EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, November 24, 2014

MINOTI YA ESCROW INAUMA SANA!

Stori: Ojuku Abraham
THIS is not fair (Hii siyo sawa)! Tunaweza kufumba macho na kuacha kusema kinachoendelea katika baadhi ya ‘madudu’ serikalini, lakini linapokuja suala la uchotwaji wa Sh. bilioni 306 za umma kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow, tuache masihara, minoti hiyo iliyoibwa na wajanja wachache, inauma sana, Ijumaa Wikienda linakudadavulia zaidi.
Mfano wa burungutu la fedha yaliyochotwa Benki Kuu.
KWANZA ESCROW NI NINI?
Tunajua wengi wanafahamu kinachoendelea kuhusu Escrow ambapo sasa limekuwa gumzo ndani ya bunge na kwenye mijadala mbalimbali ya wananchi wa kada tofauti lakini si vibaya tukaijua zaidi kwani inadaiwa sakata hilo linampa wakati mgumu Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Akaunti ya Tegeta Escrow ilifunguliwa na serikali ili kuhifadhi fedha za umma baada ya Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) kuingia mkataba wa kununua nishati ya umeme kutoka Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) mapema miaka ya 2000.
Baadaye Tanesco iligundua kwamba, bei ya umeme wanayouziwa na kampuni hiyo ni kubwa, hivyo walikwenda kuipinga katika mahakama ya kibiashara.
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda.
ILIVYOFUNGULIWA SASA
Wakati mvutano huo ukianza, ndipo serikali ilifungua akaunti hiyo kwenye Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambako Tanesco iliweka fedha ilizokuwa ikizilalamikia kwa ajili ya kuilipa IPTL kama tozo ya umeme (capacity charges) hadi hapo mahakama itakapotoa uamuzi juu ya kama kweli bei hiyo ilikuwa halali kwa Tanesco au la!
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
WAJANJA WAZICHOTA
Lakini wakati shauri hilo likitua kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Utatuzi wa Migogoro ya Kibiashara (UCSID) na uamuzi ukiwa bado haujatolewa, inadaiwa Wizara ya Nishati na Madini iliidhinisha fedha hizo zitolewe BoT na kulipwa Kampuni ya PAP ambayo ilishainunua IPTL, wizara ilidaiwa kuamini Tanesco wangeshindwa kesi hiyo.
Zitto Kabwe ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).
Hukumu ilipotoka, Tanesco waliibuka na ushindi na kutakiwa kulipwa fedha kibao lakini walipokwenda kuchungulia kwenye akaunti walikuta hakuna kitu, sakata likaanzia hapo sasa.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.

NI FEDHA NYINGI KIASI GANI?
Kwa utafiti uliofanywa na gazeti hili, shilingi bilioni 306 ni fedha nyingi kiasi kwamba kama zikipangwa katika chumba chenye ukubwa wa futi 10 kwa 10, vitahitajika vyumba viwili vilivyojaa kuanzia chini hadi juu pasipo na pangaboi.
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila.
INAUMA JAMANI
Kama hiyo haitoshi, hesabu zinaonesha, endapo kijana mwenye umri wa miaka 18 sasa, aliyemaliza elimu ya kidato cha nne na yupo tayari kuanza maisha, akipewa sehemu ndogo tu ya fedha hizo halafu akafanya matumizi ya kufuru bila kufanya kazi wala biashara yoyote, ataweza kufa akiwa na miaka 75 huku akibakisha chenji kubwa.
Kwamba, endapo kijana huyo atatumia shilingi laki tano (500,000) kila siku (watumishi wengi wa serikali wanalipwa chini ya kiwango hiki) kwa mwaka mzima wenye siku 365, atakuwa ametumia shilingi milioni 182.5 tu!

UFAFANUZI WAKE
Maana yake ni kwamba hadi atakapofikisha umri wa miaka 75, ikiwa ni miaka 57 tangu aanze kutumbua fedha hizo akiwa na miaka 18, atatumia shilingi bilioni 10.4 tu, sawa na asilimia chini ya sifuri ya mabilioni hayo ambayo baadhi ya wakubwa ‘wamejisevia’. Kweli inauma sana!

WABUNGE WALIOICHARUKIA
Kashfa hiyo imeshikiwa bango na wabunge karibu wote wa kambi ya upinzani na baadhi kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM), ingawa wanaoonekana kuwa vinara ni pamoja na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ambaye ndiye aliyeibua kashfa hiyo.
Kafulila, ambaye Jumamosi iliyopita alifunga ndoa nyumbani kwao Kigoma, alisababisha purukushani kubwa ndani ya bunge alipoibua sakata hilo kiasi cha kutaka kupigwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.

KINA NANI KIKAANGONI?
Sakati hili limewakalia vibaya baadhi ya vigogo serikalini, akiwemo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda anayedaiwa kutumika ili kuifunika ripoti ya CAG isijadiliwe bungeni, Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo, Katibu Mkuu wake, Eliakim Maswi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, Gavana wa Benki Kuu, Benno Ndullu na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Anna Tibaijuka.
Wengine wanaohusishwa na kashfa hiyo baada ya kubainika kupewa mgao wao kupitia kwa mmoja wa watuhumiwa ni pamoja na waziri wa zamani wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Mwanasheria Mkuu wa serikali wa zamani, Andrew Chenge.

KITAELEWEKA KESHOKUTWA
Hatima ya vigogo wanaotuhumiwa kuchota mabilioni hayo ya fedha inatarajiwa kujulikana Novemba 26, mwaka huu (keshokutwa) wakati ripoti ya uchunguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) itakapopiga hodi bungeni na waheshimiwa kuanza kuijadili.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate