EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, March 27, 2015

WANAKWAYA: JOKATE ANATUTIA AIBU

Hamida hassan
Ile skendo ya kupiga picha za nusu utupu na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii huku midume ikijirushia na kujifaidia kwa macho, ukijumlisha aibu mpya ya kukata mauno mbele ya wanaume, staa mwenye jina kubwa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ amewakera wanakwaya wenzake ambao wamedai kuwa anawatia aibu, Ijumaa lina mchapo kamili.Staa mwenye jina kubwa Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
TUJIUNGE KANISA LA SAINT PETER, OYSTERBAY, DAR
Ishu ya Jokate kutupia picha za nusu utupu mitandaoni si mpya, mara kadhaa amekuwa akiripotiwa kwa tabia yake hiyo kiasi cha kuwakera wanakwaya hao wa kanisa analosali la Saint Peter lililopo Oysterbay jijini Dar.
Mbali na picha hizo, safari hii anaandamwa na skendo mpya ya kudaiwa kukata mauno mbele ya midume anapokuwa kwenye shoo zake baada ya kutumbukia kwenye muziki wa Bongo Fleva.
AJADILIWA KANISANI
Kwa mujibu wa baadhi ya wanakwaya hao, wamekuwa wakimjadili mara kwa mara hasa wanapokuwa mazoezini kanisani hapo mara baada ya mmoja wao kurushiwa picha za mwanadada huyo kwenye mitandao ya kijamii.
NI AIBU KWA KANISA?
Baadhi ya wanakwaya hao walikwenda mbele zaidi na kudai kwamba mbali na kuwa ni kioo cha jamii lakini bado ni alama ya kanisa hivyo ni aibu kwa kanisa pia kwa sababu binti aliyelelewa kidini kama Jokate hawezi kuwa na tabia za aina hiyo.
Jokate akiwa kwenye pozi.
AU BIASHARA MATANGAZO?
Kuna baadhi walidai labda mwanadada huyo anafanya hivyo ikiwa ni njia ya kujitangaza yeye na biashara yake bila kujali kama anaweza akajiondolea ute wake na heshima aliyoijenga kwa miaka mingi.

“Ukweli ni kwamba Jojo (Jokate) anatutia aibu maana malezi ya kidini hayapo hivyo. Anatakiwa kuwa mfano wa kuigwa na watu wote.
USHAURI WA BURE
“Sisi tunamshauri arudi awe kama zamani kwani alikuwa binti wa mfano kanisani. Hakuna mtu wa kuonesha maumbile yake muhimu hadharani. Kwanza alipoingia kwenye mambo ya muziki ndiyo hali imekuwa mbaya maana ukiona video zake hutamani kuziangalia na watu wenye heshima zao,” alisema mmoja wa wanakwaya hao kwa niaba ya wenzake huko akiomba chondechonde kutotajwa gazetini.
Mwingine akasema: “Unajua Jokate niliyekuwa namjua mimi siyo huyu, siyo huyu wa kupiga picha hizi chafu, kwa kweli ni aibu kwake na kwetu pia kwani tunaonekana huenda tukiwa kanisani tunaficha makucha yetu, abadilike.”
JOKATE AJITETEA
Akizungumza na Ijumaa juu ya sakata hilo, Jokate alifunguka kuwa, kanisa analosali halimzuii kukata mauno jukwaani kwani anachofanya yeye ni kazi kama kazi nyingine.Jokate ambaye ndiye mmiliki wa bidhaa za ‘brandi’ ya Kidoti alisema kwamba, huwa anakwenda kanisani kama kawaida na kwaya anaimba kama siku zote na hilo haliwezi kumzuia kufanya kazi yake ya muziki na kukata mauno.
MAUNO KWA WINGI YANAKUJA
Jokate alisema kuwa ngoma yake mpya aliyokuja nayo hivi karibuni ya Leo Leo aliyomshirikisha Ice Prince wa Nigeria ndiyo imemdatisha na watu watarajie mauno kwa wingi kwani amejipanga vilivyo.“Mashabiki wangu wakae mkao wa kula kwani mauno ya sasa si mchezo, ni hatari tupu, nimedata na huu muziki, kiukweli nitajiachia kuliko siku zote,” alisema Jokate ambaye pia ni mwigizaji wa sinema za Kibongo.
CHANZO: IJUMAA

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate