EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 27, 2015

NISAMEHE: HAKYANANI, NENO HILI LITAMWINGIZA LOWASSA IKULU


CHANZO: UWAZI MIZENGWE
KIPYENGA! Mpambano wa kuteuliwa na hatimaye kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu Oktoba, mwaka huu kuwania urais unazidi kushamiri huku jina la waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ‘EL’ likiongoza kutajwa midomoni mwa Watanzania.
Imebainika kuwa pamoja na  kelele nyingi zinazosikika mitaani za “Lowassa! Lowassa!” bado hazitoshi kumwingiza madarakani, kama Rais Kikwete hatamwona anafaa kuwa mrithi wake.
Lowassa alikuwa mmoja wa wanamtandao waliofanikisha kuingia ikulu kwa Rais Jakaya Kikwete ‘JK’ katika uchaguzi wa mwaka 2005. Baada ya JK kuingia ikulu,  Lowassa aliteuliwa kuwa waziri mkuu wa serikali ya awamu ya nne hadi alipojiuzulu, Februari 2008 kufuatia tuhuma za kashfa ya mkataba tata wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond.
Rais Jakaya Kikwete ‘JK’.
WANAMTANDAO WENGINE
Mbali na Lowassa, wanamtandao wengine waliofanikisha JK kuingia ‘magogoni’ ni Bernard Membe, Emmanuel Nchimbi, Abdulahman Kinana na Rostam Aziz.
Kwa utaratibu usio rasmi wa mitandao ya kisiasa duniani, Rais Kikwete baada ya kumaliza muhula wake wa miaka kumi anatakiwa kumrithisha kiti mmoja kati ya wanamtandao waliopigana kufa na kupona kumwingiza madarakani.

Miongoni mwa wanamtandao hao, Kinana ana kikwazo cha kugombea kwa sababu tayari amezunguka nchi nzima kukisafisha chama chake, wakati wenzake wakiwa wamepigwa kufuli, hivyo kitendo cha kuchukua fomu kitatafsiriwa kama aliwazuia wenzake ili yeye apate nafasi ya kujitangaza.
Mwanamtandao mwingine ni Rostam ambaye kwa sababu ya shughuli zake nyingi za kibiashara, hana ndoto za kuingia ikulu na kuongoza taifa. Hii inafanya wabaki wanamtandao watatu, Lowassa, Nchimbi na Membe.
Edward Ngoyai Lowassa.
Duru za kisiasa zinaonesha kuwa yeyote kati ya watatu atakayeungwa mkono na rais aliyeko madarakani anayo nafasi kubwa ya kuibuka rais kama atawashinda wagombea wa vyama vya upinzani.
Pamoja na kung’ara kwa Lowassa, wachambuzi wa siasa za ndani wa chama tawala na serikali wanampa nafasi ndogo ya kupenya kukiwakilisha chama chake kupambana na wapinzani kutokana na mambo kadhaa, lakini kubwa likionekana ni fununu za kutoungwa mkono ndani ya chama chake, hasa na baadhi ya viongozi wa juu.
Imedaiwa kuwa jambo pekee linaloweza kumfanya Lowassa akafanikiwa kuvunja kuta zilizoko mbele yake ni kuketi mezani na mwenyekiti wa chama chake (Kikwete), kufanya mazungumzo magumu juu ya tofauti zozote zilizopo ndani ya chama chake na ikibidi kuomba msamaha, afanye hivyo.
Kitendo cha Lowassa kuchelewa au kupuuza jambo hilo kinaweza kusababisha Rais Kikwete kumuunga mkono mtu mwingine miongoni mwa wanamtandao watakaochukua fomu kuwania nafasi hiyo jambo litakalofanya uwezekano wa yeye kuingia ikulu kuwa finyu.
NAPE AMETAJWA TOKA ZAMANI
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Nape Nnauye  anatajwa kuwa mpinzani ‘nambari wani’ wa EL huku mwenyewe akijitetea kwamba anachokifanya si kumpinga Lowassa bali ni kusimamia maadili ya chama chake.
Hivi karibuni, Nape alisema kuwa, rais ajaye lazima awe mwadilifu wa kutosha kwa vile licha ya nafasi hiyo serikalini, pia ndiye atakayekuwa mwenyekiti wa chama taifa.
RAIS NI RAIS TU!
Ingawa historia ya nchi ya Tanzania haimpi nafasi rais aliye madarakani kumpendekeza, kumteua au kumpitisha mtu anayemtaka ashike kijiti chake, lakini bado mfumo wa utawala unatoa nafasi kubwa kwa rais kushawishi kwenye ngazi husika ili kumpata mgombea wa kwenda kupambana na vyama vingine.
Vipo vikao rasmi na visivyo rasmi vinavyohusika katika kuwachuja wagombea, achilia mbali taasisi zingine za kiserikali zinazohusika kumpata mtu muafaka, hasa Usalama wa Taifa.Katika chama, majina yote ya wanachama wanaotaka urais yatapaswa kwanza kujadiliwa na Kamati Kuu (CC), ambako mwenyekiti wa kikao hicho ni rais aliye madarakani.
Kabla, baraza la wazee linalowajumuisha marais wastaafu, litahusika kupitia majina hayo ili kutoa baraka kabla ya CC.Ingawa EL anaonekana ana mtaji mkubwa wa watu, hiyo inaweza kuwa sababu isiyo na mashiko kwa sababu mfumo wa uchaguzi hauwapi wananchi nafasi ya kuwateua wagombea katika hatua za awali, badala yake Rais Kikwete anabaki kuwa na nguvu ya uamuzi kutokana na mamlaka aliyonayo kwenye mabaraza ya awali ya uteuzi.
Duru za kisiasa zinaeleza kwamba kabla ya baraza la wazee halijakaa kuwachambua wagombea wote wa nafasi ya urais, rais wa nchi huulizwa chaguo lake. Kwa hiyo kama JK  hatamwona EL anafaa kuwa mrithi wake hatampendekeza.
Kwa upande wa Kamati Kuu ambako rais ni mwenyekiti, ana nafasi kubwa ya kushawishi kuondolewa kwa jina asilolitaka kabla ya kupelekwa katika Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kwa ajili ya kupigiwa kura ya mwisho ya kupata wagombea watatu ambao watapelekwa kwenye Mkutano Mkuu wa CCM ili kumpata mmoja ambaye ndiye atakuwa mgombea wa CCM katika uchaguzi mkuu ujao.
Lakini hata kama ushawishi wake kwa wajumbe wa kikao hicho utashindwa kuliondoa jina asilolitaka, bado yeye kama mwenyekiti wa chama anayo turufu ya kuliondoa kwenye Mkutano wa NEC.
Nguvu hii ya ushawishi inafanya kitendo cha Lowassa kukaa meza moja na Kikwete kuwa cha lazima ili kufanya safari yake kwenda ikulu kuwa rahisi na laini.
Hata hivyo, ziko taarifa za kuwepo kwa wajumbe wa kamati kuu ‘maslahi’ ambao huangalia zaidi maisha yao ya baadaye kisiasa, ambao hupenda kuwekeza kwa kiongozi atakayeingia baada ya aliyepo kuondoka. Hawa wanaweza kuonesha kumuunga mkono rais lakini wakati wa kupiga kura wakageuka.
WAKATI HUOHUO
Wakati hilo likiendelea, Kamati Kuu ya CCM (CC), itategua kitendawili dhidi ya makada sita waliopewa adhabu ya mwaka mmoja kwa madai ya kuanza kampeni za kuwania urais ndani ya chama hicho kabla ya wakati.
Katika kikao hicho kitakachofanyika kesho Februari 28, jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Maadili ya CCM, Philip Mangula, atawasilisha ripoti yake ya tathimini dhidi ya makada hao kama walitii adhabu waliyopewa na chama ya kutojihusisha na kampeni mapema au la! Makada hao walipewa adhabu hiyo Februari 18, mwaka jana.
Katibu wa Nec, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ilisema juzi kuwa kikao hicho cha CC kitafanyika chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya CCM Mtaa wa Lumumba, Dar kiliiambia Uwazi Mizengwe ya Uchaguzi  kuwa, kwa siku kadhaa Kamati ya Mangula imekuwa ikifanya vikao vyake hadi usiku wa manane kuwajadili makada hao.
Makada hao ni Lowassa, waziri mkuu mstaafu awamu ya tatu, Frederick Sumaye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Steven Wasira, Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba na Mbunge wa Sengerema kwa tiketi ya CCM, William Ngeleja.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate