Sunday, May 19, 2013

VUGURU ZATOKEA MJINI IRINGA, POLISI WATUMIA MABOMU KUREJESHA AMANI.


Hivi ndivyo hali ilivyokuwa baada ya Machinga kufunga barabara kuu ya Iringa - Dodoma na ile ya Mashine Tatu mjini Iringa leo.
Hali ikiwa tete eneo hilo.

PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-


Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0 limeingiza sh. 500,390,000.
 
Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
 
Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
 
Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.
 
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81, tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 14,708,415.12.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Bill Gates is back as the world’s richest man.

bill-gates
Bill Gates has reclaimed his throne again as the richest man in the world! Latest reports from Bloomberg Billionaires Index that daily lists the world’s richest, claimed so. Guess Carlos Slim, topper on Forbes Billionaire List 2013 would be quite unhappy after having heard this piece because his fortune has seen a fall through of about $3 billion. This is owing to a bill passed by the Mexico Congress that has led Slim to loosen his grip over America Movil SAB, the largest mobile operator in the Americas.
bill-gates-and-carlos-slim-600x432
However Bill Gates, the runner up on the Forbes Billionaires List 2013 has happily climbed up to the top-most position with a recent net worth of $72.7 billion. The credit to this goes to a big-enough increase of 28% in Microsoft’s shares, though Windows 8 hasn’t fared as predicted.
Seems like Gates has impressed ‘Mother of Good Fortune’ with his philanthropic work through the Bill & Melinda Gates Foundation.
It’s after six long years that Gates has resumed his mark as the richest man.
[Via - Latimes and Bloomberg]

MBUNGE MSIGWA ATINGA ENEO LA VURUGU.



 mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akiwasili  eneo la vurugu kabla  ya kuanza kwa  vurugu  hizo 

 Mbunge Msigwa akiondoka  eneo la mashine  tatu  

TENGENEZA WEBSITE NA BLOG ZENYE MVUTO.

Tupigie simu upate Website na blog yenye muonekano wa kuvutia.Na tunafanya Blog na Website Modification kwa bei nafuu sana.

DIVA NA MWANAMITINDO KENYA WAMGOMBEA PREZOO.

Huddah Monroe

Hakuna siri tena kuwa mtangazaji wa Clouds FM Loveness aka Diva na mfalme wa bling bling Rapcellency Prezzo ni wapenzi na wote wameconfirm. Lakini hata hivyo Diva amejikuta akipata upinzani mzito kutoka kwa model na msichana maarufu nchini Kenya Huddah Monroe ambaye kulikuwepo tetesi kuwa yeye na Prezzo waliwahi kuwa wapenzi.
Huddah amemshambulia Diva kuwa anajisifia mno kwenye Twitter kuhusu uhusiano wake na Prezzo. Pia anasema Diva ana sura mbaya.

HII NDO YANGA BINGWA WA VODACOM TANZANIAPREMIER.


Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Simba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam

Kocha wa Yanga, Ernst Brandts akiwa amebebwa na wachezaji wake.

DR. FERDINAND MASAU WA TANZANIA HEART INSTITUE AFARIKI DUNIA.


 Taarifa zilizotufikia zinasema muasisi wa hospitali ya moyo ya Tanzania Heart Institue Dr. Ferdinand Masau amefariki dunia usiku wa kuamkia leo hata hivyo bado tunaendelea kufuatilia taarifa zaidi juu ya msiba huo mkubwa kwa taifa kutokana na umuhimu wa Marehemu Dr. Ferdinand Masau, Tutawaletea taarifa zaidi kadiri tutakavyozipata.
Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya marehemu Dr. Ferdinand Masau AMIN

MADAI MAZITO NISHA AHONGWA NYUMBA

Stori:Gladness Mallya-Global Publishers.
Unakumbuka zile habari za Wema Isaac Sepetu kununuliwa jumba la kifahari na bilionea mmoja Kijitonyama, Dar? Sasa zimegeukia kwa staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ambaye naye kuna madai mazito ya kuhongwa nyumba.
Ilikuwa mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo gazeti hili lilipokea ujumbe mfupi wa simu ya mkononi ‘sms’ kutoka kwa chanzo chake.
HABARI ILIVYOANZA
Chanzo: Hivi ninyi mna habari?
Risasi Jumamosi: Nyingi tu lakini kama una ya kwako itatufaa sana.
Chanzo: Kwa taarifa yenu Nisha kanunuliwa bonge la mjengo hapa Kijitonyama karibu kabisa na Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’.
Risasi Jumamosi: Nani kamnunulia?
Chanzo: Nasikia ni bilionea mmoja mwenye fedha zake hapa Dar es Salaam, kainunua kisha kamhonga Nisha kwa sababu ni mpenzi wake.
Risasi Jumamosi: Tunashukuru kwa taarifa, kaa mkao wa kula itaruka hewani mara moja baada ya upelelezi wetu.
RISASI LATUA KIJITONYAMA
Baada ya kuzinyaka habari hizo, gazeti hili lilisaga soli hadi maeneo hayo na kuanza kugonga geti moja baada ya lingine hadi lilipofanikiwa kuinasa nyumba hiyo huku Nisha akiwa ndani kapumzika.
Msichana aliyejitambulisha kuwa ni dada wa kazi au hausigeli kwa lugha laini ndiye aliyetoboa siri kuwa ni kweli staa huyo yupo ndani na amehamia mahali hapo muda si mrefu.

SEVERINE EMMANUEL AIBUKA MISS USTAWI

Miss  Ustawi 2013 Severine Emmanua (katikati), akiwa katika pozi la pamoja na mshindi namba mbili Cecilia Francis (kulia), na kushoto ni mshindi namba tatu Angela Evarist.
Washiriki wa shindano hilo wakitoa shoo ya utangulizi kabla ya mchakato wa kutafuta washindi kuanza.
Majaji wa shindano hilo wakijadiliana jambo
Hadija Kopa kushoto akimtunza Elias Barnaba, wakati akitumbuiza kwenye mpambano huo.

Shamimu Redd’s Miss Mzizima 2013

HATIMAYE taji la Redd’s Miss Mzizima 2013, lililokuwa likiwaniwa na warembo zaidi ya 15, juzi usiku lilitwaliwa na Shamimu Mohammed ndani ya ukumbi wa hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam.Katika fainali hizo zilizokuwa na msisimko wa aina yake, wanyange hao walikuwa kwenye mchuano mkali, huku wakisindikizwa na bendi ya Twanga Pepeta, ambapo majaji wa shindano hilo walichuja na kubakia warembo watano na baadaye Shamimu alitangazwa kunyakua taji hilo.
Kwa ushindi huo, Shamimu alikabidhiwa zawadi ya sofa na fedha taslimu sh 400,000.
Mshindi wa pili, nafasi hiyo ilinyakuliwa na Munira aliyepata sh 300,000 huku mshindi wa pili akiibuka Rehema Mpanda aliyejitwalia sh 200,000.

Warembo wote walioingia tano bora, watashiriki shindano la Redd’s Miss Ilala 2013.
Kwa upande wake, Msemaji wa Kampuni ya Kowack Brothers iliyoratibu shindano hilo, Aneth Makagua, alishukuru wadhamini kwa kuwaunga mkono, pamoja na wadau mbalimbali waliojitokeza katika fainali hizo.

Wadhamini wakuu wa shindano hilo ni pamoja na Club Bilicanas, Tesco Funiture, kinywaji cha Chill Will, Tanzania Daima, CXC Africa, Gogo Shop, Lakairo Investment, Lamada Hotel, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji cha Redd’s na wengineo.

Auawa kwa kupigwa risasi baa.

JESHI la Polisi Mkoa wa Kinondoni linamshikilia Conrad Leo kwa tuhuma za kumpiga risasi na kumuua Ayoub Mlay (38), wakati wakiwa katika klabu ya Ambrosia iliyoko Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wameliambia Tanzania Daima Jumapili kuwa mtuhumiwa huyo alishawahi kupokonywa silaha yake kabla ya kurudishiwa katika mazingira ya kutatanisha siku za hivi karibuni.
Inadaiwa kuwa sababu za awali zilizosababisha mtuhumiwa huyo kupokonywa silaha hiyo na Jeshi la Polisi ni pamoja na matumizi mabaya ikiwamo kuwatishia watu kila wakati wanapotofautiana kwa kauli.

Raia wa Kenya afariki dunia ghafla hotelini.

RAIA wa Kenya, Eric Njoroge Waisaka, amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha kwenye Hoteli ya Sleep Inn iliyopo mtaa wa Mahiwa na Lumumba, jijini Dar es Salaam.

Tayari ndugu wa marehemu wameshawasili jijini Dar es Salaam, kwanza kwa ajili ya kujua sababu za kifo na kushughulikia taratibu za kuuchukua mwili huo huku viongozi wa hoteli wakitupiana mpira kuzungumzia tukio la kifo chake.

Habari ambazo chanzo hiki kilizipata, zilisema kuwa raia huyo wa Kenya aliingia hotelini hapo Jumamosi iliyopita na siku iliyofuata alikutwa amekufa akiwa kwenye choo cha chumba alichofikia katika hoteli hiyo.

Meneja wa hoteli  hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Zarina, alipopigiwa simu juu ya tukio hilo alisema hayupo katika nafasi nzuri ya kuzungumzia kwa kuwa yupo msibani jijini Tanga.

“Mimi siku ya tukio nilikuwa nyumbani hivyo nimeambiwa kama wewe na kwa sasa nipo msibani, Tanga tafadhali wasiliana na ofisini watakuwa na jambo la kukueleza,” alisema Zarina.

Mkurugenzi wa hoteli hiyo, Muslim Meghy, alipopigiwa simu alisema suala hilo hawezi kulizungumzia kwa kuwa halijawa na uzito wa kuzungumziwa katika nafasi yake.
Alimweleza mwandishi wa habari hizi awasiliane na meneja na alipoambiwa kuhusu majibu ya meneja wake, mkurugenzi huyo aliomba apigiwe simu siku iliyofuata, lakini hakuweza kupokea simu yake kila alipopigiwa.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema taarifa za awali zinaonesha mtu huyo alizidiwa na shinikizo la damu.
Mwili wa marehemu ulihifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kisha kurejeshwa kwao Kenya kwa mazishi.

Ugaidi watikisa Dodoma • Waumini wapekuliwa mbele ya JK kushuhudia kusimikwa askofu.

TISHIO la ugaidi linaloikabili Tanzania limechukua sura mpya baada ya vyombo vya ulinzi kwa kushirikiana na maofisa usalama kulazimika kukesha wakifanya doria mjini hapa kuhakikisha ibada ya kusimikwa kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana (KKKT), Dk. Jacob Chimeledya inafanyika salama.

Ulinzi huo uliendelea kutwa nzima jana kuzunguka Kanisa Kuu la Anglikana mjini hapa na maeneo jirani wakati wote wa ibada hiyo iliyohudhuriwa na Askofu Mkuu wa Cantebury nchini Uingereza,   Justin Welby huku Rais Jakaya Kikwete akiwa mgeni rasmi.
Tangu juzi usiku maofisa wa polisi waliovalia sare na kiraia pamoja na wale wa usalama walikuwa wakizunguka katika mitaa mbalimbali ya mjini, kuzunguka kanisa kuu hilo huku baadhi yao wakiwa na silaha za moto na mbwa.

Wakati wote ibada ikiendelea jana, barabara ya kutoka soko kuu la Majengo kupitia hospitali ya rufaa ya mkoa ilikuwa imefungwa huku ile ya kutoka Hoteli ya Dodoma hadi Nyerere ikiwa imefurika askari waliosheheni silaha.

Tofauti na ibada nyingine za siku zote, jana waumini waliohudhuria walilazimika kupekuliwa kwa umakini zaidi na maofisa usalama na kwa waumini waliokuwa na pochi na mikoba walitakiwa kufungua na kuonesha vitu vilivyomo licha ya kupitishwa katika mashine maalumu.
Tahadhari kwa vitisho hivyo vya kigaidi imenza kuchukuliwa kwa umakini zaidi na vyombo vya dola baada ya matukio ya mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea Zanzibar kwa viongozi wa dini kushambuliwa na lile la hivi karibuni la kulipuliwa kwa Kanisa Katoliki Parokia ya Olasiti jijini Arusha.

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nalo limechukua tahadhari kwa kuwazuia wabunge kuegesha magari yao nje ya uzio wa Bunge na badala yake wawe wanayaegesha ndani au mkabala na jengo ng’ambo ya barabara ya Dodoma-Dar.
Akizungumzia vitendo hivyo vya ugaidi muda mfupi baada ya kusimikwa, Askofu Dk. Chimeledya alisema kuwa bado tatizo hilo linaonekana kuchukua nafasi kubwa, jambo ambalo linatishia amani ya Watanzania.

“Vitendo vya ugaidi vinaonekana kushamiri nchini na kulichafua taifa letu, na serikali lazima ioneshe juhudi za makusudi kuhakikisha watu ambao wanahusika na vitendo hivyo wanachukuliwa hatua.
“Hali hii ni mbaya na kwa siku za karibuni yametokea matukio mabaya sana kwa viongozi wa makanisa. Hii inasikitisha na inatia aibu kwa taifa letu ambalo limezoea amani, upendo na mshikamano,” alisema.
Alisema serikali inatakiwa kutambua kuwa hali ya kisiasa kwa sasa ni mbaya katika nchi pamoja na dunia kwa ujumla na watu wanaonekana kukata tamaa ya kuendelea kutawaliwa kutokana na kusongwa na umasikini ambao unaonekana kuwatesa.

Translate