EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, October 25, 2014

HAKUNA UBISHI SITTI MTEMVU KADANGANYA UMRI

Stori: Mwandishi Wetu
LILE sakata la Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zubeir Mtemvu kudaiwa kudanganya limeingia ukurasa mwingine kufuatia ufukunyuku wa gazeti hili kubaini kuwa, miaka 25 ndiyo sahihi kwake.
Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Zubeir Mtemvu.
Kufuatia ushindi alioupata siku ya shindano la kumsaka Miss Tanzania 2014 lililofanyika Oktoba 11, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, kuliibuka madai kwamba mrembo huyo alidanganya umri.

MADAI YA JUKWAANI
Awali, akiwa jukwaani kujitambulisha na kujibu maswali, mlimbwende huyo alishika kipaza sauti na kusema:
“My name is Sitti Mtemvu,  ‘am  eighteen years old (jina langu ni Sitti Mtemvu, nina miaka kumi na nane).
Hapo ndipo palipoanzia utata, wanaomjua Sitti walianika umri wake kwamba, ana miaka 25 huku wakianika tarehe ya kuzaliwa kwake kwamba ni Mei 31, 1989. Miandao ikaanza kumponda kwamba alidanganya umri hivyo halimfai tena!
LUNDENGA ATOA TAMKO, ATETEA
Kufuatia hali ya hewa kuchafuka kwenye mitandao, redio na magazeti akishutumiwa Sitti, Oktoba 21, mwaka huu, mratibu wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga aliitisha mkutano na vyombo vya habari.
Cheti cha kuzaliwa cha Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu.
Katika mkutano huo ambao Sitti naye alishiriki sanjari na mama yake mzazi, Lundenga alisema vyeti vya kuzaliwa alivyowasilisha mshiriki huyo kama washiriki wengine, vilionesha ana miaka 23, alizaliwa 1991, Temeke jijini Dar.

UTATA WAIBUKA

Utata ulianza kuibukia hapo kwenye maneno ya kutoka kwenye kinywa cha Lundenga kwani alisema cheti hicho kilitolewa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) Septemba, mwaka huu ikiwa ni siku 32 tu kabla ya shindano la Mlimani City.

MASWALI

Waandishi walitaka kujua hivi; kama cheti hicho kilitolewa Septemba 9, mwaka huu na Sitti amesoma Marekani ambako mtu huwezi kwenda mpaka uwe na paspoti na ili upate paspoti lazima uwe na cheti cha kuzaliwa je, yeye alitumia cheti gani? Maana alikwenda Marekani kati ya mwaka 2010 na 2011.
Leseni ya udereva ya miss Tanzania Siti Mtemvu.
Sitti alilijibu swali hilo kuwa, cheti hicho kilipotea lakini akashindwa kukitaja kituo chochote cha polisi alichopeleka madai ya kupotelewa kwa cheti na kuishia kusema
vyombo vya habari vinamfuatafuata sana.
UFUKUNYUKU WAANZA
Kufuatia mlolongo huo wote, ndipo timu ya uchunguzi ya Magazeti Pendwa ya Global Publishers ikaingia mtaani na kuanza kuchimba ukweli wa umri wa binti huyo.
Katika chanzo cha uhakika kutoka katika idara husika ya kutoa paspoti, faili la Sitti lilisomeka hivi: (tunaandika kwa Kiswahili tu).
Jina la ukoo: Mtemvu.
Jina:
Sitti Abbas.
Utaifa
: Mtanzania.
Tarehe ya kuzaliwa:
May 31 1989.
Tarehe ya kutolewa:
17 Feb 2007.
Tarehe ya Mwisho wa matumizi:
14 Feb 2017.
Pasipoti ya miss Tanzania Siti Mtemvu.
SHULE ALIYOSOMA UGANDA
Ufukunyuku wa gazeti hili ulikwenda mbele zaidi hadi kwenye Shule ya Sekondari ya Hana Mixed iliyopo Mji wa Nsangi, Kampala, Uganda ambako Sitti alisoma kidato cha tano na sita.
Akizungumza na gazeti hili kwa sharti la jina lake kutoandikwa gazetini, mwanafunzi mmoja alisema kuwa, mwaka 2006 Sitti aliingia shuleni hapo kidato cha tano akiwa na miaka 17. (Piga hesabu mpaka mwaka huu).
BETHIDEI YAKE 2007
Mwanafunzi huyo akazidi kudai kuwa, Mei 31, 2007, Sitti akiwa kidato cha sita, alifanya sherehe fupi ya kuadhimisha kuzaliwa kwake ‘bethidei’ ambapo alisema anatimiza mwaka wa 18.
Sitti Abbas Zubeir Mtemvu.
Katika kasherehe hako ambako hakakuwa rasmi, waliohudhuria ni kijana mmoja na wanafunzi waliokuwa wakilala chumba kimoja na Sitti. Sitti alimaliza kidato cha sita Novemba 2007.
MNYAMBULISHO WAKE
Kwa hesabu za haraka, Sitti alianza darasa la kwanza akiwa na miaka 6 (1995). Darasa la 7 akamaliza akiwa na miaka 12 (2001). Alianza kidato cha kwanza akiwa na miaka 13 (2002), akamaliza kidato cha 4 akiwa na miaka 16 (2005). Akiwa na miaka 17 alianza kidato cha 5 (2006), akamaliza cha 6 akiwa na miaka 18 (2007).
Kwa mahesabu hayo, mlimbwende huyo alizaliwa mwaka 1989 sawa na hati yake ya kusafiria na leseni ya udereva ambavyo vyote vinaonesha kuwa alizaliwa mwaka huo. Hii ni aibu kwa Lundenga!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate