EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 28, 2015

MZIMU WA KANUMBA WADAIWA KUUA WAWILI

mwandishi wetu
HII ni habari ya kutisha! Takriban miaka mitatu imekatika tangu kifo cha aliyekuwa staa wa Bongo Movies, Steven Kanumba huku watu wawili wakifariki dunia kwa nyakati tofauti lakini nyuma ya pazia ya vifo vyao, mzimu wa Kanumba unatajwa kuhusika kutokana na watu hao kutaka kuishi mahali pa marehemu huyo, endelea kusoma Risasi Jumamosi.
Aliyekuwa staa wa Bongo Movies, marehemu Steven Kanumba.
SOMA TUKIO HILI LA KUSHANGAZA
Itakumbukwa kwamba, baada ya kifo cha Kanumba, mama yake mzazi, Flora Mtegoa ndiye aliyeshika jukumu la kusimamia mali za marehemu mtoto wake (alikuwa na haki).
Miongoni mwa mali hizo ukiachilia mbali, magari, vifaa vya kurekodia filamu, viwanja na filamu zilizokuwa hazijalipwa, mama Kanumba aliimiliki ofisi ya Kanumba iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Kanumba The Great Film iliyokuwa Sinza.Hata hivyo, hivi mapema Februari, mwaka huu, mama Kanumba alitoa vitu kwenye ofisi hiyo kwa madai ya kushindwa kulipa pango, hivyo ofisi ikawa wazi.

KILICHOTOKEA SASA
Habari ambazo gazeti hili ilizipata zilidai kwamba, mpangaji mwingine aliikodisha ofisi hiyo kwa mkataba wa mwaka mmoja lakini hivi karibuni mtu huyo amefariki dunia.Msikilize shuhuda: “Kuna jamaa alipanga kwenye ofisi iliyokuwa ya Kanumba mara tu baada ya mama Kanumba kuondoka vitu kwa kushindwa kulipia mkataba mpya.
“Huyo jamaa alikuwa anahusika na masuala ya ujenzi. Jamaa alilipia kodi ya mwaka mmoja, akawalipa watu wamfanyie usafi yeye akaenda ‘saiti’ kwenye mambo yake ya ujenzi. Inadaiwa akiwa kule, kuna ‘kijiko’  kilichokuwa kinachimba kiwanja, bahati mbaya kikarudi nyuma na kumgonga, akaanguka na kufariki dunia.”
JE, NI MZIMU WA KANUMBA?
Kifo cha mtu huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, kinaunganishwa na tukio lilitokea mwaka juzi baada ya kifo cha Kanumba kilichotokea  Aprili 7, mwaka 2012.Mara baada ya Kanumba kufariki dunia ghafla, mwanamke mmoja alikwenda kupanga nyumba ile aliyokuwa akiishi marehemu iliyopo Sinza, Dar, naye alifariki dunia ghafla.
MAJIRANI WALIZUNGUMZA
Wakati wa tukio hilo, wanahabari wetu walifika nyumbani kwa mwigizaji huyo ambapo walizungumza na majirani wakaelezea juu ya uwepo wa tukio hilo.Walisema japo hawaamini juu ya imani za masuala ya mzimu wa marehemu lakini kitendo cha mwanamke huyo kufariki dunia muda mfupi baada ya Kanumba kufa kiliwafanya washtuke na kuamini kwamba huenda ni mzimu wa Kanumba ndiyo ulichukua roho ya mpangaji huyo.
Mama Kanumba, Flora Mtegoa.
WENGINE WALIAMINI HIVI
Hata hivyo, baadhi ya watu wengine pia walisema yao wakidai kwamba, wanaamini kifo cha mwanamke huyo ni cha kawaida kama ilivyo kwa vifo vingine.“Kama siku za Kanumba zilivyokuwa zimewadia na huyo mpangaji pia siku zake zilikuwa zimefika ndiyo maana amefariki dunia,” alisema mmoja wa majirani.
ALIVYOSEMA MZEE ALIYEKULA CHUMVI NYINGI
Mzee mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mohamed Sumali (76), mkazi wa Mabibo-Relini, Dar akizungumza na gazeti hili kuhusu mazingira ya vifo hivyo, alisema:“Ipo mizimu ya hivyo. Mtu akifa, wa kwanza kuhamia kwenye nyumba aliyokuwa akiishi marehemu naye anakufa. Lakini si kwamba nyumba ndiyo ina mizimu. Kama hivyo vifo vimetokea kweli basi na mzimu wa Kanumba umeshaondoka.”
MAMA KANUMBA AZUNGUMZA
Baada ya kuzipata habari hizo, mwanahabari wetu alimvutia waya mama Kanumba kutaka kujua kama anajua lolote juu ya marehemu mtoto wake kuacha mzimu ambao unahusishwa na vifo hivyo ambapo alikiri kusikia taarifa za kifo cha jamaa aliyepanga kwenye ofisi za Kanumba lakini akasema hata yeye hajui sababu za kifo chake.
“Hata mimi nimesikia,  lakini sielewi chochote kuhusiana na mtu huyo kufariki dunia. Imenishtua kwa kweli maana si unakumbuka hata kule alikopanga (Kanumba) mwanzoni nako aliyepanga ile nyumba naye alifariki? Sijui hata ni kwa nini?” alihoji mama Kanumba kwa sauti iliyoashiria kushangaa sana.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate