Sunday, May 19, 2013
PAMBANO LA SIMBA, YANGA LAINGIZA MIL 500/-
Pambalo la watani wa jadi Simba na Yanga la Ligi Kuu ya Vodacom
lililochezwa jana (Mei 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam na kumalizika kwa mabingwa wapya Yanga kushinda mabao 2-0
limeingiza sh. 500,390,000.
Mechi hiyo namba 180 ambayo ilikuwa kati
ya saba la kuhitimisha ligi hiyo msimu wa 2012/2013 ilishuhudiwa na
watazamaji 57,406 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh.
7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000 na sh. 30,000.
Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,970,927.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,330,677.97.
Kiingilio
cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata
tiketi hizo walikuwa 19,039 na kuingiza sh. 95,195,000 wakati kile cha
sh. 7,000 kiliingiza watazamaji 17,647 na kupatikana sh. 123,515,000.
Mgawo
mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 63,036,064.81,
tiketi sh. 3,818,890, gharama za mechi sh. 37,821,638.88, Kamati ya Ligi
sh. 37,821,638.88, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
18,910,819.44 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)
sh. 14,708,415.12.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Bill Gates is back as the world’s richest man.

Bill Gates has reclaimed his throne again as the richest man in the world! Latest reports from Bloomberg Billionaires Index that daily lists the world’s richest, claimed so. Guess Carlos Slim, topper on Forbes Billionaire List 2013 would
be quite unhappy after having heard this piece because his fortune has
seen a fall through of about $3 billion. This is owing to a bill passed
by the Mexico Congress that has led Slim to loosen his grip over America
Movil SAB, the largest mobile operator in the Americas.

However
Bill Gates, the runner up on the Forbes Billionaires List 2013 has
happily climbed up to the top-most position with a recent net worth of
$72.7 billion. The credit to this goes to a big-enough increase of 28%
in Microsoft’s shares, though Windows 8 hasn’t fared as predicted.
Seems
like Gates has impressed ‘Mother of Good Fortune’ with his
philanthropic work through the Bill & Melinda Gates Foundation.
It’s after six long years that Gates has resumed his mark as the richest man.
MBUNGE MSIGWA ATINGA ENEO LA VURUGU.
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG ZENYE MVUTO.
DIVA NA MWANAMITINDO KENYA WAMGOMBEA PREZOO.

Huddah Monroe
Hakuna siri tena kuwa mtangazaji wa Clouds FM Loveness aka Diva na
mfalme wa bling bling Rapcellency Prezzo ni wapenzi na wote wameconfirm.
Lakini hata hivyo Diva amejikuta akipata upinzani mzito kutoka kwa
model na msichana maarufu nchini Kenya Huddah Monroe ambaye kulikuwepo
tetesi kuwa yeye na Prezzo waliwahi kuwa wapenzi.
Huddah amemshambulia Diva kuwa anajisifia mno kwenye Twitter kuhusu uhusiano wake na Prezzo. Pia anasema Diva ana sura mbaya.
Huddah amemshambulia Diva kuwa anajisifia mno kwenye Twitter kuhusu uhusiano wake na Prezzo. Pia anasema Diva ana sura mbaya.
Labels:
Diva Loveness Love
| Reactions: |
HII NDO YANGA BINGWA WA VODACOM TANZANIAPREMIER.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom baada ya kuifunga Simba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
Kocha wa Yanga, Ernst Brandts akiwa amebebwa na wachezaji wake.
Labels:
Michezo,
Yanga Bingwa 2013
| Reactions: |
DR. FERDINAND MASAU WA TANZANIA HEART INSTITUE AFARIKI DUNIA.

Taarifa zilizotufikia zinasema muasisi wa hospitali ya moyo ya Tanzania Heart Institue Dr. Ferdinand Masau amefariki dunia usiku wa kuamkia leo hata hivyo bado tunaendelea kufuatilia taarifa zaidi juu ya msiba huo mkubwa kwa taifa kutokana na umuhimu wa Marehemu Dr. Ferdinand Masau, Tutawaletea taarifa zaidi kadiri tutakavyozipata.
Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya marehemu Dr. Ferdinand Masau AMIN
MADAI MAZITO NISHA AHONGWA NYUMBA
Stori:Gladness Mallya-Global Publishers.
Unakumbuka zile habari za Wema Isaac Sepetu kununuliwa jumba la kifahari na bilionea mmoja Kijitonyama, Dar? Sasa zimegeukia kwa staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ambaye naye kuna madai mazito ya kuhongwa nyumba.
Unakumbuka zile habari za Wema Isaac Sepetu kununuliwa jumba la kifahari na bilionea mmoja Kijitonyama, Dar? Sasa zimegeukia kwa staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ambaye naye kuna madai mazito ya kuhongwa nyumba.
Ilikuwa mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo gazeti hili lilipokea ujumbe mfupi wa simu ya mkononi ‘sms’ kutoka kwa chanzo chake.
HABARI ILIVYOANZAChanzo: Hivi ninyi mna habari?
Risasi Jumamosi: Nyingi tu lakini kama una ya kwako itatufaa sana.
Chanzo: Kwa taarifa yenu Nisha kanunuliwa bonge la mjengo hapa
Kijitonyama karibu kabisa na Kituo cha Polisi cha Kijitonyama
‘Mabatini’.
Risasi Jumamosi: Nani kamnunulia?
Chanzo: Nasikia ni bilionea mmoja mwenye fedha zake hapa Dar es Salaam, kainunua kisha kamhonga Nisha kwa sababu ni mpenzi wake.
Risasi Jumamosi: Tunashukuru kwa taarifa, kaa mkao wa kula itaruka hewani mara moja baada ya upelelezi wetu.
Risasi Jumamosi: Nani kamnunulia?
Chanzo: Nasikia ni bilionea mmoja mwenye fedha zake hapa Dar es Salaam, kainunua kisha kamhonga Nisha kwa sababu ni mpenzi wake.
Risasi Jumamosi: Tunashukuru kwa taarifa, kaa mkao wa kula itaruka hewani mara moja baada ya upelelezi wetu.
RISASI LATUA KIJITONYAMABaada ya kuzinyaka habari hizo, gazeti hili lilisaga soli hadi maeneo hayo na kuanza kugonga geti moja baada ya lingine hadi lilipofanikiwa kuinasa nyumba hiyo huku Nisha akiwa ndani kapumzika.
Msichana aliyejitambulisha kuwa ni dada wa kazi au hausigeli kwa lugha laini ndiye aliyetoboa siri kuwa ni kweli staa huyo yupo ndani na amehamia mahali hapo muda si mrefu.

SEVERINE EMMANUEL AIBUKA MISS USTAWI
Shamimu Redd’s Miss Mzizima 2013
HATIMAYE taji la Redd’s Miss Mzizima 2013, lililokuwa likiwaniwa
na warembo zaidi ya 15, juzi usiku lilitwaliwa na Shamimu Mohammed
ndani ya ukumbi wa hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam.Katika fainali hizo zilizokuwa na msisimko wa aina yake, wanyange hao
walikuwa kwenye mchuano mkali, huku wakisindikizwa na bendi ya Twanga
Pepeta, ambapo majaji wa shindano hilo walichuja na kubakia warembo
watano na baadaye Shamimu alitangazwa kunyakua taji hilo.
Kwa ushindi huo, Shamimu alikabidhiwa zawadi ya sofa na fedha taslimu sh 400,000.
Mshindi wa pili, nafasi hiyo ilinyakuliwa na Munira aliyepata sh
300,000 huku mshindi wa pili akiibuka Rehema Mpanda aliyejitwalia sh
200,000.
Warembo wote walioingia tano bora, watashiriki shindano la Redd’s Miss Ilala 2013.
Kwa upande wake, Msemaji wa Kampuni ya Kowack Brothers iliyoratibu
shindano hilo, Aneth Makagua, alishukuru wadhamini kwa kuwaunga mkono,
pamoja na wadau mbalimbali waliojitokeza katika fainali hizo.
Wadhamini wakuu wa shindano hilo ni pamoja na Club Bilicanas, Tesco
Funiture, kinywaji cha Chill Will, Tanzania Daima, CXC Africa, Gogo
Shop, Lakairo Investment, Lamada Hotel, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),
kupitia kinywaji cha Redd’s na wengineo.
Auawa kwa kupigwa risasi baa.
JESHI la Polisi Mkoa wa Kinondoni linamshikilia Conrad Leo kwa
tuhuma za kumpiga risasi na kumuua Ayoub Mlay (38), wakati wakiwa katika
klabu ya Ambrosia iliyoko Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wameliambia Tanzania Daima Jumapili
kuwa mtuhumiwa huyo alishawahi kupokonywa silaha yake kabla ya
kurudishiwa katika mazingira ya kutatanisha siku za hivi karibuni.
Inadaiwa kuwa sababu za awali zilizosababisha mtuhumiwa huyo
kupokonywa silaha hiyo na Jeshi la Polisi ni pamoja na matumizi mabaya
ikiwamo kuwatishia watu kila wakati wanapotofautiana kwa kauli.
Raia wa Kenya afariki dunia ghafla hotelini.
RAIA wa Kenya, Eric Njoroge Waisaka, amefariki dunia katika
mazingira ya kutatanisha kwenye Hoteli ya Sleep Inn iliyopo mtaa wa
Mahiwa na Lumumba, jijini Dar es Salaam.
Tayari ndugu wa marehemu wameshawasili jijini Dar es Salaam, kwanza
kwa ajili ya kujua sababu za kifo na kushughulikia taratibu za kuuchukua
mwili huo huku viongozi wa hoteli wakitupiana mpira kuzungumzia tukio
la kifo chake.
Habari ambazo chanzo hiki kilizipata, zilisema kuwa raia huyo wa Kenya
aliingia hotelini hapo Jumamosi iliyopita na siku iliyofuata alikutwa
amekufa akiwa kwenye choo cha chumba alichofikia katika hoteli hiyo.
Meneja wa hoteli hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Zarina,
alipopigiwa simu juu ya tukio hilo alisema hayupo katika nafasi nzuri ya
kuzungumzia kwa kuwa yupo msibani jijini Tanga.
“Mimi siku ya tukio nilikuwa nyumbani hivyo nimeambiwa kama wewe na
kwa sasa nipo msibani, Tanga tafadhali wasiliana na ofisini watakuwa na
jambo la kukueleza,” alisema Zarina.
Mkurugenzi wa hoteli hiyo, Muslim Meghy, alipopigiwa simu alisema
suala hilo hawezi kulizungumzia kwa kuwa halijawa na uzito wa
kuzungumziwa katika nafasi yake.
Alimweleza mwandishi wa habari hizi awasiliane na meneja na
alipoambiwa kuhusu majibu ya meneja wake, mkurugenzi huyo aliomba
apigiwe simu siku iliyofuata, lakini hakuweza kupokea simu yake kila
alipopigiwa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi, amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo na kusema taarifa za awali zinaonesha mtu huyo
alizidiwa na shinikizo la damu.
Mwili wa marehemu ulihifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kisha kurejeshwa kwao Kenya kwa mazishi.
Ugaidi watikisa Dodoma • Waumini wapekuliwa mbele ya JK kushuhudia kusimikwa askofu.
TISHIO la ugaidi linaloikabili Tanzania limechukua sura mpya
baada ya vyombo vya ulinzi kwa kushirikiana na maofisa usalama
kulazimika kukesha wakifanya doria mjini hapa kuhakikisha ibada ya
kusimikwa kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana (KKKT), Dk. Jacob
Chimeledya inafanyika salama.
Ulinzi huo uliendelea kutwa nzima jana kuzunguka Kanisa Kuu la
Anglikana mjini hapa na maeneo jirani wakati wote wa ibada hiyo
iliyohudhuriwa na Askofu Mkuu wa Cantebury nchini Uingereza, Justin
Welby huku Rais Jakaya Kikwete akiwa mgeni rasmi.
Tangu juzi usiku maofisa wa polisi waliovalia sare na kiraia pamoja na
wale wa usalama walikuwa wakizunguka katika mitaa mbalimbali ya mjini,
kuzunguka kanisa kuu hilo huku baadhi yao wakiwa na silaha za moto na
mbwa.
Wakati wote ibada ikiendelea jana, barabara ya kutoka soko kuu la
Majengo kupitia hospitali ya rufaa ya mkoa ilikuwa imefungwa huku ile ya
kutoka Hoteli ya Dodoma hadi Nyerere ikiwa imefurika askari
waliosheheni silaha.
Tofauti na ibada nyingine za siku zote, jana waumini waliohudhuria
walilazimika kupekuliwa kwa umakini zaidi na maofisa usalama na kwa
waumini waliokuwa na pochi na mikoba walitakiwa kufungua na kuonesha
vitu vilivyomo licha ya kupitishwa katika mashine maalumu.
Tahadhari kwa vitisho hivyo vya kigaidi imenza kuchukuliwa kwa umakini
zaidi na vyombo vya dola baada ya matukio ya mashambulizi ya kigaidi
yaliyotokea Zanzibar kwa viongozi wa dini kushambuliwa na lile la hivi
karibuni la kulipuliwa kwa Kanisa Katoliki Parokia ya Olasiti jijini
Arusha.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nalo limechukua tahadhari kwa
kuwazuia wabunge kuegesha magari yao nje ya uzio wa Bunge na badala
yake wawe wanayaegesha ndani au mkabala na jengo ng’ambo ya barabara ya
Dodoma-Dar.
Akizungumzia vitendo hivyo vya ugaidi muda mfupi baada ya kusimikwa,
Askofu Dk. Chimeledya alisema kuwa bado tatizo hilo linaonekana kuchukua
nafasi kubwa, jambo ambalo linatishia amani ya Watanzania.
“Vitendo vya ugaidi vinaonekana kushamiri nchini na kulichafua taifa
letu, na serikali lazima ioneshe juhudi za makusudi kuhakikisha watu
ambao wanahusika na vitendo hivyo wanachukuliwa hatua.
“Hali hii ni mbaya na kwa siku za karibuni yametokea matukio mabaya
sana kwa viongozi wa makanisa. Hii inasikitisha na inatia aibu kwa taifa
letu ambalo limezoea amani, upendo na mshikamano,” alisema.
Alisema serikali inatakiwa kutambua kuwa hali ya kisiasa kwa sasa ni
mbaya katika nchi pamoja na dunia kwa ujumla na watu wanaonekana kukata
tamaa ya kuendelea kutawaliwa kutokana na kusongwa na umasikini ambao
unaonekana kuwatesa.
Subscribe to:
Posts (Atom)
HABARI MBALIMBALI
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
Amanda Poshy
Aunt Ezekiel
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
Belle 9
BI KIDUDE
Big Brother Africa
Bill Gates
CCM
CHADEMA
Chombezo
Club Bilicanas
Dayna Nyange
Diamond
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DSTV
Elizabeth Michael
Hemedy Suleiman
IRENE PAUL
Irene Uyoya
J film 4 life
Jack Chuz
JACQUELINE WOLPER
Jay Dee
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
Kapotive Star Singers
Kero Zetu
Lady Jaydee
Linah Sanga
Linex
Loveness Diva
Magazeti
Mahusiano
Makala
MAMTEI
MARIAM ISMAIL
Matangazo
mic
Michezo
Miss East Africa
MISS USTAWI
Mrisho Ngassa
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Necta
Nisha
Nyota yako
RACHEL NDAUKA
Ray
Ray C
Redds Miss wa Mikoa
Redd’s Miss IFM
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
Saikolojia
SAJUKI
Sandra
Shamsa Ford
Shilole
Snura Mushi
staa
Staa Wetu
Twanga Pepeta
Wastara
WEMA SEPETU
Yanga Bingwa 2013
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’

