 2015

Pengo aonya kuhusu urais, ashtushwa na wanaotumia fedha

Dar es Salaam.
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, ambaye alizua kizaazaa bada ya kutofautiana na maaskofu wenzake kuhusu Kura ya Maoni, jana alizungumzia suala la urais, akivitaka vyama vya siasa kuwaengua makada wake wanaotumia fedha kusaka urais.

Kardinali Pengo alisababisha mkanganyiko wakati alipotofautiana na tamko la Jukwaa la Wakristo lililotaka waumini waisome Katiba Inayopendekezwa, kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye Daftari la Wapigakura na siku ya Kura ya Maoni, wapige kura ya hapana kukataa mabadiliko hayo ya Katiba.
Tamko hilo lililotolewa na maaskofu wa madhehebu mbalimbali ya Kikristo, lilieleza sababu kadhaa za kupingana na mchakato wa kuandika Katiba Mpya, hasa suala la Serikali kuahidi kuingiza Mahakama ya Kadhi kwenye Katiba kwa lengo la kutaka Waislamu waipitishe Katiba Inayopendekezwa.

Lakini Kardinali Pengo akakosoa tamko hilo akisema waumini hawana budi kuachiwa kufanya uamuzi wao bila ya kushurutishwa, kauli ambayo ilisababishwa akosolewa na wengi, akiwamo Askofu Josephat Gwajima ambaye amefunguliwa mashtaka ya kumdhalilisha kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki.
Jana, Pardinali Pengo alizungumzia masuala ya kisiasa katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya saba ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph (SJUIT) ambako alionya dhidi ya matumizi ya fedha.
Akionya juu ya matumizi ya fedha katika harakati za kuingia Ikulu, Kardinali Pengo alisema kwa mujibu wa imani na kanuni za dini, uongozi ni baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu na 
“Kama wapo watu wanaotumia fedha kutaka kuingia Ikulu, ni bora wakaachwa mara moja na vyama vyao. Hata wasipitishwe na kuja kuomba kura kwetu. Ni vyema wakatambua kuwa uongozi haununuliwi,” alisema Pengo.
Alifafanua kuwa rushwa ni kitu kibaya kama itatumika kupata kiongozi katika ngazi yoyote ile na kwamba endapo mtoaji atapewa nafasi aitakayo, bila shaka gharama alizozitumia atataka zilipwe na wananchi anaowatumikia.
“Rushwa ni kitu ambacho kila kiongozi anapaswa kukiepuka ili kuwaondolea wananchi uwezekano wa kuingia katika mchakato wa kulipa deni ambalo kiongozi atataka alipwe (akiwa Ikulu) ingawa alitoa kwa hiari yake wakati wa kujinadi na kuwawishi wapigakura,” alisema. “Ni bora tumchague Rais maskini ambaye hatakuwa na madeni binafsi ya kuyalipa na kwa pamoja tuelekeze nguvu zetu katika ujenzi wa uchumi wa Taifa kwa ujumla. Watoa rushwa mwisho wa siku watataka tulipe gharama walizotumia kutushawishi,” alisema kiongozi huyo wa kiroho nchini.
Pamoja na hayo yote, Askofu Pengo alisema ni lazima ushindani uwepo kuanzia ndani ya vyama kabla havijapata mwakilishi atakayesimama kuviwakilisha mbele wa wananchi ili wachague anayefaa zaidi kulitumikia Taifa.
Alisema ni vyema demokrasia ikaanzia huko kabla haijahubiriwa nje kwani hilo huonekana kabla hata vyama hivyo havijasema namna vinavyojiendesha.
Askofu huyo ametoa kauli hiyo wakati Taifa likiwa kwenye mjadala kuhusu sifa za wagombea urais, huku kukiwa na malalamiko mengi, hasa kutoka chama tawala cha CCM, dhidi ya makada wanaotuhumiwa kutumia fedha kushawishi wanachama wao wawapitishe kuwania urais.

CCM, ambayo mgombea wake ndiye amekuwa akishinda urais tangu siasa za ushindani wa vyama ziliporejeshwa mwaka 1992, imekuwa ikieleza mara kwa mara kuwa makada hao hawatavumiliwa na vikao vya uamuzi vitawaondoa katika mbio za kuwania kuteuliwa kugombea urais.
Mapema wiki hii, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Phillip Mangula aliwaambia viongozi wa chama hicho mkoani Dar es Salaam kuwa fedha zinazotumiwa na makada kununua wanachama “kama maandazi”, zitakuwa kitanzi chao kwenye Uchaguzi Mkuu, akisisitiza kuwa wanachama hao watang’olewa.
Hata hivyo, chama hicho kimekuwa hakiripoti vitendo hivyo kwenye vyombo vilivyoundwa kwa ajili ya kuzuia na kupambana na rushwa na juzi, Takukuru ilisema chama hicho kikitoa ushirikiano, itaweza kukomesha uovu huo.
Akizungumzia demokrasia ndani ya vyama, Kardinali Pengo alitaka wagombea wengi zaidi kujitokeza ili kuwapa wananchi wigo mpana wa kuteua mtu anayefaa.
“Wajitokeze wengi zaidi ndani ya vyama vyao. Endapo vyama hivi vitadhihirisha demokrasia baina ya wanachama wao, ni dhahiri itakuwa sifa ya ziada kwa wananchi ambao ndiyo wapigakura wenye uamuzi wa mwisho,” alisema Kardinali Pengo.
Afya yake
Kwa muda wote wa sherehe hizo, Kardinali Pengo alikuwa ameketi kutokana na afya yake kutokuwa nzuri ikiwa ni muda mfupi tangu atoke India kwa matibabu ya mgongo na alitumia fursa hiyo kuwatoa hofu wote kuhusu hali yake.
Alisema kuwa maradhi hayo yalianza tangu mwaka 2013 na baada ya kwenda Ujerumani alibainika kuwa na tatizo hilo ambalo baadaye alishauriwa akatibiwe Hospitali ya Manipal iliyopo Bangalore, India.
“Ninaendelea vizuri. Maumivu yamepungua kwa kiasi kikubwa. Naomba wote wanaonitakia mema wasiwe na wasiwasi kwani matibabu niliyopata yalikuwa mazuri na yenye msaada mkubwa kwangu,” alisema kiongozi huyo ambaye anatembelea mkongojo.
CHANZO; MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate