EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 22, 2014

VITA NZITO: ALI KIBA VS DIAMOND, CLOUDS VS TIMES

Stori: Erick Evarist, Musa Mateja na Chande Abdallah
MTIFUANO! Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 limepita lakini nyuma yake limeacha vita nzito iliyowahusisha mafahari wawili, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Ali Kiba huku waandaaji wa tamasha hilo, Clouds FM wakisigana na Times FM kumgombea msanii wa Nigeria, David Adedeji Adeleke ‘Davido’, Risasi Mchanganyiko linakupa mchongo kamili.
Msanii wa Bongo Fleva, Ali Kiba akipafomu.
TIFU LILIVYOKUWA
Kwenye shoo hiyo iliyofanyika wikiendi iliyopita katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar, mashabiki wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Ali Kiba (Team Kiba), walipiga kelele za ‘buuu’ pale alipopanda Diamond kutumbuiza ili kumharibia.
CHANZO CHANENA
Chanzo makini kimedai kuwa, vurugu hizo hazikutokea kwa bahati mbaya bali zilipangwa na wafuasi wa Kiba ambapo inasemekana ziliandaliwa gari aina ya Toyota-Costa zipatazo 25 zilizokuwa zimejaa watu na kwenda kuwamwaga viwanjani hapo kwa shughuli mbili muhimu; kuzomea na kuhamasisha wengine wazomee pindi Diamond atakapopanda jukwaani.

Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akifanya shoo na Davido wa Nigeria
“Ishu ilipangwa, Team Kiba waliibuka na Costa kama 25 hivi, wakajipanga katika maeneo tofauti ya uwanja huo lakini zaidi walikaa karibu na jukwaa ili kuweza kutimiza vizuri azma yao ya kuharibu pindi Diamond atakapokuwa akitumbuiza,” kilidai chanzo hicho.
WALIFANIKIWA?
Kwa namna moja mashabiki hao walionekana kufanikiwa kwani waliweza kuwashawishi watu wengi wazomee kiasi cha kumfanya Diamond ashtukie  na kuamua kutamka hadharani: “Jamani kuna uhuni unaendelea hapa.”
Mkurugenzi wa Times FM, Rehure Nyaulawa.
TEAM DIAMOND WACHARUKA
Madai yanasema mara baada ya Team Kiba kufanya vurugu hizo na kufanikiwa, baadhi ya mashabiki ambao waliaminika ni wa Diamond (Team Diamond), walicharuka na kusema hawakubaliani na uhuni huo ambao umefanywa hivyo watahakikisha wanapambana kulipiza kisasi kwa namna yoyote ile.
“Hatukubali, wao si walijipanga hapa kumharibia Diamond, sasa na sisi tutahakikisha tunalipiza kisasi kwa namna yoyote,” walisikika wakisema mashabiki wa Diamond.
TALE AKIRI KUSIKIA
Paparazi wetu aliwatafuta Diamond na Kiba ili kujua wanazungumziaje vurugu hizo. Baada ya kumtafuta Diamond bila mafanikio, alipatikana meneja wake, Hamis Taletale ‘Bab Tale’ ambaye alikiri kuwepo kwa maandalizi ya zomeazomea ambayo yalikuwa na lengo ya kumharibia msanii wake.
Mkurugenzi wa Vipindi Clouds FM, Ruge Mtahaba.
“Hizi kwetu tumezichukulia kama changamoto, tulisikia kwamba kuna watu wamelipwa kwa ajili ya kufanya fujo lakini hatukujali sana kwani lengo letu si kugombana na mtu, sisi tunafanya muziki mzuri ambao ndoto zetu ni kuufikisha katika levo za Kimataifa,” alisema Bab Tale.
KIBA ANAHUSIKA?
Alipotafutwa Kiba kuzungumzia suala hilo alikataa kuhusika nalo na kudai halina ukweli wowote kwani si rahisi kuwalipa pesa mashabiki wengi kiasi kile waliojitokeza uwanjani.
“Hiyo si kweli ni uzushi tu, sasa mimi nitawalipa nini hao mashabiki wote waweze kumzomea huyo Diamond? Siyo rahisi. Kwanza mimi nifanye hivyo ili iweje? Mimi si mtu wa kushindana na Diamond hata siku moja, nafanya muziki wangu, mashabiki wanauelewa, nashukuru Mungu kwa hilo,” alisema Kiba.
CLOUDS FM VS TIMES FM
Kwa upande mwingine, vita nzito ilizidi kutokota kupitia tamasha hilo baada ya msanii Davido kupanda jukwaani na kutumbuiza ilhali akiwa amewekewa pingamizi la kibali kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) sambamba na zuio la Mahakama ya Kisutu lililowekwa na Redio Times FM waliodai kuwa na mkataba wa kufanya shoo na msanii huyo Novemba, mwaka huu Bongo.
TIMES WANASEMAJE?
Mkurugenzi wa Redio Times FM, Rehure Nyaulawa alipotafutwa kwa simu kuhusiana na suala hilo alisema mahakama ilishaweka pingamizi, anashangaa kuona msanii huyo alipanda jukwaani lakini akasema hawezi kukaa kimya, atakwenda mbele zaidi ili haki itendeke.
CLOUDS JE?
Kwa upande wao, Clouds walipotafutwa hawakupatikana hewani lakini kimsingi na wao wana hoja zao ambazo zitabainika pindi kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa.
Hata hivyo, kuna madai kwamba, zuio la Davido kutopanda jukwaani Leaders Club lilipelekwa na mahakama kwa Clouds Media Group wakati Tamasha la Fiesta linaandaliwa na Kampuni ya Primetime Promotion, kwa hiyo barua hiyo ilikuwa ‘missing in action’.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate