EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, February 28, 2013

Mbeya: Igodima waandamana na kujigawia eneo la biashara baada ya ahadi kutokutekelezwa

WAKAZI wa Mtaa wa Igodima kata ya Iganzo Jijini Mbeya wameandamana kushinikiza kutekelezewa ahadi walioahidiwa na Diwani wa Kata hiyo ya kuwagawia eneo kwa ajili ya kufanyia biashara.

Wakazi hao zaidi ya 50 wameandamana hadi katika Ofisi za kata na kupokelewa na uongozi wa kata hiyo akiwemo Diwani Uswege Furika (Chadema) na Ofisa Mtendaji wa kata hiyo Jumapili Mwasenga  huku wakiwa na majembe mikononi wakishinikiza kuanza kugawiwa eneo hilo.
Awali ilidaiwa kuwa Diwani huyo aliwaahidi wananchi hao kuwapa eneo kwa ajili ya biashara ambapo aliwaambia wananchi hao kufika eneo husika asubuhi mapema kwa ajili ya kila mtu kuoneshwa sehemu yake ambayo angefanyia biashara zake.
Wakazi  zaidi ya 50 wameandamana hadi katika Ofisi za kata ya Iganzo wakidai kupewa eneo la kufanyia biashara huku wakiwa na majembe wakimtaka mweshimiwa diwani wa kata hiyo awagawie eneo hilo kwani wamechoka kudaganywa mara kwa mara
Ni vurugu tupu
Diwani Uswege Furika (Chadema) kata ya iganzo akiwatuliza wakazi wake watulie ili awaeleze ukweli kilichotokea
Kiukweli mambo yote anayafahamu yulee yaani akimnyooshea afisa mtendaji wa kata hiyo kuwa anafahamu vyema juu ya kiwanja hicho cha soko 
Afisa Mtendaji wa kata Iganzo Jumapili Mwasenga  amemkana mweshimiwa diwani kuwa hana taarifa yeyote juu ya swala hilo huku akisema jamani wananchi muulizeni vizuri diwani wenu sisi tunafanya kazi kimaandishi
Wananchi wangu sasa sijui tufanyeje maana naona hili swala limekuwa gumu kwangu  itabidi nikae na uongozi wangu halafu nitawapa jibu
Mweshimiwa diwani tuna taka haki yetu 

Taarifa ya Mabadiliko ya Mfumo wa Ukusanyaji Mapato Hospitalini Muhimbili

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MABADILIKO YAMFUMO WA UKUSANYAJI MAPATO

Menejimenti ya Hospitali ya Taifa Muhimbili iko kwenye mchakato wa kutekeleza mikakati mbalimbali inayolengakuongeza mapato ili kuiongezea uwezo wa kifedha unaohitajikakatika kuboresha utekelezaji wa shughuli mbalimbali zaHospitali ikiwemo utoaji wa huduma kwa wagonjwa. Mikakati hiyo pamoja na malengo mengineyo, inakusudia kuhakikisha kuwa Hospitali inakusanya kikamilifu mapato yatokanayo naada mbalimbali wanazolipa wagonjwa ili kuchangia gharama za huduma mbalimbali zitolewazo hivyo kuongeza kiwango chaubora wa utoaji huduma ya tiba kwa wagonjwa.

Aidha, kufanikiwa kwa lengo hili kutaiwezesha Hospitali kuvuka lengo la kugharamia bajeti ya matumizi ya kawaida, kwa kutumia mapato ya ndani kwa asilimia arobaini kama Sera ya Mabadilikoya Taasisi za Umma inavyoelekeza. (Public Sector Reforms). Kwa sasa Hospitali inagharamia bajeti ya matumizi ya kawaidakwa kutumia mapato ya ndani kwa asilimia 58%.

MTOTO ABAKWA NA MJOMBA WAKE!!

Mkoani Geita Mtoto ambaye jina lake limehifadhiwa mwenye umri wa miaka 9 anaishi na Bibi yake baada ya wazazi kutengana amefanyiwa kitendo cha kikatili na cha udhalilishaji kwa kubakwa na mjomba wake na akimaliza kumbaka humwita rafiki yake ambaye nae humbaka wakati huo huo.

Mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa pili katika shule ya msingi Geita amesema amekuwa akifanyiwa vitendo hivyo mara kwa mara kabla ya kwenda shule licha ya kukataa mjomba wake humpiga na hata alipotoa taarifa kwa bibi,bibi alimwita na kumkanya kuacha lakini kijana huyo aliendelea kumbaka.

Tatizo la mtoto huyo limejulika shuleni hasa baada ya kuwa anachelewa shule na maendeleo kuwa mabaya huku wakati mwingi akitumia kwenda msalani kujisaidia hali iliyowalazimu waalimu kumuhoji na ndipo kugundua unyama huo.

CHRIS BROWN AJUTA KUMPIGA RIHANNA


LOS ANGELES, MAREKANI
CHRIS BROWN amesema kitendo chake cha kumpiga Rihanna ni kosa baya zaidi alilowahi kulifanya katika maisha yake, na kuongeza kuwa bado mwanadada huyo anampenda.
Staa huyo wa R & B - ambaye bado yupo kwenye kipindi cha uangalizi kutokana na shambulio alilofanya mwaka 2009 dhidi ya Rihanna anayetamba na kibao chake ‘Diamonds’, amedai kuwa sasa ni mtu aliyebadilika.
Alisema: “Wakati mwingine unagombana, unapigana na mtu unayempenda… Usiku ule ni wa majuto makubwa katika maisha yangu, kosa kubwa. Lakini ananipenda — ninaweza kusema nini? Mimi ni wa kusamehewa… lakini, ndiyo, ninafanya kazi kwa bidii kwa ajili ya hilo.”
Wawili hao ambao walijitenga baada ya tukio hilo, sasa wamerudi tena kuwa pamoja, na Chris, mwenye umri wa miaka 23, anasisitiza kuwa amejifunza kutokana na makosa yake na kwamba hataweza kumuumiza tena Rihanna.

Papa wawili katika mgongano wa kimadaraka

YAMETIMIA. Safari ya miaka saba ya Baba Mtakatifu Benedict XVI inakamilika leo pale atakapong’atuka rasmi katika uongozi wa Kanisa Katoliki, ifikapo saa 2:00 usiku kwa saa za Italia (saa 4:00 usiku kwa saa za Tanzania).
 
Kwa siku mbili, Papa amekuwa na shughuli nyingi katika makao yake, Gandolfo Castel, Vatican akijiandaa kimwili kuondoka, akiweka sawa nyaraka zake binafsi na zile za kanisa ambazo zitawekwa katika kumbukumbu.

Kwa upande mwingine Vatican, nchi ambayo ipo ndani ya Jiji la Rome iliyozungukwa na ukuta, ikiwa na ukubwa wa hekta 44 na wakazi 832 pekee, imekuwa katika hekaheka nyingi.
Jana, waumini zaidi ya 50,000 na wengine wengi kutoka sehemu mbalimbali duniani wakiwamo makardinali, maaskofu, mapadri na walei walialikwa kwa shughuli rasmi ya kumuaga kiongozi huyo.

Mtanzania apewa uwaziri Rwanda ni Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu

RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.
 
Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.

Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).

Meya CCM Bukoba atoswa

MGOGORO ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bukoba Mjini, unazidi kuchukua sura mpya baada ya madiwani wake tisa kuungana na wenzao wawili wa Chama cha Wananchi (CUF) na wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kukwamisha kikao cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kiketi jana kujadili bajeti ya 2014/2014.
Hatua hiyo inakuja siku moja baada ya madiwani 10 wa Halmashauri ya Mji wa Bukoba akiwemo Mbunge wa jimbo hilo, Balozi Khamis Kagesheki kutukanwa matusi ya nguoni kupitia vipeperushi vilivyosambazwa mjini humo na watu wasiojulikana.

Madiwani waliotukanwa matusi hayo mazito ni nane wa CCM na wawili wa CUF waliosaini hati ya kumtaka mkurugenzi wa manispaa hiyo kuitisha kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani ili kumng’oa Meya Anatory Amani anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi.
Halmashauri hiyo ina madiwani 24, watatu wa CUF, wanne wa CHADEMA na 17 wa CCM. Ili kikao cha baraza kiweze kuendelea ni lazima akidi ya mahudhurio iwe na nusu ya wajumbe jambo ambalo lilishindikana jana.

Wakizungumza kutoka mjini Bukoba, baadhi ya madiwani walisema kuwa Meya Amani ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kagondo, alipata wakati mgumu hadi kulazimika kukiahirisha kikao hicho.
Kwamba muda wa kuanza kikao ulipowadia, ukumbini walikuwemo wajumbe 11, yaani madiwani nane wa CCM, wawili wa CHADEMA na mmoja wa CUF, jambo lililomlazimu meya huyo kuwapigia simu baadhi ya wale ambao walikuwa hawajafika na kuwashawishi bila mafanikio.

Wizi wa ATM watikisa Mbeya wafanyakazi wa serikali walizwa zaidi ya mil. 20/-

WIMBI la wizi wa fedha kwenye mitandao ya benki kupitia njia ya mashine za kuchukulia fedha (ATM), umewatia hasara wateja wengi wa benki ambao zaidi ya sh milioni 20 zinadaiwa kuchotwa kwa nyakati tofauti na watu wanne wanaomiliki kadi zipatazo 150.

Uchunguzi uliofanywa umegundua kuwepo kwa mtandao wa wizi kwa njia ya ATM unaotumiwa na watu wanaojifanya kuwa ni madalali wa fedha wanaowalaghai watumishi wa serikali.

Madalali hao wanadaiwa kuwakopesha watumishi hao wa serikali kwa sharti kwamba wawapatie kadi zao za kuchukulia fedha benki kama dhamana.

Uchunguzi umebaini kuwa, mtindo huo umeenea katika maeneo kadhaa mkoani Mbeya na hasa ukiwalenga watumishi wa serikali ambao kutokana na hali ngumu ya kifedha, wamejikuta wakiingia kwenye mtego huo na kuamua kutoa kadi zao za ATM ili waweze kupata mikopo.

YANGA 1 – KAGERA 0


KIUNGO Mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima, jana ameiwezesha timu yake kutimiza jumla ya Pointi 42, baada ya kuifungia bao pekee dhidi ya Kagera Sugar, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

KITU CHA VICTORIA SOUND

Wednesday, February 27, 2013

Mizengo Pinda aponda wanaoibeza tume yake kuchunguza matokeo

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewaponda watu wanaoipinga tume aliyoiunda kuchunguza sababu za idadi kubwa ya wanafunzi wa kidato cha nne kuvurunda katika mtihani huo akieleza kuwa huenda watu hao hawaelewi ukubwa wa tatizo na jinsi linavyotakiwa lishughulikiwe. Katika matokeo hayo ambayo yanatajwa kuwa mabovu kuliko yoyote yaliyowahi kutokea katika historia ya Tanzania, asilimia 60 ya wanafunzi waliofanya mtihani huo walipata sifuri.
 
                                                     WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda
Pinda alisema hayo jana Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua mkutano wa siku moja kuhusu mafanikio ya ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi.

Alisema ni lazima waelewe kuwa mambo yatakayoangaliwa ndani ya uchunguzi huo ni mengi na si kama wanavyofikiri baadhi ya wanaopinga hivyo ni muhimu wakatulia na kusubiri matokeo.

“Wengine wanasema tume zipo nyingi, si kweli kwamba zipo nyingi na hazifanyi kazi, kila mtu ana mawazo yake, jambo hili ni kubwa na lazima lishughulikiwe kwa ukubwa wake,”alisema Pinda.

MAMBO MACHACHE YA KUYAFAHAMU ILI KUEPUKA KUSALITIWA

1.Amini hawezi kukusaliti
Jambo la kwanza kabisa ni kujenga imani kwamba mpenzi wako anakupenda, anakuheshimu na kukuthamini hivyo hawezi kushawishika kwa namna yoyote ile kukusaliti.

Hii itakufanya kuwa na furaha na yeye, pia utamfanyia mambo ya kumfurahisha. Ukiwa huna imani na mpenzi wako, unaweza kujikuta unapunguza mapenzi kwake na matokeo yake ukachochea yeye kuanza kukusaliti.

2.Mtosheleze
Mpenzi wako mchukulie kama mtoto. Unapomlisha unahakikisha ameshiba ndiyo unamuacha. Akitaka pipi unamnunulia. Vivyo hivyo kwa mpenzi wako. Mtoshelezea katika kila nyanja.

3.Muoneshe upendo wa hali ya juu, mpe heshima anayostahili na pale mnapokuwa kwenye mambo yetu yalee, mpe hadi aseme nimeshiba mpenzi wangu. Ukifanya hivyo aende nje kutafuta nini? Akienda, huyo ana tamaa zake za kijinga na ukibaini muache haraka.

4.Zungumza naye
Ndiyo, vunja ukimya, zungumza naye! Si vibaya ukawa unazungumza na mpenzi wako juu ya mambo yahusuyo uhusiano wenu. Muulize ni mambo gani ukimfanyia anasikia furaha, akikuambia na mambo hayo yakawa ndani ya uwezo wako, jitahidi kumtimizia.

5.Muulize, anachukizwa na mambo gani, akikuambia basi jiepushe nayo. Hata asipokuambia, ukimchunguza utayabaini tu.
Hayo ni baadhi tu ya mambo ambayo ukiyazingatia yanaweza kukusaidia katika kumfunga ‘spidi gavana’ kimtindo mpenzi wako ili asikusaliti. Kama itatokea akakusaliti licha ya kumfanyia yote hayo, huyo siyo mtu wa kuendelea kuwa naye.

Albino auawa, wawili wakatwa viungo

HALI ya wasiwasi imetanda miongoni mwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) nchini, baada ya watu watatu kukatwa viungo na mmoja wao kuuawa mwezi huu.

Katika miaka ya hivi karibuni, jumla ya albino 72 wameuawa, 34 wamenusurika, wengi wao kwa kukatwa viungo au kuumizwa. Makaburi 15 yamefukuliwa na viungo kuchukuliwa na kumekuwa na majaribio manne ya kufukua makaburi.
Katika matukio ya hivi karibuni, walemavu hao wakazi wa Tabora na Sumbawanga wamekatwa mikono ya kushoto. Ukatili huo safari hii umekwenda kinyume na ilivyokuwa mwaka 2010-2011 wakati mikono ya kuume ndiyo iliyokuwa inakisiwa.
Aliyeuawa ni
Lugolola Bunzari (7) na waliojeruhiwa ni Mwigulu Matonange (10) na Maria Chambanenge (39).

KAPOTIVE STAR SINGERS KUTOKA NDANI YA UBUNGO PLAZA 31.03.2013


IRENE MWAMFUPE JAMII Blog tutakuwepo ukumbini tujumuike pamoja.Ukumbi ni Ubungo Plaza.Tarehe 31.03.2013 kuanzia saa nane mchana mpaka saa mbili usiku,Mtu mmoja sh 15,000/=,Watu wanne 50,000/=watu watano 100,000/=

MACHO YOTE YANGA V/S KAGERA SUGAR LEO

Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho (Februari 27 mwaka huu) kwa  mechi tano zitakazochezwa katika viwanja tofauti.
 Nyuma y'umukino, ibyishimo byari byose ku bakinnyi ba Yanga barimo Haruna Niyonzima wigeze gukinira APR FC.
Vinara wa ligi hiyo Yanga wataikaribisha Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwa viingilio vya sh. 5,000 (viti vya bluu na kijani), sh. 8,000 (viti vya rangi ya chungwa), sh. 15,000 (VIP C na B) na sh. 20,000 (VIP A).Mechi nyingine za ligi hiyo ni Coastal Union vs Ruvu Shooting (Mkwakwani, Tanga), Polisi Morogoro vs Mgambo Shooting (Jamhuri, Morogoro), JKT Ruvu vs Toto Africans (Azam Complex, Dar es Salaam) na Mtibwa Sugar vs Tanzania Prisons (Manungu, Morogoro).

Utafiti wa Synovate wapondwa,wadau wasema ulikuwa na ajenda ya siri

BAADHI ya wasomi nchini wameuponda utafiti uliofanywa na Shirika la Synovate huku miongoni mwao wakienda mbali zaidi kwa kusema: “Ulikuwa na ajenda ya siri.”
                                     Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba 
Utafiti huo pia umepondwa na wanasiasa akiwamo Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba ambaye amesema haziamini tafiti zinazotolewa na Syonovate akidai hazina ukweli wowote.

Licha ya matokeo ya utafiti huo wa Desemba mwaka jana kuonyesha kushuka kwa asilimia 25 kwa umaarufu wa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa pamoja na chama chake, lakini unaweka wazi kwamba kiongozi huyu angechaguliwa kuwa Rais kama uchaguzi huo ungefanyika sasa.

Dk Slaa anaongoza kwa asilimia 17, akifuatiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

WEMA : NAFASI ZA KAZI ENDLESS FAME PRODUCTION


IMANI RADIO FM NA NEEMA FM ZAFUNGIWA NA TCRA


19 wafariki katika ajali ya Puto Misri

Zaidi ya watalii 19 wakiwemo waingereza na wafaransa ,wamefariki Kusini mwa Misri baada ya puto la joto walimokuwa kulipuka katika mji wa Luxor.
Ripoti zinaarifu kuwa kulikuwa na watalii ishirini katika puto hilo.
Moto na mlipuko vilisikika kabla ya puto hilo kuanguka Magharibi mwa Luxor.

REAL MADRRID YAIFUAMUA BARCELONA

REAL MADRID imefanikwa kuwang’oa Barcelona katika kombe la mfalme (Copa Del Rey) kufuatia ushindi mnono wa mabao 3-1 ndani ya uwanja wa Nou Camp.
Cristiano Ronaldo and Sergio Ramos
Shujaa na nyota wa mchezo alikuwa ni Cristiano Ronaldo aliyeifungia Real Madrid mabao wawili.
Real Madrid inasonga mbele kwa jumla ya magoli 4-2 kufuatia sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza uliofanyika Santiago Bernabeu.
Bao la kwanza la Real Madrid lilifungwa na Ronaldo kwa njia ya penalti katika dakika ya 14.
Ronaldo aliingia na mpira ndani ya eneo la hatari la Barcelona, akakatwa na Gerard Piqué na mwamuzi hakusita kutoa penalti.

Tuesday, February 26, 2013

RAY AKONGOROKA AIBUA MASWALI KWA WADAU WAKE

MWIGIZAJI Vincent Kigosi ‘Ray’ amezua hofu kwa ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wake baada ya kukongoroka ghafla akihisiwa anaumwa, Ijumaa Wikienda limemfuatilia hatua kwa hatua.
 
Vincent Kigosi ‘Ray’ alivyo kwa sasa.
KWENYE ‘BETHIDEI’ YA BATULI
Wiki kadhaa zilizopita paparazi wetu alishtuka alipomuona Ray kwenye ‘bethidei’ ya mwigizaji sistaduu Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ndani ya Hoteli ya Shamoll iliyopo Sinza ya Lion, Dar akiwa amekongoroka na kuibua maswali kwa wahudhuriaji.
 
Akiwa ukumbini hapo, minong’ono ilienea kuwa Ray alionekana kukondeana katika kipindi kifupi huku baadhi ya watu wakisikika wakiulizana kulikoni kwani alikuwa meza moja na bonge la mtu, Jacob Steven ‘JB’ hivyo kumfanya kuonekana mdogo mno.

Askari wanaswa kwa ujambazi.

Wamo pia wafanyabiashara wakidaiwa kushiriki mauaji

JESHI la Polisi katika mikoa ya Iringa na Mbeya, limewakamata watu 29 wakiwemo askari wawili wanaotuhumiwa kuwa majambazi hatari waliohusika na matukio ya mauaji na uporaji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athuman, aliwaambia waandishi wa habari kuwa miongoni mwa waliokamatwa ni askari Samuel Balumwina (31) mwenye namba MT 85393 kutoka kikosi cha JKT Itende (844KJ) na PC Samuel Kigunye (27) namba G.9101.
Askari hao wanatuhumiwa kuazimisha sare za majeshi hayo kwa majambazi. Na kuongeza kuwa polisi atashtakiwa kijeshi na kuunganishwa na wengine kwa makosa ya mauaji na uporaji wa mali.

Watuhumiwa hao wa ujambazi wanadaiwa kuhusika katika matukio makubwa likiwemo la mauaji ya askari polisi G 68 PC Japhary aliyepigwa risasi ubavuni akiendesha gari la namba PT 0665 lilipokuwa doria Mkwajuni, wilayani Chunya.

Vumilia, endelea kuwa ‘singo’ kuliko mpenzi pasua kichwa

KILA mtu angeyaheshimu mapenzi, angejua jinsi ya kulinda hisia za mwenzi wake. Angeelewa maana ya kupenda, asigekuwa na shaka pale anapopendwa. 
Angeishi ndani ya mwenzake, hivyo kuumizana kusingekuwepo, migogoro mikubwa na kuachana isingetokea.Migogoro mingi inatokea kwa sababu wengi wameyageuza mapenzi kama mchezo (game), hawajui kuwa saikolojia inaonya vitendo vya kuucheza shere moyo wa mtu. Kumfanyia hivyo mtu mwenye hisia za ndani na za kweli katika kupenda unaweza kuua bila kukusudia. 
Katika sehemu ya kwanza ya makala haya wiki iliyopita, nilieleza kuwa kama hujawa tayari kupenda, kunyenyekea na kuheshimu ni vizuri ukakaa pembeni kwa sababu unaruhusiwa kucheza game na mtu lakini ni kosa kubwa kucheza game na moyo wa mtu.

Waziri amuondoa, aagiza katiba mpya ifutwe, itumike ya zamani

SERIKALI imemuondoa Msajili wa Vyama na Klabu za Michezo nchini na kuagiza kufutwa kwa katiba mpya ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na badala yake itumike ile ya mwaka 2006.

Hatua hiyo, imekuja baada ya hivi karibuni kuibuka kwa utata juu ya katiba mpya ya TFF, iliyopitishwa kwa njia ya waraka, wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo uliopangwa kufanyika Februari 24 na ule wa Bodi ya Ligi Februari 22, kabla ya kusitishwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alisema kuwa ameamua kumteua msajili mpya, baada ya aliyekuwepo kupitisha katiba mpya ya TFF kinyume na utaratibu.
Alisema kuna mengi yalijitokeza ikiwemo baadhi ya wagombea kulalamikia kuenguliwa, hivyo wizara iliamua kuliangalia hilo kwa uzito unaostahili na kuamua kuchukua hatua stahiki.
             Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara
Mukangara alisema sheria Na.12 ya BMT na marekebisho yake Na.6 ya mwaka 1971 pamoja na kanuni za BMT na kanuni za usajili Na. 442 mwaka 1999 zimekiukwa.

Mama Kanumba alia na kalenda za mwanaye

MAMA mzazi wa aliyekuwa msanii nyota wa filamu nchini, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtagoa, amelalamikia kitendo cha mtu aliyetengeneza na kusambaza kalenda zenye picha ya mtoto wake bila idhini yake.

Akizungumza mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Flora alisema ni bora yule aliyetoa kitabu, alifanya ustaarabu pamoja na Zamaradi Mketema aliyetoa ‘CD’ iliyokwenda kwa jina la ‘Neno la Mwisho’ ambao walifuata taratibu na ridhaa, kisha kumlipa fedha aliyotaka.

“Zamaradi na yule aliyechapa kitabu cha Kanumba, hawa walikuja wakazungumza na mimi nikawatajia fedha niliyotaka wakanilipa bila ubishi, lakini huyu mtu aliyefyatua kalenda za mwaka huu, yeye hana ustaarabu, kwani amejifanyia kiholela tu kwa kutumia jina la mtoto wangu bila ridhaa yangu na hajailipa familia chochote, hii si sawa,” alilalamika Flora.

Aliviomba vyombo vya habari vimsaidie kumtafuta mhusika huyo kwa sababu hata namba walizoziandika chini ya kalenda hizo zikipigwa hazipatikani.
Aliongeza kuwa baada ya kifo cha mwanaye, wapo watu wengi waliofaidika huku wengine wakitangaza kuwa wamevunja rekodi ya mauzo lakini bila hata kwenda kuipa familia kiasi chochote cha fedha kama pole.

Mbowe ahoji Tume ya Pinda kuchunguza chanzo cha matokeo mabaya ya kidato cha nne

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, ameponda hatua ya serikali kuunda tume ya kuchunguza chanzo cha matokeo mabaya ya kidato cha nne, akisema kufanya hivyo bila uwajibikaji ni matumizi mabaya ya rasilimali za walipa kodi.
Akitoa salaam baada ya kushiriki uzinduzi wa jengo la Chuo cha Walezi wa Watoto cha Kumbukumbu ya Helen, katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Neema wilayani Hai, Mbowe alisema mkakati huo ni wa kupunguza hasira ya umma dhidi ya serikali.
Alisema kuwa kutokana na ubovu wa mfumo wa elimu, kinachohitajika si tume ya kuchunguza mambo yanayojulikana, bali kunahitajika hatua za kisera, kibajeti, kitaasisi na kiuongozi.

Mbowe alifafanua kuwa masuala  hayo serikali ya CCM haiko tayari kuyafanyia kazi kwa sababu ya kupuuza sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Alisema kuwa kitendo cha wa Waziri wa Elimu, Dk. Shukuru Kawambwa, na viongozi waandamizi wenzake wizarani kuendelea kuingia ofisini huku asilimia 90 ya wanafunzi wa sekondari wakiwa wamefeli vibaya ni aibu kwa Waziri Mkuu na Rais.
Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, alisisitiza kuwa hatua yoyote inayochukuliwa na serikali katika suala hilo inapaswa kutanguliwa na uwajibikaji kwa watu waliopewa dhamana ya kusimamia elimu ya watoto wa Tanzania.

“Ndugu zangu leo tunashuhuhudia tukio muhimu sana hapa Kalali, kuanzishwa kwa chuo kitakachofundisha walimu au walezi wa watoto hawa yatima walioko hapa ambao kweli ni watoto waliokosa fursa fulani katika maisha yao.
Alisema kuwa wakati wanafikiria kuwatunza hao watoto yatima, ni vyema wakaanza kutafakari kama taifa juu ya elimu ambayo wamewatia giza katika upeo wa macho yao na maisha yao kwa kuwafelisha.
Mbowe alisema kuwa hana haja ya kupinga hatua ya Pinda kuunda tume, lakini hatua yoyote itayochukuliwa na serikali bila kuendana na uwajibikaji ni ghiliba kubwa kwa Watanzania.

CHADEMA yailiza tena CCM

KWA mara nyingine tena Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimekiliza Chama cha Mapinduzi (CCM) baada ya Mbunge wake wa Meatu, Meshack Opurukwa, kushinda kesi katika Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, kwa pingamizi la awali kutokana na mlalamikaji kutofuata sheria katika kukata rufaa.

Kesi hiyo iliyokuwa imefunguliwa na mpiga kura wa jimbo hilo, ambaye pia ni Katibu wa Mbunge aliyeshindwa, Masanja Salu, ilitupiliwa mbali na jopo la majaji, Edward Rutakangwa, Catherine Urio na Mbarouk Salum Mbarouk.

Katika kesi hiyo, mlalamikaji Salu, alikuwa na madai matatu tangu awali, la kwanza likiwa ni kutumia ukabila kwenye kampeni, tofauti ya kura zilizotangazwa na msimamizi wa uchaguzi na zile zilizopelekwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na mlalamikaji kudai kuwa Opurukwa alikiuka taratibu za kampeni kwa kujiendea bila utaratibu.

Awali katika kesi hiyo iliyokuwa inasikilizwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, mbele ya Jaji Fredrick Wambali, mlalamikaji alishindwa kuthibitisha malalamiko yake, hivyo mahakama hiyo kumpa ushindi Opurukwa Mei 4 mwaka jana.

CCM wadhalilishana Bukoba..Wamsusia meya, watuma ujumbe mzito kwa Mangula

CHAMA cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Bukoba Mjini, kimeingia katika siasa chafu za kudhalilishana huku vipeperushi vya kuwatusi madiwani 10 wa chama hicho na wale wa Chama cha Wananchi (CUF) vikisambazwa mitaani.

Madiwani hao waliochafuliwa kwa matusi mazito ya nguoni ambayo mengine hayaandikiki kwa kuzingatia maadili ni wale nane wa CCM akiwemo Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki, na wawili wa CUF waliosaini hati ya kumtaka mkurugenzi wa manispaa hiyo kuitisha kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani ili kumng’oa Meya Anatory Amani anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi.

Hatua hiyo inakuja siku chache tangu Dk. Amani aamue kupuuza maagizo ya Makamu Mwenyekiti wao chama hicho taifa, Philip Mangula, kwa kufungua kesi mahakamani kupinga kujadiliwa na kung’olewa na madiwani.
Mangula ambaye alilazimika kufika mjini Bukoba mwezi uliopita ili kunusuru mtafaruku huo, aliagiza madiwani nane wa CCM waliokuwa wamesaini hati hiyo, waondoe tuhuma hizo na kuzipeleka kwenye chama ili zipatiwe ufumbuzi.

Lakini katika hatua ambayo imetafsiriwa kuwa mgogoro huo unazidi kushika kasi, juzi vipeperushi hivyo vya matusi vilisambazwa na watu wasiojulikana kwa kuvibandika katika maeneo mbalimbali ya mji wa Bukoba.
Madiwani waliosaini hati ya kutaka kuitishwa kikao cha kumng’oa meya huyo mbali na Kagasheki ni Naibu wake, Alexander Ngalinda (Kata ya Buhende) na Yusuf Ngaiza (Kashai) ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Manispaa ya Bukoba.

Polisi watumia nguvu kuzuia maiti kusafirishwa Geita

POLISI wa Mkoa wa Geita wametumia nguvu kuzuia msafara wa waombolezaji waliokuwa na mwili wa marehemu mfanyabiashara, Yemuga Fungungu (48), mwishoni mwa wiki iliyopita na kusababisha vurugu kubwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Leonard Paulo alikuwapo wakati askari wake walipoingilia msafara huo na kusababisha vurumai kubwa.
Waombolezaji hao walikuwa wakiuhamisha mwili wa marehemu Fungungu kutoka Hospitali ya Runzewa kuupeleka katika Hospitali ya Geita.

Sakata hilo la ndugu na polisi lililotokea saa nane mchana juzi Jumamosi katika Pori la Samina, Geita na polisi wakiwa kwenye magari matatu wakiwa wamesheheni silaha mbalimbali walifika na kuzuia mwili wa marehemu kusafirishwa.

Baadhi ya ndugu wa marehemu akiwamo mkewe, wanadai kwamba Fungungu alifariki dunia baada ya kupigwa risasi na polisi wanaosemekana kwamba walimvamia nyumbani kwake usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita kisha kupora mamilioni ya fedha. Wanadai kwamba alipigwa risasi tumboni na kichwani katika Kijiji cha Runzewe, Wilaya ya Bukombe mkoani hapa.

Katika tukio hilo inadaiwa kuwa kiasi cha Sh360 milioni kiliporwa. Kati ya fedha hizo, Sh60 milioni zinadaiwa kwamba zilikuwa kwenye gari wakati Sh300 milioni zilikuwa kwenye masanduku mawili yaliyokuwa ndani ya nyumba.

Mamilioni yatolewa kwa dijitali

KATIKA mkakati wa kusambaza mawasiliano ya mfumo mpya  wa dijitali katika mikoa 14 nchini, jumla ya Sh50 milioni zimetolewa na Kampuni ya StarTimes ili kuwezesha kazi hiyo.
Meneja Habari wa StarTime, Erick David aliitaja mikoa ambayo kampuni hiyo imewekeza kuwa ni pamoja na Shinyanga, Iringa, Tabara,  Ruvuma, Mara, Kigoma  na Manyara.
 
David aliyasema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine, alisema hatua hiyo ni kuunga mkono Serikali kuhusu dhamira ya kusambaza mfumo  huo nchi nzima, ambapo inakwenda sambamba na kutoa huduma mpya ya kukodisha ving’amuzi kwa wateja.

Mikoa mingine ni Singida,  Kusini Pemba, Kaskazini Pemba na Rukwa, Mtwara na Lindi  na kwamba mikoa 23 inatarajia kupatiwa huduma hiyo kufikia mwisho wa mwaka huu.
“Huduma hii ya kukodisha ving’amuzi ni mpya  kutoka Startimes, kutatua changamoto zinazoikabili dijitali na kwamba mteja anatakiwa kutoa Sh39,000 kama dhamana ya kuchukua king’amuzi na pia mteja anatakiwa kulipa  Sh6,000 kama malipo ya kila mwezi  na itakuwa na chaneli 15 za nyumbani na nyinginezo,” alisema David.

Alisema mteja anaweza kurudisha  na akarudishiwa Sh39,000 aliyotoa kama dhamana baada ya matumizi yake na huduma hiyo inayolenga kuwanufaisha watu wa kipato cha chini kwani licha ya kukodishwa  utapata  channel zaidi ya 15 saa 24 kwa mwezi mzima.
Alisema katika kuifanya jamii kuwa karibu na ulimwengu huu wa dijitali na kuepuka  gharama kubwa za ununuzi wa ving’amuzi na malipo ya vifurushi kwa kila mwezi kampuni yao inarahisisha hilo.

Vinara tisa urais

WAKATI baadhi ya wanasiasa wakiwa wameanza kujiwinda kwa ajili ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Shirika la Utafiti la Synovate limetoa matokeo ya utafiti wake ambao unaonyesha vigogo tisa kuwamo katika mchuano huo.
Utafiti huo umeonyesha kuwa endapo uchaguzi huo ungefanyika sasa, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa angeibuka mshindi baada ya kuongoza orodha hiyo akipata asilimia 17.
 
Katika matokeo ya utafiti huo uliofanywa Desemba mwaka jana, Dk Slaa anafuatiwa kwa mbali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amefungana na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kila mmoja akipata asilimia tisa.

Hata hivyo, licha ya kuongoza, Dk Slaa ameporomoka kwa asilimia 25 ikilinganishwa na matokeo ya utafiti kama huo uliofanywa na taasisi hiyo mwaka 2011 ambapo alipata asilimia 42.

Kadhalika, umaarufu wa Pinda ambaye anaongoza miongoni mwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeshuka kwa asilimia tatu kutoka 12 za mwaka juzi, wakati Zitto ameendelea na kiwango kilekile cha asilimia tisa alizopata katika utafiti uliotangulia.
Wengine wanaofuata na asilimia walizopata kwenye mabano ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (8), Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (7) na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (5).

Pia wamo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (4) ambaye amefungana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (4) na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2).

Ikilinganishwa na utafiti wa 2011, Lipumba ameporomoka kwa asilimia tisa.
Lowassa amepanda kwa asilimia sita, Dk Magufuli asilimia nne, Mbowe na Membe wamepanda kwa asilimia mbili kila mmoja, wakati Sitta amebaki katika kiwango kilekile cha asilimia mbili.

Monday, February 25, 2013

Matokeo ya kidato cha Nne: Wakuu wa shule wadai ilitungwa kwa mfumo tofauti

MATOKEO mabaya ya mtihani wa kidato cha nne yamezidi kuibua mapya, baada ya wamiliki wa shule na vyuo binafsi nchini kusema mitihani ilitungwa kwa mfumo tofauti na uliozoeleka miaka yote, huku tume iliyounndwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ikipondwa na baadhi ya watu.
Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi nchini (TAMONGSCO), Mahmoud Mringo alisema kwamba maswali waliyoulizwa watahiniwa yalikuwa ya kujieleza tofauti na miaka ya nyuma, ambapo mfumo uliotumika uliwataka watahiniwa kutaja vitu tu bila ya kulazimika kuvielezea kwa undani.

Kauli yake iliungwa mkono na Mkuu wa Taaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Marian, Florence Mapunda ambaye alisema kuwa mtihani wa mwaka jana ulitaka zaidi watoto kujieleza tofauti na miaka ya nyuma wakati wanafunzi walipokuwa wanakariri.
Hata hivyo, Msemaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), John Nchimbi alisema mfumo wa mtihani haukubadilika kwa namna yoyote na kuwa upo kama ule wa miaka yote.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo, kwa upande wake alisema madai yanayotolewa hayana msingi, huku akihoji kwa nini yasitoke tangu mitihani ilipokuwa ikifanyika na badala yake yanatoka baada ya kutangazwa kwa matokeo.

Maskini Simba...Yalala kwa Mtibwa, vurugu kubwa zaibuka Taifa

KAMA ni mtoto, unaweza kusema si riziki. Hivi ndivyo hali ilivyo ndani ya klabu ya Simba, ambako imeendelea na mwenendo wa shaka katika Ligi Kuu Tanzania bara, baada ya jana kukubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa wakata miwa wa Mtibwa Sugar kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaam.

Simba ambao ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo, msimu huu imekuwa na mwenendo mbovu na hata kufuta mawazo ya kutetea taji hilo miongoni mwa mashabiki wake, ambao hivi sasa wako katika hali mbaya kutokana na kufanya vibaya.
Hadi sasa, Simba imepoteza mechi tatu huku ikijikongoja katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 31 baada ya kushuka dimbani mara 18. Yanga wako kileleni kwa pointi 39 huku Azam ikifuatia kwa pointi 36.

Katika mechi ya jana, Simba ilianza kwa kasi na dakika ya tatu tu, Shomari Kapombe alipokea pande la Amir Maftah, lakini shuti lake likaokolewa na kipa Hussein Sharrif, kabla ya Mtibwa kujibu mashambulizi na kupata kona ambayo haikuzaa matunda.
Alikuwa ni Salvatory Ntebe dakika ya 16, aliyeiandikia Mtibwa bao hilo la pekee, baada ya kuunganisha mpira uliotokana na kona.

Dakika ya 41, Simba walifanya mabadiliko kwa kumtoa Ramadhani Chombo ‘Redondo’ na nafasi yake kuchukuliwa na Kigi Makasi.

Tume ya Pinda yapingwa... Dk. Slaa adai hoja ya Mbatia ilikuwa na majibu yote

 
SIKU moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuunda tume maalumu ya kuchunguza matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni, wanasiasa na wasomi wamempinga wakidai ni kupoteza muda na fedha kwa kuwa hoja binafsi ya Mbunge wa kuteuliwa, James Mbatia ilikuwa na majibu.

Kwa nyakati tofauti katika mahojiano na gazeti hili, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, na Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Benson Bana walihoji ni tume na kamati ngapi zimeundwa na kutolewa taarifa kuhusu matatizo ya elimu katika miaka 15 iliyopita na hatua zipi zimechukuliwa kurekebisha dosari zilizoonekana.

Dk. Slaa alishangazwa na hatua hiyo ya Waziri Mkuu kuunda tume kwa ajili ya kufuatilia kufeli kwa wanafunzi, akisema ni juzi tu Bunge limemaliza kikao chake Dodoma na kuitupilia mbali hoja binafsi ya Mbatia.

Alisema hoja binafsi ya Mbatia ilikuwa na nia ya kupitisha azimio la Bunge kuunda kamati teule ya kuchunguza tatizo la udhaifu katika sekta ya elimu, lakini kwa ushabiki wa wabunge wa CCM akiwemo Waziri Mkuu, ilikataliwa.

Zitto ahusishwa kifungo cha MwanaHalisi

WAKATI wadau wa tasnia ya habari wakihoji ubabe uliotumiwa na serikali kulifungia gazeti la wiki la MwanaHalisi kwa madai ya uchochezi, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Assa Mwambene, amembebesha sakata hilo Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto.

Mwambene katika kuivua lawama serikali, alidai kuwa Zitto alikuwa mtu wa kwanza baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo, aliyemtahadharisha asiende ofisini kumchekea Mkurugenzi wa Kampuni ya Hali Halisi, wachapishaji wa MwanaHalisi, Said Kubenea ili isije kumharibia kazi.

Serikali ililifungia gazeti la MwanaHalisi Julai 30 mwaka jana, kutochapisha nakala yoyote kwa muda usiojulikana kwa madai ya kuandika habari na makala ya uchochezi.
MwanaHalisi ndilo gazeti lililoandika kwa undani tukio zima la watu wanaoshukiwa kumteka kumpiga, kumng’oa meno na kisha kumtelekeza Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madakatari nchini, Dk. Stephen Ulimboka.

Mwambene ambaye aliteuliwa kushika nafasi hiyo kutoka kwa Clement Mshana aliyehamishiwa TBC, alijikuta akitoa siri hiyo Ijumaa iliyopita wakati wa kongamano la kutimiza miaka 50 ya Redio ya Ujerumani ‘Deutsche Welle’ (DW) Idhaa ya Kiswahili lililofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo ilikuja baada ya kubanwa kwa maswali yaliyokuwa yanamshutumu yeye na serikali yake kubana uhuru wa vyombo vya habari, huku baadhi ya washiriki wakiinyooshea kidole cha moja kwa moja serikali katika suala zima la kulifungia MwanaHalisi ili lisizidi kuwaumbua.

Sunday, February 24, 2013

Iringa: Ajali yametokea alfajiri, sababu ya ulevi wa pombe (?)

Picture
Picture
Picha na Meshack Maganga; Maelezo  na Francis Godwin (via blog)
Ajali  mbaya  imetokea  mjini Iringa majira ya saa kumi alfajiri ya leo,  eneo la Makosa ama CRDB ya  zamani kwenye barabara  kuu ya Iringa -Dodoma baada ya gari aina ya RAV 4 yenye namba za usajili T 319 AFL kuhama njia na  kuigonga  gari nyingine inayotumika kama taxi yenye namba  za usajili T 510 AYU iliyokuwa  ikiendeshwa na dereva Kevin Kaduma.

Ajali  hiyo  imetokea wakati  dereva  wa RAV4 hiyo akitokea maeneo ya mji  wa Iringa akielekea  mwelekeo ambao wakazi  wa mji wa Iringa wamekuwa  wakipata  starehe zao eneo la  Dragon Bar na Club  Twistas  kuendelea  kumalizia starehe za mwisho  wa wiki.

Mama Kikwete akabidhi msaada wa vifaa vya tiba Rufiji, Pwani

Picture
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,mara baada ya makabidhiano ya msaada wa vifaa vya tiba na dawa wenye thamani ya shilingi Mil 20 kutoka Vodacom Foundation kwa ajili ya wakazi wa eneo

Hyatt Regency Kilimanjaro Hotel na Green Waste Pro wasafisha fukwe za Kivukoni Front

Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro imeamua kuialika kampuni ya usafi ya Green Waste Pro baada ya kuona juhudi zao za kuweka Manispaa ya Ilala safi na mabadiliko yanaonekana ndipo wakaamua kushirikiana nao katika zoezi la kusafisha fukwe hizo.
Picha juu na chini ni Wafanyakazi wa Hoteli ya Hyatt Regency wakishirikiana na Kampuni ya usafi ya Green Waste Pro kusafisha fukwe za Kivukoni Front jijini Dar zilizopo mbele ya hoteli hiyo ikiwa ni utaratibu wa hoteli hiyo kufanya zoezi hilo mara moja kwa mwezi ili kutunza mazingira.

Saturday, February 23, 2013

IMAM WA MSIKITI WA MWAKAJE AUWAWA ZANZIBAR

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar 
SIKU chache baada ya kutokea kifo cha Padri Evarist Gabriel Mushi na watu wasiojulikana kwa kupigwa risasi kichwani eneo la Beit el Raas, Jana Imamu wa Msikiti wa Mwakaje amefariki dunia baada ya kupigwa mapanga hadi kufa.

Kwa mujibu wa maelezo ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ahmada Khamis amethibitisha kutokea kwa tukio hilo hapo jana mchana majira ya saa 8 mchana na kumtaja aliyefariki ni Sheikh Ali Khamis ambaye ameuawa na watu wasiojulikana.

Kamanda Ahmada alisema Sheikh Khamis mbali ya kuwa ni Imamu wa Msikiti lakini pia ni mkulima na ameuliwa wakati akiwa katika mazingira ya kazi zake ndani ya shamba lake huko Kidoti Mkoa wa Kaskazini Unguja.

CHADEMA: Kawambwa amebakiza siku kumi

KAULI ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa kwamba hawezi kujiuzulu, imeamsha hasira ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kimesisitiza kwamba maandamano ya kumng’oa yako pale pale na sasa amebakiza siku kumi.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi, John Mnyika wakati alipotakiwa kueleza msimamo wa chama chao, hasa baada ya kauli ya Waziri Kawambwa jana kwamba hawezi kujiuzulu.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mnyika ambaye ni Mbunge wa Ubungo, alisema kauli aliyoitoa Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe kwamba anampa siku 14 Waziri Kawambwa ajiuzulu, vinginevyo atang’olewa kwa maandamano bado ipo pale pale.
Alisema majibu ya Waziri Kawambwa yameonesha dharau kwa Watanzania, hasa walalahoi ambao ndio watoto wao wengi wamepata ziro katika mitihani yao ya kidato cha nne.

“CHADEMA tunaendelea kusisitiza kwamba Waziri Kawambwa ang’oke, awajibike, ameshindwa kazi na hili tunamaanisha,” alisisitiza Mnyika.
Alisema CHADEMA inaangalia namna ya kuitisha maandamano hayo kwa kuwashirikisha vijana waliofeli kwani wanaamini wamehujumiwa.
Mnyika aliwataka Watanzania na wengine wenye uchungu na udhaifu wa elimu ya Tanzania, hasa wazazi wajitokeze kwani fedha walizowekeza kwa watoto wao kwa ajili ya elimu, zimeteketea.

Obama, JK, Ridhiwan watumika kutapeli Dar

WAKATI watanzania wengi hawajasahau machungu ya kulizwa na kampuni ya kupanda na kuvuna mbegu ya DECI, kumeibuka taasisi mpya ya fedha inayojitapa kutoa mikopo kwa njia ya mtandao, huku ikitumia vibaya majina ya Rais Jakaya Kikwete na Barack Obama wa Marekani.

Mbali ya taasisi hiyo ya Tanzania Loans Society kutumia majina ya marais hao, imewahusisha pia Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Ridhiwani Kikwete, ambapo inahofiwa kutapeli mamilioni ya walalahoi.

Taarifa za taasisi hiyo zinaonesha kuwa ilianza shughuli zake mwaka 2012, na kupata ufadhili wa fedha kutoka kwa Rais Obama, ambapo inasimamiwa na Rais Kikwete, Waziri Mkuu Pinda na mratibu mkuu ni Ridhiwani.
Watendaji wengine ni Michael John ambaye namba yake ya simu ya mkononi ndiyo inayotumika kutuma pesa za usajili.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa taasisi hiyo, imekuwa ikijitangaza kutoa huduma ya mikopo na mawasiliano ya jinsi ya kupata mikopo hiyo, hufanyika kwa njia ya mtandao ili kuwawezesha wateja wa mikoani kupata mikopo hiyo kirahisi bila usumbufu wa kuja makao makuu yao jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wananchi walioomba kupata mikopo hiyo, waliliambia gazeti hili kuwa, fomu za mikopo ya taasisi hiyo hutolewa kwa sh 15,000 ambazo nazo hulipiwa kwa njia ya mtandao.
Mmoja wa wateja wa taasisi hiyo aliyedai kutapeliwa, Maywood Maganga alisema alionja machungu baada ya kuingia kwenye tovuti yake na kukutana na maelekezo ya kumtaka ajaze fomu na taarifa zake binafsi na kisha kutakiwa kutuma sh 15,000 kwenda kwenye namba 0656 73 64 16, iliyosajiliwa kwa jina la Michael John.
Maganga alisema kuwa alifanya hivyo, na kusubiri majibu.

Kwa mujibu wa mkopo huo wenye masharti nafuu, tena usio na riba, mteja hutakiwa kurejesha na kuanza kukatwa baada ya miezi miwili tangu siku ya kupokea pesa hizo za mkopo.
“Maelezo ya mkopo huo yanaonesha kuwa una masharti nafuu sana na marejesho yake ni sh 60,000 kila mwezi bila kujali kiasi ambacho mteja amekopa.
“Maelezo ya fomu niliyojaza yalinionesha kwamba nitapata sh 300,000 kama zawadi kwa kukubali kukopa na baada ya dakika 30, ningeingiziwa kiasi cha fedha za mkopo nilizoomba,” alisema.

Yanga, Azam FC kumenyana leo

VINARA Yanga wanahitaji matokeo mazuri kwenye mchezo wao muhimu wa leo dhidi ya Azam FC ili kujiimarisha zaidi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Yanga inawakaribisha Azam wanaolingana nao kwa pointi kwenye msimamo katika mechi iliyoteka hisia za mashabiki wengi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kila timu ina pointi 36, lakini Yanga ikifaidika kileleni kutokana na tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa dhidi ya Azam inayokuja kwa kasi.

Endapo Yanga itapiga mwereka kwenye mchezo huo, basi itakuwa imeiruhusu Azam kupanda kileleni kwa mara ya kwanza katika mzunguko wa pili.
Mbali na matokeo mazuri yanayowaniwa na kila timu, upande wa pili wa mchezo huo ni Azam kuja na jaribio la kulipa kisasi baada ya mchezo wa kwanza kuogelea na kichapo cha mabao 2-0.

Ni wazi Azam itaingia uwanjani safari hii kwa lengo la kulipa kisasi ingawa Yanga nayo itapigana kuhakikisha inavuna pointi tatu na kuendeleza ubabe wake.
Mashabiki wa soka nao wana hamu ya kujua nani zaidi kati ya viungo mahiri na chipukizi, Salum ‘Sure Boy’Abubakari wa Azam na Frank Domayo wa Yanga.

Mama Kikwete kusaidia hospitali sita nchini

MWENYEKITI wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete anatarajia kukabidhi kontena la futi 40 lenye vifaa tiba vya thamani ya Sh700 milioni katika hospitali sita nchini.
 

Vifaa hivyo vya tiba ya kuzuia vifo vya mama na mtoto vilipatikana kupitia uchangishaji fedha uliofanyika katika Jimbo la Arizona nchini Marekani.

Akizungumza jana Jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa Wama, Daudi Nassib alisema lengo la taasisi hiyo kugawa vifaa hivyo ni baada ya tathmini ya huduma ya mama na mtoto iliyofanywa katika hospitali hizo. Alisema lengo la kugawa vifaa hivyo ni kuboresha maisha ya wanawake na wasichana kwenye masuala ya afya.

“Malengo ya Wama ni kusaidia kuboresha utoaji wa matumizi ya huduma bora ya afya kwa wanawake na watoto kwa jumla kupitia ugawaji vifaa kwenye hospitali zenye mahitaji makubwa,”alisema Nassib.

Nassib alivitaja vifaa vitakavyokabidhiwa katika hospitali hizo kuwa ni pamoja na Mashine ya X-Ray, Mitungi ya gesi ya Oxygen,Utra Sound, mitambo pamoja na vitanda katika vyumba vya uangalizi wa karibu(ICU),
Alisema hospitali itakayokabidhiwa vifaa hivyo ni pamoja na Hospitali ya Lugulai,Mtwara ,kitete,Tabora, Simiyu na Tumbi ya mkoani Pwani.

Katoliki waruhusu kuzuia mimba

KANISA Katoliki nchini Ujerumani limeamua kuhalalisha wanamke kutumia vidonge vya kuzuia mimba mara tu baada ya kubakwa.
Uamuzi huo umetolewa muda mfupi baada ya kutangaza kujiuzulu kwa Papa Benedict XVI mwanzoni mwa mwezi huu kwa sababu za kiafya.

Uamuzi huo umefanywa kutokana na mkutano wa viongozi wa Kanisa Katoliki nchini Ujerumani baada ya mwanamke mmoja aliyekuwa amebakwa kusema kuwa alizuiwa kufanyiwa matibabu siku mbili mfululizo katika Hospitali zinazofadhiliwa na Kanisa hilo kwa madai kuwa kuzuia mimba ni kinyume cha maongozi ya kanisa.

Maaskofu hao hatimaye walikubaliana kuwa itakuwa halali ikiwa vidonge hivyo vitatumiwa na mwanamke aliyebakwa.
kwa lengo la kuzuia kushika mimba badala ya kutoa mimba.

Hii ina maana kuwa itaweza kutumiwa tu kama kifaa cha kuzuia kushika mimba.
Vidonge hivyo hutumiwa na wanawake wengi wasiotaka kushika mimba baada ya tendo la ndoa.

Hata hivyo, Kanisa Katoliki nchini Ujerumani ambako Papa wa sasa alitoka, limegawanyika kufuatia tendo hilo la ubakaji.
Ubishi kama huo nchini Marekani haukufikia uamuzi baada ya pande zote zilizokuwa zikibishania dawa hiyo kusema kuwa ni vigumu kujua kama baada ya kitendo cha ndoa asubuhi inayofuata mwanamke ameshika mimba au la.

Serikali ya Awamu ya Nne yaongoza kukopa

TAASISI isiyo ya kiserikali ina yojishughulisha na masuala ya Madeni ya Taifa na Maendeleo (TCDD), imesema Serikali ya Tanzania ndiyo inaongoza kwa kukopa zaidi, ikieleza kuwa kati ya mwaka 2008 hadi mwaka 2011, imekopa kiasi cha Sh15trilioni na kufanya deni la taifa kufikia Sh21trilioni.
Add caption


Rais Kikwete aliingia madarakani mwaka 2005, baada ya rais aliye mtangulia, Benjamin Mkapa kumaliza kipindi chake cha uongozi wa miaka 10 kilichoanzia mwaka 1995 hadi mwaka 2005.

TCDD imebainisha kuwa Serikali inakopa fedha hizo kutoka Benki Kuu (BoT), Benki za Biashara, Kampuni za Bima na Mashirika ya Hifadhi za Jamii. Pia inakopa katika taasisi za kimataifa ikiwamo, Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo Afrika (ADB) na Shirika la Fedha Duniani (IMF).

Katika maelezo yake, Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Hebron Mwakagenda, alisema kuwa kite ndo cha Serikali kukopa fedha kwa ajili ya matumizi yasiyo muhimu pamoja na kuwalipa watumishi wake mishahara, ndiyo sababu ya kukua kwa deni hilo la taifa.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate