EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, October 25, 2014

MAZISHI YA MEJA JENERALI HERMAN LUPOGO

 Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na mkewe wakiwasili katika viwanja vya makaburi ya Kinondoni wakati wa mazishi ya Meja Jenerali mstaafu, Herman Lupogo. Meja Lupogo alifariki Oktoba 19 katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo  jijini Dar es Salaam. (Picha na Francis Dande)
Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa  akisalimiana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi.
 Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na akizungumza na Waziri wa Ulinzi wa zamani, Prof. Philemon Sarungi.
 Askari akiwa amebeba shada la maua.
 Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akiwasili.
 Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa akisalimiana na Mkuu wa Majeshi.
 Mkuu wa Majeshi mstaafu, Robert Mboma (kushoto) akibadilishana mawazo na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akiweka shada la maua.
 Mwili wa marehemu Meja Jenerali, Herman Lupogo ukiwasili makaburini.
 Gwaride likiwa mguu sawa.
 Maofisa wa JWTZ wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa Meja Jenerali Herman Lupogo.
 Maofisa wa JWTZ wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa Meja Jenerali Herman Lupogo. 
 Brass Band ikiongoza.
 Maofisa wa JWTZ wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa Meja Jenerali Herman Lupogo.
 Maofisa wa JWTZ wakiweka jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu Meja Jenerali Herman Lupogo kaburini.
 Mwili ukiwekwa kaburini.
 Mke wa marehemu Meja Jenerali Herma lupogo akiweka udongo katika kaburi.
 Ndugu na jamaa wwakiweka udongo.
 Rais mstaafu, Benjamin Mkapa akiweka udongo.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi akiweka udongo.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wa zamani, Edgar Maokola Majogo akiweka udongo.
Kazi ya kuweka zege katika kaburi ikiendelea.
 Mke wa marehemu akiweka shada la maua.
 Familia ikiweka shada la maua.
 Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na mkewe wakiweka shada la maua katika kaburi la Meja Jenerali mstaafu, Herman Lupogo wakati wa mazishi yake katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Meja Lupogo alifariki Oktoba 19 katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo. 
 Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akiweka shada la maua.
 Mashada ya maua yakiwekwa.
 Heshima kwa marehemu Meja Jenerali Herman Lupogo.
  Heshima kwa marehemu Meja Jenerali Herman Lupogo.
 Mwakilishi wa Jeshi,  Meja Jenerali Gaudence Milanzi akisoma wasifu wa marehemu.
 Kaburi la Meja Jenerali Herman Lupogo.
Rais mstaafu Benjamin mkapa akiagana na mke wa marehemu.

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa awamu ya tatu wa Tanzania, Benjamin  Mkapa amewaongoza maelfu ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Meja Jenerali Herman Corneli Lupogo kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Viongozi wengine walioudhulia mazishi hayo ni, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange, Jenerali Mstaafu Robert Mboma pamoja na Mawaziri waliowai kuongoza Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga, Prof, Philemoni Sarungi na Edgar Maokola Majogo.

Akisoma risala mara baada ya mazishi, Mwakilishi wa Jeshi,  Meja Jenerali Gaudence Milanzi alisema, marehemu alifariki dunia mnamo Oktoba 19, mwaka huu kwa ugonjwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo alikokuwa akipata matibabu.

Alisema, marehemu alimaliza elimu ya Kidato cha sita katika shule ya Sekondari Pugu mwaka 1956, baadae akapata Stashahada ya Ualimu na Shahada ya kwanza ya Sanaa katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda.

“Marehemu alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania mnamo Julai 23, 1965 na kutunukiwa Kamisheni Januari 21, 1966 na baadae kwa nyakati tofauti alipandishwa vyeo hadi kufikia Cheo cha Meja Jenerali mnamo Februari 9, 1983 ambacho alistaafu nacho Jeshini,”alisema.

Aliongeza kuwa, baada ya marehemu kustaafu aliendelea na shughuli mbalimbali za kujenga taifa ikiwamo, kuwa Mkuu wa Mkoa Iringa mwaka 1990, Mwenyekiti Chuo cha Diplomasia 1987 hadi 1991, Mkurugenzi Mtendaji wa AICC 1993.

“Pia alikuwa Mwenyekiti wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania(TACAIDS), 2001 hadi 2014, marehemu mara kwa mara alienda kushiriki kutoa mihadhara kama mwalimu wa kualikwa katika Vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya Jeshi ikiwamo Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC),”alisema.

Aidha, alimalizia kwa kutoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma wa JWTZ kutokana na msiba mzito uliotokea na kwamba sio pigo kwa familia yake, bali kwa ndugu, jamaa, majirani, jeshi na Taifa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate