EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 31, 2013

World's Top 10 Richest Football Clubs.

10. Liverpool - Value: $651 million

9. Manchester City - Value: $689 million

8. Juventus - Value: $694 million

7. Chelsea - Value: $901 million

6. AC Milan - Value: $945 million

5. Bayern Munich - Value: $1.32 billion

4. Arsenal - Value: $1.33 billion

3. Barcelona - Value: $2.6 billion

2. Manchester United - Value: $3.16 billion

1. Real Madrid - Value: $3.3 billion

HATIMAYE SERIKALI YAIFUNGA SHULE YA SEKONDARI YA LUTHERAN JOURNIOR YA MJINI MOROGORO BAADA YA WANAFUNZI KUGOMA KWA SIKU TATU.

Mgomo wa wanafunzi zaidi ya 600 wa shule ya sekondari ya seminari ya lutheran journior ya mjini Morogoro wa kutoingia darasani mpaka madai ya kero zao yatatuliwe umeingia hatua mpya baada ya serikali kuchukua hatua ya kuwafukuza wanafunzi wote shuleni hapo na kufunga shule hiyo kwa muda usiofahamika .

Hatua hiyo ya serikali imekuja kufuatia wanafunzi hao kukataa kuzungumza na kumzomea katibu mkuu wa kanisa la kinjiri la kirutheri KKKT Brighton Killewa ambaye alitumwa na askofu wa kanisa hilo nchini Alex Malasusa kusikiliza madai ya wanafunzi hao ambayo ni pamoja na kutaka mkuu wa shule hiyo aondolewa shuleni hao kutokana na kuendesha shule huyo kidikteta pamoja na walimu wanaoajiriwa hapo kutokuwa na sifa hali inayofanya shule kushuka kitaaluma .
 
Kasilda Mgeni Mulimila kutoka Morogoro anataarifa zaidi.......

Huyu ni katibu mkuu KKKT akiwa hana la kufanya baada ya wanafunzi hawa kumzumea hata kabla ya kuanza kusikiliza kero zao, hali hii inalilazimu jeshi la polisi kutuma askari wake kulinda usalama shuleni hapo kwa siku ya tatu leo huku uongozi wa shule hiyo ukiendelea kuwasiliana na serikali juu ya yale yanayoendelea shuleni hapo ,na hatimaye afisa elimu wa mkoa wariambora Nkya anakuja shuleni hapo na kisha kutoa uamuzi wa bodi ya shule na serikali.

WARAKA MZITO WA PAPII KOCHA KWA JK

ULE waraka wa mwanamuziki aliyefungwa gerezani kifungo cha maisha sambamba na baba yake mzazi, Nguza Viking ‘Babu Seya’, Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ umeibua mjadala tena huku Naibu Waziri wa Mali Asili na Utalii, Lazaro Nyalandu akiombwa na kukubali kuufikisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.
Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ (kushoto) akiwa na baba yake Nguza Viking ‘Babu Seya’.
MIAKA 10 GEREZANI
Hivi karibuni wasanii hao walitimiza miaka kumi tangu walipofungwa katika Gereza la Ukonga, Dar mwaka 2003 hivyo kusababisha waraka huo aliouandika Papii Kocha Februari mwaka 2010 kusababisha mjadala upya.
Kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, Julai 21, mwaka huu waraka huo ulikuwa gumzo kubwa juu ya ombi la Papii Kocha kwa Rais Kikwete kuwa amhurumie atoke gerezani kwa kuwa bado ni kijana mdogo huku nyuma yake watu wakituhumiana bila ushahidi.

Tottenham chief Daniel Levy the target of anti-semitic abuse over Gareth Bale transfer.

Internet trolls have labelled Tottenham chairman Daniel Levy a "greedy Jewish b*****d" in a glut of anti-semitic comments about the Spurs chief.
 Abuse: Daniel Levy's tough negotiation tactics have provoked disgusting insults from internet trolls
The Twitter abuse was in reference to Levy's handling of Real Madrid's interest in Gareth Bale, with Tottenham holding out for a world record transfer fee for the Welsh winger.

In the last season alone, Chelsea have launched probes into anti-semitism abuse from fans and West Ham supporters were warned for offensive chants towards the Spurs support.  
SOURCE: Daily morror     

NI MSIMU WA SIKUKUU NDANI YA DAR LIVE

SERIKALI YATILIANA SAINI NA UINGEREZA UTEKELEZAJI MRADI WA INTERNATIONAL INSPIRATION‏.

 
Balozi wa Uingereza hapa nchini Bibi Dianna Melrose akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kutiliana saini mkataba wa makubaliano kuhusu mradi wa International Inspiration awamu ya pili, baina ya Tanzania na Uingereza. Mradi huu umekuwa ukitekelezwa kwa muda wa miaka miwili sasa hapa nchini na unahusisha michezo mashuleni ambapo jumla ya shule 15 zinanufaika na mradi huo.
Balozi wa Uingereza hapa nchini Bibi Dianna Melrose akifafanua jambo kwa  waandishi wa habari wakati wa hafla ya kutiliana saini mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa shughuli za mradi wa International Inspiration awamu ya pili leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Sihaba Nkinga.Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetiliana saini ya makubaliano na Serikali ya Uingereza katika utekelezaji wa mradi huo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Sihaba Nkinga na Balozi wa Uingereza hapa nchini Bibi Dianna Melrose kushoto wakiweka saini kwenye mkataba wa makubaliano ya utekelezaji wa shughuli za mradi wa International Inspiration leo jijini Dar es Salaam.

Rasimu ya Katiba mpya haimtaji mkulima.

Kadri mjadala wa Rasimu ya Katiba unavyozidi kupamba moto, wanasiasa wanazidi kubaini ufinyu wa nafasi zao iwapo rasimu hiyo itapita bila mabadiliko, hivyo kulazimika kuibua vihoja na mambo ambayo hawataki yawemo wakidhani kuwa yanaweza kuwaathiri.

Mada kuu katika rasimu iliyotolewa na Tume ya Jaji Joseph Warioba inayoleta hofu kwa wengi ni muundo wa Muungano wa Serikali tatu. Muundo huu ndiyo unaotoa taswira ya hali ya kisiasa hapa nchini hapo baadaye, iwapo Katiba Mpya itapitishwa.

Miongoni mwa wanasiasa waliotikisika ni wanasiasa kutoka Zanzibar, hasa kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), na hata wenzao wa bara ambao wameonyesha kila dalili za woga wa kupoteza madaraka.

Chama hicho kimeamua kutoa waraka wa ‘kuichana’ Rasimu ya Katiba, kikipinga Serikali tatu na mambo mengine mengi yanayopendekezwa.
Wanasiasa wenye mwelekeo huo wamejificha katika kivuli cha ‘gharama kubwa za uendeshaji wa Serikali tatu’.

Kwa mfano, Samuel Sitta, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki anasema haijawahi kuwapo nchi yoyote duniani yenye marais watatu kama inayopendekezwa, kana kwamba ilishawahi kuwapo nchi yenye marais wawili kama iliyopo sasa, Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar katika nchi moja.

SAKATA LA YANGA KUPINGA MECHI ZAO KUONYESHWA AZAM TV - WANACHAMA WA KLABU HIYO WAUNGA MKONO UONGOZI.

Uongozi wa matawi wa klabu ya Yanga (wenyeviti na makatibu) leo umefanya kikao katika makao makuu ya klabu mtaa wa twiga/jangwani kisha kutoa tamko lao kwa waandishi wa habari kuhusiana na tamko la uongozi (kamati ya utendaji) kutokubali kuonyeshwa kwa michezo yake kwenye luninga.
 
Awali klabu ya Yanga juzi kupitia kamati ya utendaji ilifanya mkutano na waandishi wa habari juu ya mustakabali wa klabu kuhusiana na kutoridhishwa na kamati ya muda ya Ligi (TPL) kuingia makubaliano ya kurushwa matangazo ya televsheni kwenye michezo yake.
 
Akiongea na waandishi wa habari leo katibu mkuu wa Yanga Lawrence Mwalusako alisema baada ya kukaa na viongozi wa matawi ya klabu ya Yanga jijni Dar es salaam kwa pamoja wamekubali na kuunga mkono hoja zilizowasilisha na viongozi juu ya haki ya matangazo.
 
Mmoja wa viongozi wa matawi Bakili Makele akiongea kwa niaba ya viongozi wa matawi, alisema TFF inaamua kukandamiza soka la Tanzania kwa kuviamulia maamuzi yake juu ya kuonyeshwa kwa michezo ya timu kwenye luninga.

CHOMBEZO: KITANDA CHA MAMA MWENYE NYUMBA....SEHEMU YA.... 01

Mtunzi_Na: IRENE MWAMFUPE NDAUKA
 “Mke wangu, kila
siku namwona huyu kijana mchafuchafu anakuja kuokota chupa tupu hapa, ina maana
tuna chupa tupu kila siku?”
“Siyo hivyo mume
wangu, we hujamfuatilia tu, anakuja kila baada ya siku tano. Tumsaidie mume wangu,
si unamwona kijana mwenyewe masikini huyu,” alisema mama Joy huku macho yake
yote yakimwangalia yule kijana mwokota makopo…
 
“Awe anakuja
mchana basi, usiku kama huu hapa nje, mimi naweza kumchapa risasi nikidhani
mwizi. Si unaona hata mavazi yake? Kwanza haogi huyu, hata harufu anatoa…”
 
“Mume wangu
usimkufuru Mungu, sisi kupewa uwezo ni matakwa yake, hakuna binadamu ambaye
akipewa nafasi ya kuchagua maisha bora na duni, atasema anataka duni.”
“Mimi sijafika
huko, ila nasema awe anakuja mchana tu  si usiku kama huu.”
 
“Sawa mume wangu,”
alisema mama. Hayo yalitendeka  wakati
baba Joy akiegesha gari mahali pake kisha akashuka na kuanza kutembea mkononi
ameshika brifkesi yake. Siku hiyo, baba Junior alikuwa kama amevaa Kinaijeria
f’lani.
 
Mama Joy alimpokesa
mumewe brifkesi kisha akamwacha apite ili yeye amfuate kwa nyuma. Wakati mumewe
anaingia, mama Joy aligeuka kumwangalia mwokota chupa tupu ambaye kwa muda huo
alikuwa amebeba fukp la ‘salfeti’ begani.
 
Mama Joy alimwonesgha ishara kwamba aondoke haraka sana kwa vile mumewe amerudi. Kijana
wa watu, alitoka getini kwa kuruhusiwa na mlinzi.

Selly afurahia Nando kutimulia BBA.

Aliyekuwa mshiriki kutoka Ghana Selly ambaye alitoka wiki kadhaa zilizopita Selly, ameonyesha jinsi gani alivyoshukuru na kufurahi baada ya kuona Nando kawa disqualified katika jumba la BBA. Muda mfupi baada ya Nando kupewa amri ya kuondoka katika jumba hilo kwa kuvunja masharti,kupitia twitter account yake Selly aliandika..

Selly na Nando wameshawahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi katika jumba la BBA kabla ya Nando kumbwaga mawanadada huyo.Pia iliwahi kuripotiwa kuwa Selly kamuambukiza Nando gonjwa la zinaa.Inaelekea Selly ana hasira na Nando japo alishawahi kukiri kuwa anamzimia sana.
Selly

MATOKEO YA UALIMU 2013


NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

MATOKEO YA UALIMU 2013






CHANZO NI HAPA NECTA

IRENE UWOYA ANAKUJA NA SHOW YAKE YA KUTENGENEZA NA KUKARABATI NYUMBA ITAKAYO RUSHWA CLOUDS TV.

Irene Uwoya anakuja na kipindi chake kipya cha Tv kwa ajili ya kutengeneza na kukarabati nyumba mbalimbali za watu atakazotembelea. Kipindi hicho kitarushwa kupitia Clouds Tv na tayari actress huyo ameanza kushoot kipindi hicho kama anavyoonekana pichani hapo juu. 
Irene Uwoya ni muigizaji mwingine aliyeamua kugeukia vipindi vya Tv pia ukiachilia mbali kuigiza filamu wengine ni Rose Ndauka na Wema Sepetu ambaye show yake kuhusu maisha yake halisi pia kitarushwa Clouds Tv kuanzia mwishoni mwa mwezi wa nane mwaka huu.

KODI YA SIMU KURUDI BUNGENI AGOSTI,NI BAADA YA KUTOKEA UTATA KUHUSU KODI HIYO.

http://www.habarileo.co.tz/images/resized/images/mgimwazz_255_300.jpg

SAKATA la kodi ya simu ya Sh 1,000 kwa kila laini ya simu kwa mwezi, inayolipwa na watumiaji wa simu, litamalizwa bungeni kisheria. Waziri wa Fedha, William Mgimwa, amesema wameanza kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete, la kuitaka Wizara ya Fedha kukutana na wadau wengine, kuangalia namna ya kupata vyanzo vingine vya mapato mbadala wa kodi hiyo.
Alisema hayo alipozungumza jana na gazeti hili, baada ya kusaini mkataba wa msaada wa zaidi ya Sh bilioni 344, kutoka Benki ya Dunia, ili isaidie masuala mbalimbali katika sekta ya usafirishaji. Mgimwa alisema katika suala hilo, masuala ya kisheria yatafikishwa bungeni mwezi ujao, ili kumaliza utata wa kodi hiyo.
 
Alisema uamuzi wa kushughulikia suala hilo, ulifikiwa kutokana na agizo la Rais Kikwete la hivi karibuni, kutaka wizara hiyo na ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kukaa na kampuni za simu kumaliza utata uliojitokeza kuhusu kodi hiyo.
Awali Umoja wa Wamiliki wa Kampuni za Simu (MOAT), ulitoa maoni kutaka kufutwa kwa kodi hiyo, kutokana na kulalamikiwa na wadau wa sekta ya mawasiliano.

MFANYAKAZI WA KAMPUNI YA MWANANCHI APIGWA RISASI.

 Jessica Ngassa akimuhudumia mumewe, Jackson Ngassa ambaye ni mfanyakazi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Idara ya Usambazaji wa Magazeti aliyejeruhiwa kwa kupigwa risasi na majambazi  Jumamosi usiku jijini Dar es Salaam.

Watu ambao wanasadikiwa kuwa ni majambazi wamemjeruhi kwa risasi mfanyakazi wa Idara ya Usambazaji ya Mwananchi Communications Limited,  Jackson Ngassa.
Tukio hilo lilitokea juzi Jumamosi saa 4 usiku eneo la Tabata Matumbi baada ya watu hao kumfuatilia Ngassa tangu alipokuwa anatoka ofisi za Mwananchi eneo la Tabata Relini.
 
Akizungumza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (Moi), Ngassa alisema wakati akitoka ofisini siku hiyo aliona pikipiki tatu zikiwa nyuma yake lakini hakuhisi kama zilikuwa zinamfuata mpaka walipofika taa  za kuongozea magari za Tabata Dampo.
 
“Nilipofika Tabata Dampo nilihisi kufuatiliwa kwa sababu kila nilipopunguza mwendo nao walipunguza mpaka nilipofika Matumbi ndipo nikasikia wakiniambia simama haraka na kisha wakapiga risasi moja ambayo ilitoboa tanki la mafuta la pikikipiki,” alisema Ngassa.

TAARIFA KWA WAOMBAJI WA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inawatangazia waombaji wote wa mikopo wanaotarajia kujiunga na Vyuo vya Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2013/2014 na wale wanaoendelea na masomo kuwa mwisho wa kupokea maombi ya mikopo ni tarehe 31 Julai, 2013 na kwamba hakutakuwa na muda wa nyongeza baada ya tarehe hiyo kupita.

Bodi inawasisitizia waombaji wapya na wanafunzi wanaoendelea na masomo ambao hawajaomba mikopo kwa njia ya mtandao, kuhakikisha wanatumia muda uliobaki kukamilisha taratibu zote za maombi kupitia anuani ifuatayo: www.olas.heslb.go.tz au kupitia tovuti:www.heslb.go.tz kabla ya tarehe 31 Julai, 2013.

Kila mwombaji anakumbushwa kusoma kwa umakini mwongozo wa ujazaji wa fomu ya maombi ya mikopo kwa mwaka 2013/2014 na kulipia ada ya shilingi 30,000/= kwa waombaji wapya kwa njia ya M-Pesa.

Tangazo hili limetolewa na:
Mkurugenzi Mtendaji
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

Download wimbo mpya wa Snura - NIMEVURUGWA

Tuesday, July 30, 2013

AHUKUMIWA MIAKA 30 KWA KUMBAKA NA KUMZALISHA MWANAYE.

Yusufu Amani (39) aliyembaka mwanaye wa kumzaa kisha kumzalisha baada ya kutengana na mkewe akiwa kizimbani. Yusufu akificha sura yake asipigwe picha baada ya hukumu ya miaka 30.

WANAWAKE KUMI BONGO WENYE VYEO VIKUBWA.

WANAWAKE wengi nchini wameshika vyeo mbalimbali vya juu serikali au kwenye taasisi binafsi. Wafuatao ni wanawake 10 ambao wanakalia au wamekalia vyeo hivyo hapa nchini kama walivyomulikwa na Elvan Stambuli.

JULIET  KARIUKI
HUYU ni Mkuruggenzi Mtendaji wa kwanza mwanamke katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) . Uteuzi wake ulifanywa na Rais Jakaya Kikwete Aprili 12 mwaka huu na akakabidhiwa ofisi siku hiyohiyo.
Bibi Kariuki ana shahada ya kwanza ya sheria na ya uzamili, kwenye sheria ni mtalamu wa ubia kati ya serikali na watu binafsi (Public Private Partnership). Aliwahi kufanya kazi katika Chama Cha Mabenki ya Afrika Kusini.


MIZINGA MELU
NI  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC tangu  Machi 20 mwaka huu. Alichukua nafasi hiyo kutoka kwa  Lawrance Mafuru. Ni mzaliwa wa  Zambia katika Kijiji cha Mazabuka na ana shahada ya juu ya biashara (MBA), Zambia National Commercial Bank na Standard Chartered Bank.


SAUDA S. RAJABU
NAYE ni mwanamke wa kwanza kushika wadhifa wa juu wa Mkurugenzi Mkuu na Mtendaji Mkuu (CEO) wa Kampuni ya Ndege ya Precision Air hapa nchini. Alianza kutumikia nafasi hiyo Machi Mosi, mwaka huu baada ya aliyekuwa akikalia kiti hicho, Alfonce Kioko kumaliza muda wake.
 

Ana shahada ya kwanza ya biashara na sasa yupo mbioni ‘kuchimbua’ shahada ya juu ya biashara. Amewahi kufanya kazi katika mashirika mengine ya ndege kama vile Kenya Airways na ya Rwanda na Burundi.

ANNE MAKINDA
NI mwanamke wa kwanza nchini kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Samwel Sitta ambaye aliliendesha Bunge kwa msimu mmoja tu mwaka 2005 hadi 2010.
Makinda amevunja rekodi kwa kukaa bungeni kwa miaka mingi kwani alianza kuwa Mbunge wa Jimbo la Njombe mwaka 1975 hadi leo. Tayari ametangaza kung’atuka (2015).

BILIONEA ALIYEMWAGIWA TINDIKALI DAR… HALI TETE.

HALI ni tete kuhusiana na tukio la bilionea Said Mohamed Saad kumwagiwa tindikali, athari ni kubwa. Jinsi alivyoharibika inatia simanzi lakini kumpata mhusika wa unyama huo ni kitendawili kinacholitega Jeshi la Polisi Tanzania.
Rais Kikwete akimjulia hali mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, Said Mohamed Saad.
Said ambaye ndiye mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, yenye maduka mengi makubwa ya vitu vya nyumbani ndani ya Dar es Salaam na mikoa kadhaa ya Tanzania, anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini lakini mmoja wa watu waliomshuhudia, amefafanua jinsi hali ilivyo mbaya.
 
“Ameungua sana, tunatarajia kati ya kesho au keshokutwa (wikiendi iliyopita) atafanyiwa oparesheni ya jicho. Jamani tindikali ni mbaya sana, usimmwagie mwenzako. Ndugu yetu ameharibika sana,” kilisema chanzo chetu kwa ombi la kutotajwa jina gazetini, kikaongeza:
“Kila anayemjua vizuri, anapomwona anamwaga machozi. Picha za jinsi alivyoathirika baada ya kumwagiwa tindikali zimevuja mpaka kwa familia, ni kilio kwa ndugu. Wanawake wanalia zaidi.”

JK ATINGA HOSPITALI
Wiki iliyopita, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, alikuwa kwenye ziara ya kikazi nchini Afrika Kusini alipokwenda kuhudhuria Mkutano wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini ya Afrika (SADC).
Mkutano huo ni wa Pande Tatu za SADC (Troika of SADC) na akiwa huko, alipata fursa ya kwenda kumjulia hali katika hospitali aliyolazwa ambayo haijajulikana jina.
Chazo chetu kilisema: “Rais Kikwete alisikitika sana. Wakati anatoka wodini alisonya. Alionesha jinsi alivyosikitishwa na unyama aliotendewa Said.”

Mwanasheria Mkuu amgeuka Pinda.

*Awataka polisi wasitumie nguvu kubwa kudhibiti raia
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, amelitaka Jeshi la Polisi nchini, kuacha kutumia nguvu zilizopita kiasi, pindi linapokuwa likituliza ghasia.

Amesema, pamoja na kwamba jeshi hilo linaruhusiwa kisheria kutumia nguvu wakati wa kutuliza ghasia, nguvu hizo hazitakiwi kuzidi kipimo kwa kuwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria.

Jaji Werema alitoa kauli hiyo mjini hapa jana, alipokuwa akifungua mkutano wa mawakili wafawidhi wa Serikali, wakuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wa mikoa na vikosi vingine vya polisi.

“Sheria inaruhusu polisi kutumia nguvu katika baadhi ya maeneo, lakini utaratibu lazima ufuatwe.

Banner 
“Tusitumie nguvu kubwa kupita kiasi, polisi mmejifunza kutumia mabomu, bunduki na mmejifunza pia kutumia bunduki na kulenga shabaha, usimpige mtu kichwani, hilo ni kosa, lenga kwenye mguu,” alisema Jaji Werema.

Kauli hiyo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, inaonekana kwenda kinyume na kauli iliyotolewa hivi karibuni na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda dhidi ya wanaokaidi maagizo ya polisi.

Polisi wahaha tukio la Home Shopping Center.

WAKATI hali ya mmiliki wa maduka ya Home Shopping Centre, aliyemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana, Said Mohammed Saad, ikiendelea kuimarika kutokana na matibabu anayopata, hakuna mtuhumiwa aliyekamatwa kutokana na tukio hilo.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema polisi wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo.

“Jamani mambo mengine ni ya ndani ya polisi na si vema tukayatoa hadharani, tulieni jamani, upelelezi ukikamilika tutawaita na kutoa taarifa,” alisema Kamanda Wambura.

Saad alimwagiwa tindikali hivi karibuni maeneo ya Msasani City Mall, jijini Dar es Salaam na mtu asiyejulikana.

Baada ya tukio hilo, mtu huyo ambaye hadi sasa hajakamatwa, alikimbia na kutokomea kusikojulikana.

Taarifa za kipolisi zilieleza kwamba, Saad alimwagiwa tindikali akiwa anazungumza na mfanyakazi wa duka lake lililopo kwenye Jengo la Msasani City Mall.

Tukio la kumwagiwa tindikali mfanyabiashara huyo, limekuja ikiwa ni wiki mbili tangu Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha, Said Juma Makamba, ajeruhiwe vibaya usoni kwa kumwagiwa majimaji yanayosadikiwa kuwa ni tindikali.

Wanaokwamisha ujenzi wa barabara kukiona.

SERIKALI imeonya kuwa haitaruhusu watu wachache wakwamishe juhudi za Serikali za kuunganisha nchi na mtandao wa barabara za lami.
Rais Jakaya Kikwete, alisema hayo jana katika eneo la Omugakorongo Kata ya Ndama, wilayani Karagwe, wakati akiweka jiwe la msingi katika barabara ya Kyaka –Bugene yenye urefu wa kilometa 59.1, inayojengwa kwa kiwango cha lami.
Rais Jakaya Kikwete akisimikwa kuwa Chifu wa Wahaya na kukabidhiwa mgolole na silaha za jadi za Wahaya katika sherehe ya kuzindua Wilaya mpya ya Kyerwa mkoani Kagera mwishoni mwa wiki. (Picha na Ikulu).
Alitoa kauli hiyo baada ya Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, kumuomba amuunge mkono wakati wa kupambana na wananchi wanne, waliokataa kupokea fidia na kubomoa nyumba zao, ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo.
Dk Magufuli alisema watu hao, akiwemo mzee marufu wa Wilaya ya Karagwe, Nehemia Kazimoto, wanataka fidia zaidi, la sivyo nyumba zao hazibomolewi au watakwenda mahakamani.
Alisema wananchi 400 waliokumbwa na athari za kubomolewa nyumba kupisha ujenzi wa barabra hiyo, wamelipwa fidia Sh bilioni 2.8 kwa mujibu wa sheria, isipokuwa wananchi wanne tu akiwemo Kazimoto, ambao wamegoma kupokea fidia.

HIZI NDIO SABABU KWANINI YANGA INAPINGA MKATABA WA KAMATI YA LIGI/TFF NA AZAM MEDIA KUONYESHWA KWA LIGI KUU KWENYE TV



















Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji (katikati) akiongea na waanidishi wa habari, Makamu mwenyekiti Clement Sanga (kushoto) na mjumbe wa kamati ya utendaji Mark Anthony (kulia)






















Uongozi wa klabu ya Yanga siku ya jana umefanya mkutano na waandishi wa habari juu ya urushwaji wa michezo yake ya Ligi Kuu katika kituo cha luninga cha Azam ambacho kimeingia makubaliano na kamati ya Ligi Kuu  kuonyeshwa michezo yote ya ligi kwa kipindi cha miaka miatatu (3).
 
Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa klabu ya Yanga Yusuf Manji amesema uamuzi wa kamati ya ligi kuingia mkataba na kituo cha Azam Tv bila ya kuwashirikisha wahusika wenyewe ambao ni vilabu vishiriki haukuwa sawa.
Sisi kama klabu ya Yanga tulikaa kikao cha kamati ya utendaji na kuona taratibu za kupewa haki ya matangazo kwa kampuni ya Azam haikua sawa, sisi viongozi wa kalbu ya Yanga hatukushirikishwa katika mchakato huo hivyo tukaona ni vema tuje kwa vyombo vya habari tuulezee umma juu ya maazimio ya kamati ya utendaji.
Ifuatayo ni taarifa kamili kwa vyombo vya habari: 
YAH: URUSHWAJI KATIKA TELEVISHENI MICHEZO YA YANGA.

Hivi karibuni, Tanzania Football Federation (TFF)  iliunda Tanzania Premier League chini ya Bodi ya mpito Bodi ya TPL ambayo ni msimamizi mpaka hapo Bodi itakayokuwa imechaguliwa kidemokrasia. Bodi hii imeamua peke yake kuingia katika mkataba wa miaka 3 (mitatu) na kampuni inayoitwa Azam Television (ambayo ina  mapromota wale wale wanaomiliki Azam Football Club). Makubaliano ambayo Bodi ya TPL inatarajia kuingia na Azam Television, Kamati ya Utendaji ya YANGA inalipinga kwa nguvu zote katika misingi ifuatayo:

TAIFA STARS ILIVYOREJEA DAR ES SALAAM KWA UNYONGE - IKITOKEA KAMPALA KUPITIA KILIMANJARO

Monday, July 29, 2013

Watu 480 wauawa kwenye machafuko ya Misri

Harakati ya Ikhwaanul Muslimiin ya Misri imetangaza kuwa, kwa akali watu 480 wameuawa, 8,000 kujeruhiwa na wengine 1,500 kutiwa mbaroni kwenye ghasia na machafuko yaliyodumu kwa wiki tatu nchini humo. 

 Chama cha Uadilifu na Uhuru, tawi la kisiasa la Ikhwaanul Muslimiin, kimeeleza kuwa katika kipindi cha wiki tatu zilizopita, watu wasiopungua mia nne na themanini  wameuawa na wengine elfu nane kujeruhiwa pamoja na kufungwa kanali tisa za televisheni za harakati hiyo.

 Taarifa zinasema kuwa, machafuko na mapigano nchini humo yamesababishwa na hatua ya jeshi ya kumuondoa madarakani na kumuweka kizuizini Rais Mohammad Morsi wa nchi hiyo. 

Wafuasi wa Morsi wamekuwa wakijitokeza barabarani kila siku kumuunga mkono kiongozi huyo na hivyo kukabiliwa na hatua kali za jeshi.
Chanzo: kiswahili.irib.ir

Wafuasi wa Morsi waendelea kuandamana.

Wafuasi wa Rais aliyeondolewa madarakani nchini Misri Mohammed Morsi wamepanga maandamano zaidi kuelekea kambi za kijeshi. Pia wameitisha maandamano makubwa hapo kesho Jumanne.

Haya yanajiri huku, Mjumbe wa mambo ya nje wa Muungano wa Ulaya akiwa mjini Cairo kwa mazungumzo ya kumaliza taharuki zinazoendelea kufuatia mauaji ya zaidi ya waandamanji 70 wengi wakiwa wafuasi wa Muslim Brothehood .
Maelfu ya wafuasi wa Mohammed Morsi wameendelea kupiga kambi nje ya msikiti mashariki mwa Cairo kwa majuma kadhaa sasa na wanapanga kuendelea na maandamano yao usiku kucha.

Waandamanji hao wameitisha maandamano makubwa hapo kesho jumanne kuelekea katika kambi kuu ya jeshi.

Kampeini zaelekea kileleni Zimbabwe.

Rais mstaafu wa Nigeria Olesegun Obasanjo yuko nchini Zimbabwe kama mwangalizi wa uchaguzi mkuu

Kampeini za kisiasa nchini Zimbabwe zinamalizika hii leo kabla ya uchaguzi mkuu hapo Jumatano wiki hii.

Kiongozi wa chama cha Movement for Democratic Change ambaye pia ni Waziri MKuu ,Morgan Tsvangirai, hii leo atahutubia mkutano wa hadhara mjini Harare katika uwanja alikofanya mkutano wake hio jana Rais Robert Mugabe.
Viongozi hao wawili wamekua katika serikali ya muungano tangu mwaka wa 2008 na wametofautiana kuhusu muda uliowekwa kufanyika uchaguzi. Kumekua pia na madai ya wizi wa kura, na vitisho dhidi ya wafuasi wa MDC.

Shirika la kimataifa linalotathmini hali ya mizozo The International Crisis Group limeonya kwamba hakuna mazingira ya uchaguzi huru na haki Zimbabwe.

WASTARA ALIPIZA MSOTO WA MUMEWE

MSANII mwenye heshima tele kunako gemu la filamu Bongo, Wastara Juma amesema ameamua kulipiza muda aliosota kumuuguza mumewe, marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’  kwa kufanya kazi kwa bidii ili aweze kufikia levo waliyopo wasanii wenzake.
Wastara Juma.
Wastara ameiambia Stori 3 kuwa, anafanya kazi yake kwa bidii ambapo anatarajia kutoa muvi tatu kwa mpigo ndipo apumzike kulipiza muda ambao hakufanya kazi hiyo alipokuwa akimuuguza mumewe.
 
“Nimemaliza kushuti filamu yangu ya Shaymaa (Kialama) na sasa naendelea kucheza nyingine walau nilipize muda niliokaa bila kucheza filamu,” alisema Wastara.

MCHUNGAJI MBARONI KWA ULAWITI.


MCHUNGAJI wa kanisa moja la kilokole lililopo Kichangani, Majohe, Dar aliyetajwa kwa jina moja la Benard anadaiwa kutiwa mbaroni kwa tuhuma za ulawiti wa mtoto wa kiume (jina tunalo) mwenye umri wa miaka 15.
 
Hivi karibuni, gazeti hili lilipenyezewa kuwepo kwa sakata hilo ambapo lilitinga eneo la tukio na kuweka ‘patroo’ ili kunasa habari kamili.
 
Kwa mujibu wa mdogo wa mchungaji huyo aliyejitambulisha kwa jina la Hamis, kaka yake huyo alikamatwa wiki iliyopita baada ya watu waliojitambulisha kuwa ni askari kufika nyumbani na kumuweka chini ya ulinzi.
 
Alisema kuwa katika kuishi na kaka yake huyo, aliwahi kumuona huyo mtoto anayedaiwa kulawitiwa mara moja tu kwani yeye bado ni mgeni.
 
Kwa mujibu wa dogo aliyedaiwa kuingiliwa, alikutana na mchungaji huyo mwaka jana maeneo ya Stendi ya Banana-Ukonga, Dar ambapo alimuomba na kumwambia kuwa alikuwa anatafuta mtoto wa kumfanyia biashara ya mayai huko Majohe nyumbani kwake.
 
Alisema kuwa alikataa na kumwambia hawezi kwenda naye bali aende akazungumze na wazazi wake nyumbani.
 
Alisimulia kuwa baada ya hapo, aliongozana na baba mchungaji hadi kwa wazazi wake ambapo walikubaliana kuwa kila mwezi atamlipa mshahara wa shilingi 30,000.
Baada ya makubaliano hayo ‘dogo’ alisema kuwa aliondoka na mchungaji na baada ya kukaa kwa muda mfupi huku akiendelea na biashara ya mayai, mchunga kondoo huyo wa 
Mungu alianza tabia ya kumfanyia unyama huo huku akimdanganya kuwa atampa simu.
“Kuna wakati kweli ananipa simu kwa muda na kuninyang’anya.
“Kwa siku moja alikuwa ananiingilia mara mbili, asubuhi na jioni,” alisema mtoto huyo kwa uchungu.
 
Alisema kuwa baba mchungaji aliendelea kumfanyia ‘usodoma’ kwa muda mrefu.
Alisema baada ya kufika nyumbani kwa wazazi wake, mama yake alimgundua na kumtaka kueleza ukweli.
 
“Nilimweleza baba na mama jinsi mchungaji anavyonifanyia ukatili, walimwita nyumbani wakiwa tayari wameshaandaa polisi jamii, alipofika aliwekwa chini ya ulinzi lakini aliwaomba msamaha polisi jamii hao pamoja na wazazi huku akiahidi kutorudia tena.
 
“Kila mtu alikubaliana na msamaha na kumpa masharti kwamba afilisiwe vitu vyake vyote kama faini ya kosa.

MONALISA ACHOMOA KUOLEWA TENA.

MKONGWE kwenye soko la filamu Bongo, Yvonne Cherry ‘Monalisa’ amesema hatarajii kuolewa tena baada ya kuvunjika kwa ndoa zake ikiwemo ile ya prodyuza, George Otieno ‘Tyson’.
Yvonne Cherry ‘Monalisa’.
Akisimulia maisha yake mbele ya paparazi wetu, Monalisa alisema kuna siku walipokuwa kwenye kikao cha maandalizi ya send off ya mama yake (Suzan Lewis ‘Natasha’), alitania kwa kusema ataolewa Desemba lakini hakuwa ‘siriasi’.
“Sina mpango wa kuolewa kabisa, kwanza sina mchumba nitaolewaje? Siku ile nilikuwa natania tu kwa sasa sipo tayari kufanya tendo hilo,” alisema Monalisa.
Credit GLP

Hii ndio pete ya uchumba kaonekana nayo Nicki Minaj baada ya Dj Khaled kuomba uchumba, Rick Ross kasemaje?.

1 
Baada ya Dj Khaled kutokea MTV akitangaza mapenzi yake ya dhati kuhusu nia ya kumuoa Nicki Minaj, mrembo huyu wa Young Money ameonekana Crustacean Restaurant Los Angeles Marekani akiwa na pete ya uchumba kwenye mkono wake wa kushoto wakati alipotoka kula chakula cha jioni na baadhi ya marafiki zake waliosoma pamoja High school.

Unadhani hiyo pete kavishwa na Khaled????!!! Biiig No…. kwa mujibu wa Necole hii ni pete ambayo inaaminika alivishwa na boyfriend wake wa longtime kitambo anaitwa Safaree ambae nae amekua akionekana kavaa pete kama hiyo ya gold ambayo imesababisha watu waamini pia uwezekano wa ndoa ya siri ya wawili hawa.
2
3
Dj Khaled na huu mpango wake wa kutangaza nia ya kumchumbia Nicki Minaj aliiambia Power 106 kwamba anampenda sana Nicki Minaj kama ambavyo wanaume wengi wamekua wakivutiwa kumuoa pia, lakini akasisitiza kama Nicki atakataa kuchumbiwa na yeye… hakutakua na ubaya, bado ni marafiki…

MSHIRIKI WA TANZANIA (NANDO ) ATIMULIWA BIG BROTHER BAADA YA KUGOMBANA NA MSHIRIKI MWENZAKE.


Breaking News: Nando Disqualified-Elikem gets a Strike
Tanzania's Nando has been Disqualified from the Big Brother House.

After tonight's Evictions that saw Annabel and Sulu being given the boot, Big Brother then gathered all of the Housemates in the living room.

Today Big Brother reproached Nando for the fight that he had with Elikem on Friday. The heated face-off with Elikem saw the two fellas exchanging fiery words between them. Nando is the one that instigated the fight. Instigation and provocation is a violation of the Big Brother rules.

"Any Housemate who becomes physically violent will be removed from the House immediately. Violence can refer to self-inflicted violence, or violence towards another. Violence includes provocation, goading, bullying and victimisation," said Biggie.

This season Big Brother has imposed a Three Strike Rule, which will be applicable to Housemates who commit serious infringements. For this fight Nando received his second Strike and Elikem was served with his first Strike. Afterwards the Tanzanian was called into the Diary Room. He was given his third Strike for making threats against Elikem's life, saying: "I feel like stabbing him. A nigga like that deserves to die".

TASWIRA MBALIMBALI ZA ZIARA YA RAIS KIKWETE MKOANI KAGERA.


Rais Kikwete akihutubia umati Ngara.
Kivuko cha zamani kilichokuwa kikitumiwa na wananchi wa Ngara kuvuka mto Rusumo.
Kivuko kipya cha MV Ruvuvu katika mto Rusumo kilichozinduliwa na Rais Kikwete Jumamosi Julai 27, 2013.
Rais Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya Kagoma-Lusahunga katika wilayani Biharamulo.

TID AIBIWA POWER WINDOW NA BAADHI YA VITU KATIKA GARI LAKE.

Gari la TID baada ya kuibiwa vifaa.
Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Khaleed Mohamed 'TID', usiku wa kuamkia JANA ameibiwa vifaaa mbalimbali katika gari lake ikiwemo power window. Kupitia akaunti yake ya Facebook, TID ameandika kuwa mtu aliyemwibia atakuwa anamjua na akaahidi kutoa shilingi laki mbili kwa mtu atakayemtajia mwizi wake ambapo ametoa na namba yake ya simu.

MTOTO WA DAVIS MOSHA AITWA CHELSEA KUFANYA MAJARIBIO,TAZAMA AKIFANYA MAHOJIANO NA VOA.

Picture
Davis Mosha "The Boss" akifanya mahojiano na kituo cha VOA jijini Washington DC, kulia ni mwanae Edgar Mosha mwanafunzi mwenye kipaji cha masomo na soka.
Picture
Edgar Davis Mosha mtoto wa mfanyabiashara tajiri na maarufu boss wa kampuni ya DELINA, Bwana Davis Mosha ahojiwa na VOA (Voice of America). Edgar na baba yake wametua kwa kishindo nchini Marekani wakitokea Uingereza ambapo Edgar amepeperusha vyema bendera ya Tanzania kwa kuitwa  kufanya majaribio na klabu ya Chelsea ya Uingereza. Swahili TV itakuletea Exclusive video karibuni.
Picture
Kutoka kushoto; Juliet , Sunday Shomary, Edgar Mosha, Davis Mosha "The Boss" na Chief wa VOA Idhaa ya Kiswahili Dkt. Hamza Mwamoyo.

Hatimaye Cesc Fabregas akubali kwenda Manchester United.

Chanzo cha habari cha The Daily express kimeeleza kwamba Cesc Fabregas amekubali kujiunga na Manchester United.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 amekuwa gumzo baada ya ofa mbili za kumnunua toka kwa Manchester United kukataliwa, lakini sasa mchezaji huyo wa
kimataifa ameonesha dhamira yake kurudi Ligi ya Uingereza.
Wakala wa Fabregas Darren Dein amekutana na makamu mwenyekiti wa Manchester United, Ed Woodward na imebainika kwamba Nyota huyo wa zamani wa Arsenal yuko tayari kujiunga na Manchester United msimu ujao.
Fabregas ana furaha na anakubaliana na vigezo vilivyotolewa na Man United na sasa atamsikiliza bosi mpya wa Barcelona Gerardo Martino kama atamruhusu kuondoka Nou Camp, lakini kwa upande wa mchezaji huyo yuko tayari kupeleka maombi ya kuondoka Barca.

Meya atishia kumuua Mbunge • Alitoa kauli hiyo mbele ya DC, akaachwa.

MEYA wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata, amefunguliwa jalada polisi akidaiwa kutishia kumuua mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia (CHADEMA), katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichohudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemema, Amina Masenza.

Matata ambaye ni Diwani wa Kata ya Kitangiri aliyevuliwa uanachama wa CHADEMA mwaka jana kutokana na kusababisha mgogoro ndani ya chama mkoani Mwanza lakini alifungua kesi mahakamani kupinga uamuzi huo ambapo kesi hiyo bado inaendelea.

Hata hivyo katika hatua ya kushangaza, Septemba mwaka jana, Matata alichaguliwa kwenye mkutano ambao ulikuwa haukidhi akidi ya wajumbe ambao ni madiwani 14 na kwa mujibu wa sheria ndio wanaounda halmashauri hiyo mpya iliyomegwa kutoka katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini hapa, Kiwia alisema Matata alimtishia kumuua Julai 26, mwaka huu, katika kikao hicho na kwamba tayari amefungua jalada polisi mkoa Mwanza kulalamikia vitisho hivyo.

Kiwia alisema kuwa chanzo cha vitisho hivyo ni msimamo wake wa kumpinga Meya Matata kuongoza kikao hicho ambapo siku hiyo mbunge huyo alisimama na kumuomba Mkurugenzi wa Manispaa, Zuberi Mbyana, amteue mwenyekiti wa muda ili aongoze kikao.

Sunday, July 28, 2013

KIBAKA ANUSURIKA KUFA KWA KIPIGO CHA WANANCHI KAWE.


Mtuhumiwa wa wizi akiomba kusamehewa wakati mtu mwenye hasira kali akijiandaa kumtupia tofali kichwani ambalo lilimjeruhi vibaya mtuhumiwa huyo.
Mwananchi mwenye hasira akimsulubu mtuhumiwa huyo kwa teke.
Akisulubiwa kwa bakora na mmoja wa wananchi waliochoshwa na wizi.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate