EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, October 30, 2014

SIYO DHAMBI KUMPENDA MPENZI WA MWENZAKO ILA FANYA HIVI…

Utafiti ambao umefanyika unaonesha kuwa, asilimia kubwa wapo kwenye uhusiano na watu ambao siyo waliopangiwa na Mungu kuwa nao.Kutokana na hilo ndiyo maana utakubaliana na mimi kwamba, usaliti umekuwa ukishamiri, watu wamekuwa wakiachana kila siku na wengine kuendelea kuishi pamoja lakini si kwa amani.
Hii ni kwa sababu wameingia kwenye penzi na watu ambao si sahihi. Kutokana na mazingira hayo, haiwezi kuwa kitu cha ajabu mume wa mtu kutokea kumpenda sana mke wa mtu au kinyume chake.
Pia huwezi kuonekana mwendawazimu kwa kumpenda mtu ambaye tayari ana mpenzi wake. Hii ni kwa sababu inawezekana una mapenzi ya kweli zaidi kwake kuliko huyo aliye naye. Hata hivyo, hakuna kitu kibaya kama kuanzisha uhusiano na mtu ambaye tayari ana mpenzi wake au ameshaingia kwenye ndoa. Utakuwa unatafuta matatizo kama utamtongoza mke wa mtu au utaonesha kumzimikia mume wa mtu na kujikuta ukishawishika kutaka kumpasulia ukweli.

Madhara yake ni makubwa kwani kuingilia uhusiano wa watu kunaweza kuyagharimu maisha yako. Wapo ambao wameuawa kwa kuwapenda wake za watu. Yawezekana si kwa u-kiwembe wao bali mapenzi ya kweli waliyonayo lakini ukweli unabaki kwamba, unayempenda tayari ana mtu wake, wewe huna jinsi tena.  Itakubidi ubaki ukiumia moyoni huku wakati mwingine ukiomba hata waachane ili wewe uweze kuchukua nafasi. Hiyo inatokea sana huko mtaani.
Sasa basi, ni yapi ambayo unatakiwa kuyafanya pale ambapo umetokea kumpenda mtu ambaye tayari ana mtu wake? Kwanza kabisa, hakikisha unafanya kila uwezalo ajue kile kilichomo moyoni mwako. Tumia mbinu yoyote kumpata na kumpasulia ukweli. Utamueleza jinsi unavyompenda na namna anavyokukosesha amani lakini mwisho wa siku mweleze kwamba humaanishi aachane na huyo aliyenaye bali kokote atakakoenda ajue yupo mtu f’lani, sehemu f’lani anampenda.
Ukifanikiwa kufanya hivyo, angalau unaweza kubaki na amani. Kunaweza kuwa na ugumu kumpata kutokana na mazingira hasa ukichukulia kwamba kunatakiwa kuwe na usiri mkubwa sana kwenye kufikisha ujumbe huo. Pili, hakikisha unaonana naye mara kwa mara. Hiyo angalau itakupunguzia machungu hasa kama na yeye atakuwa na chembechembe za kukupenda.
Ukibahatika kuonana naye akiwa peke yake, msalimie kwa kumchangamkia huku ukionesha kufarijika kukutana na mtu ambaye ana nafasi kwenye moyo wako. Tatu, weka kumbukumbu kwa kumnunulia zawadi ndogo au kubwa ambayo itamfanya kila anapoiangalia akukumbuke. Isiwe zawadi ambayo inaweza kumletea matatizo kwenye uhusiano wake. Kwa mfano, kama ni mwanafunzi unaweza kumnunulia kalamu au leso, vitu ambavyo hata mpenzi wake hawezi kumshitukia. Kama ni mtu mnayefanya kazi au mnasoma pamoja, siku mojamoja mkikutana hotelini, mlipie bili ya chakula au kinywaji.
Fanya hivyo bila mtu mwingine kujua. Unajua kwa nini hii inatajwa kuwa moja ya njia inayoweza kukufanya ukawa na amani? Ni kwa sababu endapo ataipokea zawadi ama ofa yako, utabaki na furaha hata kama hajakukubalia wewe uwe mpenzi wake.
Kumbuka unafanya hayo yote si kwa ajili ya kumtega wala kumshawishi achepuke au amuache mpenzi aliyenaye awe na wewe, unafanya hayo kuonesha upendo wako kwake lakini pia kutafuta amani ya moyo. Tahadhari kubwa unayotakiwa kuichukua ni kuhakikisha humshawishi kufanya naye mapenzi wala kumuonesha upendo wako katika mazingira ambayo yeye asingependa. Kwa mfano, yawezekana kutokana na unavyomzimikia ukajikuta unatamani kumpigia simu na kuongea naye au kumtumia hata sms nzuri.
Usithubutu kabisa kufanya hivyo kwani unaweza kumfanya akuogope na asikuchangamkie akihisi utamharibua uhisiano wake. Pia epuka kuonesha upendo wako kwake akiwa na marafiki zake. Ukifanya hivyo inawezekana mmoja wa marafiki zake anajuana na mpenzi wa huyo unayempenda kisha akazifikisha taarifa ikawa tatizo. Mawasiliano yako na yeye ikiwezekana iwe mnapoonana tu akiwa hayuko na mpenzi wake.
Hii ni kwa sababu unaweza kumtumia sms kumbe simu anayo mpenzi wake au ukampigia simu akapokea mpenzi wake na kusababisha matatizo kwa mwenzako. Mwisho naomba niseme kwamba, unapotokea kumpenda mtu ambaye yuko kwenye uhusiano, hata kama na yeye anakupenda, chukulia kwamba huwezi kumpata tena.
Tafuta mwingine ambaye utamuonesha mapenzi yako na hakikisha unapambana na hisia zako za kumpenda mpenzi wa mwenzako kwani ukiziendekeza, zitakutesa sana. Nihitimishe kwa kukuambia wewe msomaji wangu kwamba, kumpenda mtu mwingine licha ya kwamba uko kwenye uhusiano wala si dhambi, ni hali ya kawaida ya kibinadamu inayowakumba wengi.
Kikubwa ni kuwa makini katika kila unachokifanya ili uendelee kuishi maisha ya furaha na amani lakini pia huwezi jua, yawezekana siku moja Mungu akatimiza aliyopanga na huyo unayempenda akaingia mikononi mwako. Kumbuka subira inahitajika katika kila jambo!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate