EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 28, 2015

UCHAWI WAFUMULIWA SOKONI

CHANZO: RISASI JUMAMOSI/GPL
WE acha tu! Sangoma mmoja aliyejulikana kwa jina la Mohamed Chimwaganje (44), amezua kizaazaa katika Soko la Kapera lililopo Mwembechai jijini Dar kufuatia kufumua vitu chini ya ardhi vinavyodhaniwa ni vya ushirikina,  Risasi Jumamosi linakujuza.
Sangoma Mohamed Chimwaganje akishika hirizi aliyoitoa katika Soko la Kapera lililopo Mwembechai jijini Dar.
Tukio hilo la aina yake lilijiri asubuhi ya Machi 25, mwaka huu katika soko hilo ambapo awali taarifa zilimfikia sangoma huyo kwamba, baadhi ya  wafanyabiashara wa soko hilo wamekuwa wakiibiwa pesa zao kwa njia ya maajabu  .
MFANYABIASHARA AZUNGUMZA
Akizungumza na Risasi Jumamosi, mmoja wa mashuhuda sokoni hapo alisema kuwa, ilifika wakati wafanyabiashara hao walikuwa hawaingizi faida wakiwa sokoni hapo na wanaweza wakauza lakini kwenye mahesabu jioni, pesa kibao zimepotea, hivyo kusababisha wengi kuacha biashara baada ya kufilisika.
“Lakini cha kushangaza ni kwamba, baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo wamekuwa wakiuza sana vitu visivyokuwa na ubora na vile vyenye ubora kuachwa na wateja ambapo mwishowe huharibika na kutupwa.“Basi, kutokana na hali hiyo tukaamua kumwomba huyo mtaalamu ‘sangoma’ aje afanye mambo yake maana tunamwamini kwa sababu  ameshamponya uchizi mtu mmoja wa hapa mtaani,” alisema mfanyabiashara huyo akikataa kutaja jina lake gazetini.

Moja ya hirizi iliyotolewa katika soko hilo.
UMATI WAMZUNGUKA SANGOMA
Waandishi wetu wakiwa eneo la tukio walishuhudia umati sokoni hapo ukiwa umemzunguka sangoma huyo ambapo alipandisha mzuka wake na kusema kuna wafanyabiashara wanne ambao wamechimbia hirizi sokoni hapo ili kukusanya fedha za wenzao kwa njia ya chuma ulete.
Sangoma huyo aliendelea kusema kuwa, kazi ya hirizi hiyo ni kutoa kafara ya kuua mtu yeyote anayepita sokoni hapo kila baada ya miezi sita lakini pia kuna chungu ambacho kimekuwa kikikusanya fedha hizo, maneno yaliyowafanya wateja sokoni hapo wapigwe butwaa.
SANGOMA AANZA KUFUMUA
Baada ya kusema hayo, Risasi Jumamosi lilimshuhudia sangoma huyo akianza kuchimba ardhi katikati ya soko hilo na chini yake kwenye shimo alitoa hirizi hiyo iliyozungushwa ushanga.Sangoma aliimwagia maji maalum hirizi hiyo. Alisema maji hayo ni moja ya dawa zake za kupoza makali ya hirizi na kisha akaiteketeza kwa moto.

...Sangoma akiichoma hirizi hiyo.
USHIRIKINA MWINGINE
Ukiacha mbali hirizi, vitu vingine alivyoviibua sangoma huyo ni meno ya samaki hatari baharini aitwaye  papa, chupa kadhaa za pafyumu zilizochanganywa na maji ya maiti za watu na paka ambao hutumika pia kuchukua bidhaa kimazingara sokoni hapo.

MZUKA WA SANGOMA WAPOA, AONGEA NA RISASI JUMAMOSI
Risasi Jumamosi lilisubiri mzuka wa mganga huyo utulie ndipo likazungumza naye ambapo katika maelezo yake alisema hirizi aliyoiibua ardhini  ilitengenezwa kwa kutumia sehemu za siri za wanawake ambao hawajazaa.“Inavyotokea ni kwamba, maiti za wanawake hukatwa kwa siri wakati wa kuoshwa na watu wa mochwari kabla ya kuuzwa kwa watu wanaozitumia kishirikina,” alisema sangoma huyo.
Wateja waliokuja kununua bidhaa sokoni hapo wakishuhudia tukio hilo.
NI MEZA KWA MEZA
Sangoma alisisitiza kuwa, oparesheni hiyo itakuwa meza hadi meza pamoja na kuwaumbua wale wote wenye tabia za kishirikina na hatamuogopa mtu wala yeye haogopi kufa kwa vile mizimu yake imemtuma kuwasaidia wote wenye matatizo kulingana na anavyoelekezwa.

Imeandaliwa na: Deogratius Mongela, Chande Abdallah na Mayasa Mariwata

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate