EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 20, 2014

MAXIMO RASMI ATUPIWA VIRAGO YANGA

 

Klabu ya Yanga na wawakilishi wa michuano ya shirikisho ya Afrika imewatupia virago rasmi makocha wabrazil Marcio Maximo na msaidizi wake, Leonardo Neiva kwa kile kinachoelezwa kutofurahishwa na mwenendo wa timu katika ligi licha ya kuwa na wachezaji wengi mastaa wa kigeni na kutumia mamilioni katika kusajili wachezaji mahiri wa kigeni.

Yanga hivi karibuni ilimsajili mrundi na mfungaji bora msumu uliopita, Hamis Tambwe kutoka kwa mahasimu wao (Simba) akiungana na Mliberia, Kpah Sherman, Wanyarwanda Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Mbrazil Andrey Coutinho kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni


Tayari uongozi wa Yanga, katika kile kinachoonekana pesa si tatizo, chini ya Mwenyekiti bilionea Yusuf Manji umemrudisha klabuni aliyekuwa kocha wa zamani, Mholanzi Van de Pluijm, atakayesaidiwa na kocha mzalendo na mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa na klabu hiyo, Charles Boniface Mkwasa.
Katika maelezo yake, Manji amewatakia kila la kheri wabrazil hao na kusema na mungu akipenda wataendelea kushirikiana nao katika siku za usoni.
 
Alama ya wana Jangwani
Tayari makocha hao wawili , Pluijm na Mkwasa wameshatambulishwa kwa wachezaji wa Yanga na habari za uhakika kutoka klabu hapo zinasema baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu, Pluijm, aliyewahi kuipatia yanga mafanikio katika ligi kuu, ana anza kibarua chake rasmi leo.
Hata hivyo, kuondoka kwa Maximo, aliyewahi kuajiriwa na Serikali ya Tanzania kama kocha mkuu wa timu ya taifa, Stars Stars katika miaka ya nyuma na kurudi nchini kivingine kuongoza Yanga, kumegubikwa na sintofahamu huku kukiwa na habari kuwa bado anavutana na uongozi juu ya mafao yake kwa kuvunjiwa mkataba.
Maximo, aliiongoza Yanga katika mechi tisa ndani ya miezi mitatu (akipoteza mechi mbili katika mechi saba) baada ya kupokelewa kwa shangwe uwanja wa ndege alipowasili kuwafundisha mabingwa hao wa zamani wa Tanzania.
Inasemekana kuondolewa kwake kunatokana na kipigo cha mabao 2-0 Yanga ilichokipata baada ya kufungwa na watani wao wa jadi, Simba katika mechi isiyo ya ligi (Nani Mtani Jembe) chini ya kocha Mzambia Patrick Phiri.
Maximo anakuwa kocha wa pili kufukuzwa na Yanga baada ya matokeo mabaya ya mechi ya Nani Mtani Jembe. Kocha kutoka Uholanzi, Ernie Brandts, pia alifukuwa baada ya kupata kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Simba .

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate